Ni dharau kubwa Kiongozi wa Taifa letu kutoa risala huko Brazil wakati wanaotakiwa kusikiliza wanaendelea na shughuli za kupakua chakula

Ni dharau kubwa Kiongozi wa Taifa letu kutoa risala huko Brazil wakati wanaotakiwa kusikiliza wanaendelea na shughuli za kupakua chakula

Kuna wazo linaniingia akilini kukuhusu wewe.
Nipoteze muda wa kumweka kijana 'intern', apitie michango yako humu JF; na hasa kumhusu huyu, na kuifanyia udadavuzi kuelewa akili yako ilivyo lala kwa sehemu kubwa unapo changia. Jikumbushe vimistari miwili mitatu ulivyo andika wakati akiondoka kwenda kwenye mkutano huo.

Sasa sina hakika, kama kazi hiyo ya huyo kijana itakuwa na manufaa yoyote!
 
Hata Mkapa ni uongo,maana naye speech zake zilikuwa za kusoma.
Mtu pekee aliweza ni nyerere maana speech nyingi alikuwa hasomi anatoa kichwani.
Linganisha hotuba ya kusoma ya Che Nkapa, na hotuba ya kusoma ya Jpm, au Ssh. Ni sawa na bahari ya hindi, dhidi ya kudimbwi.
 
Nimepitia risala alotoa mheshimiwa Rais wetu huko Brazil sijapenda the way walivyo mpa sikio,

Watu wameonekana Kama vile hawana muda na anachozungumza, wanazunguka na sahani za Chakula,

Ni Kama kwenye sherehe wakati wa chakula wanaweka kibwagizo!

View: https://x.com/swahilitimes/status/1858937943106159057?s=46&t=wVwOX7Oilw0E0zILKPC7xg

Ningekuwa Rais ningesema kwanza Naomba msikilize nasema nini

Britanicca

Hiyo magufuri ndo alikuwa na uwezo huo.

Alimpiga stop mkalimani huko Kenya asitafisiri hotuba yake Kwa kiingereza
 
Sasa mtu mwenyewe ni masikini wa Kila kitu utamsikiliza nini?.kitendo tu Cha kuwaacha wananchi wakiwa wameangukiwa na jengo kariakoo na kwenda huko kujikombakomba tayari kaon esha umasikini wa hali ya juu ndiyo maana wazungu hawana muda na kusikiliza hotuba yake.Vinalia vijiko tu lakini hotuba yake haisikiki hata kidogo
 
Hakuna mtu mwenye akili timamu atapoteza muda wake kumsikia kiongozi kutoka bara la kiza,ambaye anapata misaada ya ujenzi wa vyoo na wakati huo huo anatumia 500b kununua magari ya kifahari na 200b kuwalipa Wabunge wa vitu maalum.

Mabeberu huwa wanajua kuwa nyoosha viongozi wa Afrika,hasa wakiwa kwenye mataifa Yao kwamba wewe si chochote si lolote umungu mtu ni uko kwa wajinga na wapumbavu.
Mkuu sio kweli, mbona asilimia kubwa walikuwa wanamsikiliza.
 
Si mnapenda kujikomba nchi hii diplomasia na ushawishi kwenye mikutano mikubwa aliweza Nyerere na Mkapa

The rest hamna kitu

Kikwete angalu alijitahidi kwenye msiba wa Mandela

Nyerere alikuwa akihutubia UN wazungu wanasimama na kumpigia makofi kabisa

Mkapa alikuwa na hotuba zilizonyooka alikuwa amepikwa kweli kuwa Rais wa nchi.

Mwinyi, Magufuli, Samia Hawa kwenye hotuba hamna kitu

Hotuba inahitaji ipitiwe na ichakatwe na wataalamu sio unaamka tu una hasira na mmeo au mkeo unaanza kuongea mambo ambayo hayapo hapo ndio tunapofeli hakuna Kama vile sheikh kuhubiri habari za Mtume kanisani siku ya krismas au askofu kumhubiri Kristo msikitini siku ya idi.
Matajiri wako ktk kikao chao, agenda "Kuwatawala maskini" alafu ghafla anaingia ombaomba na kopo lake akipaza sauti "...saidia maskini ...nk".
Wkt wa Mwalimu, akisimama kuhutubia, hata kama mtu alibanwa anaena msalani, anaahirisha mpaka amsikilize kwanza. Na walikua wakimtafta, wajifunze toka kwake.
Yalotokea Brazil liwe fundisho kama tunafundishika
 
Back
Top Bottom