Ni dharau kubwa Kiongozi wa Taifa letu kutoa risala huko Brazil wakati wanaotakiwa kusikiliza wanaendelea na shughuli za kupakua chakula

Magufuli alitoa hotuba ya corona dunia nzima iliyikisika, hadi Trump akaitisha maombi
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜‚πŸ˜‚ Niliuliza hapa hapa... Ameenda kufanya Nini??? Chawa MMOJA akanitukana kuwa Nina wivu na chuki kwa maisha ya watu.πŸ™ŒπŸ™Œ

We watu wamekufa na wengine wapo chini ya kifusi unaona sawa unasafiri. Kwa staili hii wazungu wataendelea kutuona manyani hasa na ni sawa TU....
 
Kule kuna watu wanasikiliza mambo ya maana sio kusikiliza ngonjera aliyoandikiwa na na Waziri na Steve Nyerere
 
Ndo maana mm huwa nasema huyu rais wetu tubadilishane na Rais wa Equatorial Guinea huyu aende kule yule wa kule aje huku.
 
Wamueshimu kwa lipi?
Anatumia cheo cha dokta wakati hajasoma PHD darasa ni, hapo tu, anaonekana kilaza,nchi yake inanuka rushwa, u tawala usiofsta sheria, mauaji ya wapinzani,
Wao wanamuona kama yule Rais Shekh Having aliyekimbia nchi yake baada ya wananchi kuandamana!

Wakubwa wanatushangaa tunaongozwaje na mtu mwenye akili ndogo kama huyo, kwa ufupi ni aibu tupu, analiaibisha Taifa
 
Ila haters wa Samia wanahangaika aisee, dah! Poleni sana lakini ndo hivyo hamtokuja mfanane nae hata siku Moja nyie tumbiri.......ameshawapiga gepu amewapiga tu. Mlicjobako ni kizisja tu hili na lile kutwa kucha, hebu tuonyesheni na speech za watu wengine kwanza.
 
Sema nini'? Haters wa Samia mmekuwa kama wake wenzake, mna gubu kweli kweli na vijembe vya vidole juu.
 
Acha uongo.

HAKUNA aliposema anawasihi mataifa tajiri yatambue na kutumia fursa zilizopo Africa.

Ametumia risala hiyo kuomba misaada na kusema dunia sio fair, Afrika tuna njaa na utapiamloa, magonjwa, ni masikini wa kutupwa, hatuna mashine za kilimo, wala mbolea, wala utafiti, na tuna madeni, na ushindani wa dunia ni mkali sana.

Halafu akasema bado tunasubiri ahadi ya mafanikio itakayoletwa na globalization.

Hivi nchi tajiri zilituahidi kwamba globalization itatutoa ???

Na zilitusukuma tuingie kwenye globalization ?

Waingereza ndio waliwaambia Waafrika wakafuate mataka taka kama ma ndala na ma vikombe ya plastiki CHINA badala ya kujifunza kuvizalisha nyumbani kuokoa foreign currency ???

Watu wanakula, sisi tunapita na bakuli kutangaza umasikini. Basi angeenda na ndege commercial, tiketi daraja la tatu, sio kwa luxury class kwenye ndege kapanda mwenyewe, too expensive! Wangemuelewa na wangemheshimu zaidi.
 
Lakini kiukweli kabisa huyo mama ataongea kitu gani cha kusikilizwa na watu wa G20
 
Hotuba za waalikwa ambao hawapo kwenye umoja rasmi hua mara nyingi ni muda wa chai, muda wa chakula cha mchana au kwenye mapumziko, hawawezi kuwapa muda rasmi ambapo wao hutumia kujadili mambo yao ya msingi na hao waalikwa hubaki kama watumbuizaji , kama kwenye ngumi kuna wale watu wa amsha amsha kabla ya pambano rasmi
 
Kimsingi huna hoja unatafuta attention,is like wewe ni mgeni wa kwenye mikutano 😁😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…