Ni dharau kubwa Kiongozi wa Taifa letu kutoa risala huko Brazil wakati wanaotakiwa kusikiliza wanaendelea na shughuli za kupakua chakula

Kuna wazo linaniingia akilini kukuhusu wewe.
Nipoteze muda wa kumweka kijana 'intern', apitie michango yako humu JF; na hasa kumhusu huyu, na kuifanyia udadavuzi kuelewa akili yako ilivyo lala kwa sehemu kubwa unapo changia. Jikumbushe vimistari miwili mitatu ulivyo andika wakati akiondoka kwenda kwenye mkutano huo.

Sasa sina hakika, kama kazi hiyo ya huyo kijana itakuwa na manufaa yoyote!
 
Hata Mkapa ni uongo,maana naye speech zake zilikuwa za kusoma.
Mtu pekee aliweza ni nyerere maana speech nyingi alikuwa hasomi anatoa kichwani.
Linganisha hotuba ya kusoma ya Che Nkapa, na hotuba ya kusoma ya Jpm, au Ssh. Ni sawa na bahari ya hindi, dhidi ya kudimbwi.
 
Hiyo magufuri ndo alikuwa na uwezo huo.

Alimpiga stop mkalimani huko Kenya asitafisiri hotuba yake Kwa kiingereza
 
Sasa mtu mwenyewe ni masikini wa Kila kitu utamsikiliza nini?.kitendo tu Cha kuwaacha wananchi wakiwa wameangukiwa na jengo kariakoo na kwenda huko kujikombakomba tayari kaon esha umasikini wa hali ya juu ndiyo maana wazungu hawana muda na kusikiliza hotuba yake.Vinalia vijiko tu lakini hotuba yake haisikiki hata kidogo
 
Mkuu sio kweli, mbona asilimia kubwa walikuwa wanamsikiliza.
 
Matajiri wako ktk kikao chao, agenda "Kuwatawala maskini" alafu ghafla anaingia ombaomba na kopo lake akipaza sauti "...saidia maskini ...nk".
Wkt wa Mwalimu, akisimama kuhutubia, hata kama mtu alibanwa anaena msalani, anaahirisha mpaka amsikilize kwanza. Na walikua wakimtafta, wajifunze toka kwake.
Yalotokea Brazil liwe fundisho kama tunafundishika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…