Ni halali Wazanzibari kufanya kazi za Watanganyika?

Ni halali Wazanzibari kufanya kazi za Watanganyika?

Uzi wa kibaguzi na uliokosa mashiko. Kama mzanzibar kaoa au kaolewa huku bara huyo mtoto anayezaliwa abaguliwe kwa sababu ya wazazi wake?.

Mada nyepesi inayokwenda kinyume na tamaduni za kitanzania inaweza kuvunja mshikamano wetu badala ya kuufanya ukawa imara.
Uzi una mantiki sana nashangaa hujibu hoja umeingiza mambo yasiyokuwepo

1. Mtoto anayezaliwa na wazazi wa pande mbili ni Mtanzania. Tatizo linakuja kwamba Mtanzania ni Mtu wa bara halafu kuna Mzanzibar. Mtoto huyo anabaguliwa na Wazanzibar kwasababu ya huo Uzanzibar.

2. Hoja ya Allen Kilewella : yapo mambo Wazanzibar wanalamika si ya muungano.

21% ajira zilizotengwa kwa Wazanzibar ni pamoja na mambo yasiyo ya muungano, je hiyo ni kuwatendea haki Watanganyika ambao hawana fursa hiyo Zanzibar?

Hivyo unatakiwa kujibu hoja za mleta mada si kugundua hoja nje ya mada.

Kwa lugha rahisi Wazanzibar wanalaani kuongezwa kwa mambo ya muungano kama elimu ya juu, lakini wapo bodi ya mkiopo ya elimu ya juu na wanapewa kutoka HESLB. Je Mtanganyika anapewa ZHESLB?

Hapa ni kwamba Wazanzibar wanasema '' Nguruwe ni haramu lakini mchuzi wake ni halali''

Tunakuuliza wewe, je hiyo ni sawa?
 
Nawaza sana mantiki ya kwenda kujenga Ikulu ndogo Zanzibar, ofisi ya Makamu wa Rais, na cha kustaajabisha sana ofisi ya waziri Mkuu. Hivi Waziri Mkuu ni mambo ya Muungano?? Hivi hawajui ni kwa nini tuna Waziri Mkuu kwenye serikali ya Muungano Tanzania?

iko siku tutakuwa na Waziri Mkuu toka Zanzibar na watanganyika watakaa kimya.
 
Duh!

Hata Jumbe mwenyewe niliyemtaja hapo juu; si ni akina Maalim waliomchomea utambi?

Kwa hiyo mambo yanaanzia huko huko kwa waZanzibari wenyewe?

Hata hivyo, sina mfano, na sijui kama unao mfano wewe, mahsusi wa waZanzibari walioko CCM, waliokomalia jambo ambalo CCM ya waTanganyika hawakulitaka na wakafanikiwa kulipitisha walivyotaka wenyewe bila ya baraka za CCM Tanganyika.
Bendera na Katiba ya Zanzibar?
Hata masheikh wa uamsho walisalitiwa na Wazanzibar wenzao waliokuwa madarakani
 
Nawaza sana mantiki ya kwenda kujenga Ikulu ndogo Zanzibar, ofisi ya Makamu wa Rais, na cha kustaajabisha sana ofisi ya waziri Mkuu. Hivi Waziri Mkuu ni mambo ya Muungano?? Hivi hawajui ni kwa nini tuna Waziri Mkuu kwenye serikali ya Muungano Tanzania?

iko siku tutakuwa na Waziri Mkuu toka Zanzibar na watanganika watakaa kimya.
Tumewahi kuwa naye.
Salim Ahmed Salim amewahi kuwa waziri mkuu
 
Uzi wa kibaguzi na uliokosa mashiko. Kama mzanzibar kaoa au kaolewa huku bara huyo mtoto anayezaliwa abaguliwe kwa sababu ya wazazi wake?.

Mada nyepesi inayokwenda kinyume na tamaduni za kitanzania inaweza kuvunja mshikamano wetu badala ya kuufanya ukawa imara.

wewe utakuwa mzanzibar , nyie ndio wabaguzi mkiambiwa ukweli mnaleta eti suala la mshikamano.
Ubaguzi wenu zidi ya wabara lazima uanikwe na upingwe kwa nguvu zote ikibidi hata kwa kuvunja huu Muungano wewe na wenzako wote akina bakharesa, samia suluhu hasan na wapemba waliojazana kkoo mrudi kwenu mkija bara muombe visa.
Hii biashara ya chetu chetu, chenu chetu ni upuudhi uliopitiliza
 
Aiseeee!

Naona umevamia mada bila kuelewa kinachojadiliwa.

Ni nani anayembagua mwenzake kati ya pande mbili za Muungano. Hili nalo hulijui wala hulioni?

Haya yanayofanyika sasa hivi ndiyo unayodhani yataufanya Muungano kuwa "imara". Unaelewa maana ya hilo neno "imara" kweli, au unajiandikia tu?
Huyu jamani ni mpemba itakuwa ni mmoja wapo wa wanufaika wa huu upuuzi anaelewa kila kitu anajifanya kujitoa ufahamu
 
Swali la ku muuliza nyerere Na wazee wa zamani hili walio fanya hili kwa hapa sidhani kama utapata jibu sahihi[emoji28][emoji28]
Sio sahihi kusubiri wazazi waliokwenda mbele ya haki warudi kukurekebishia nyumba waliyokuachia eti kwa sababu hawakuijenga vizuri !! Fanyieni ukarabati hiyo nyumba mlioachiwa vinginevyo itakuja kuwaangukia siku moja !!
 
Kwa lugha rahisi Wazanzibar wanalaani kuongezwa kwa mambo ya muungano kama elimu ya juu, lakini hao hao wapo bodi ya mkiopo ya elimu ya juu na wanapewa bure (hawakopi) kutoka HESLB
Mkuu kuna mambo ama huyajui au jazba imepanda mno. Wazanzibari, kama Watanzania wengine, wanapata mikopo kutoka HESLB na wanalipa. Lakini haya mambo ya kuambiwa nawe ongeza yako.
 
Nawaza sana mantiki ya kwenda kujenga Ikulu ndogo Zanzibar, ofisi ya Makamu wa Rais, na cha kustaajabisha sana ofisi ya waziri Mkuu. Hivi Waziri Mkuu ni mambo ya Muungano?? Hivi hawajui ni kwa nini tuna Waziri Mkuu kwenye serikali ya Muungano Tanzania?

iko siku tutakuwa na Waziri Mkuu toka Zanzibar na watanganika watakaa kimya.
Kuna mambo yanafanyika yanatia shaka mantiki yake.

Hakuna sababu za kujenga ikulu hizo kuongeza mzigo kwa mlipa kodi.

Majuzi Rais anasema Zanzibar iwe special zone ya police kwasababu ya nature yake.
Hivi Zanzibar inapakana na nchi ngapi?Tanganyika inapakana na nchi 8 inahitaji resources zaidi .
Kwanini special zone Zanzibar na siyo Mtwara ?

Haya yanatokea kwasababu hakuna mtu anayesimamia masilahi ya Tanganyika.

Watanganyika wanabeba muungano 100%. Kwenye vikao vya kero wanwakilishwa na nani?r

Ipo siku tutamuuliza Philip na hili linaweza hitimisha ndoto yake. Ataulizwa alisimamiaje Tanganyika?

G55 waliona mambo kama haya! siku hizi kule mjengo wamelala wakiamka wanaimba na kusifu
 
Mungelijua yalio kwenye mioyo ya wazanzibari, basi nadhani watanganyika msingekuwa mkija na thread kama hizi. Ukweli ukienda Zanzibar kila corner ya km kama 25 basi unapita kwenye checkpoint ya vyombo vya usalama vya Tanganyika (sawa na wapalestina).

Sasa ifike wakati tuheshimiane bana, mkiona kama mshachoka vunjeni. Huku hatuwezi kupigana na Tanganyika kwa hiyo tunawasubiri nyie huko ndio mlioshika mpini wa vyombo vya dola.

Kama mlivyokuja kupindua mkatuu na babu yenu Nyerere basi na sasa vunjeni tuu. Msianze kutuchosha na mathread ya sio na kichwa wala miguu.
 
Mungelijua yalio kwenye mioyo ya wazanzibari, basi nadhani watanganyika msingekuwa mkija na thread kama hizi. Ukweli ukienda Zanzibar kila corner ya km kama 25 basi unapita kwenye checkpoint ya vyombo vya usalama vya Tanganyika (sawa na wapalestina).

Sasa ifike wakati tuheshimiane bana, mkiona kama mshachoka vunjeni. Huku hatuwezi kupigana na Tanganyika kwa hiyo tunawasubiri nyie huko ndio mlioshika mpini wa vyombo vya dola.

Kama mlivyokuja kupindua mkatuu na babu yenu Nyerere basi na sasa vunjeni tuu. Msianze kutuchosha na mathread ya sio na kichwa wala miguu.
Ulinzi ni jambo la Muungano. Kaa kimya.

Huku bara hakuna anayehoji makamanda na maaskari toka Zanzibar walioko Tanganyika. Tunachohoji ni kwa nini Mambo na kazi za Watanganyika zifanywe na wanzibari?
 
Nguruvi3 maslahi ya Tanganyika si yanasimamiwa na Waziri Mkuu, mbona Kassim Majaaliwa yupo kimya?
Waziri mkuu si anawekwa na Rais, anaweza kuondolewa wakati wowote. Hana kauli yoyote ile
Tanganyika ingalikuwa na kiongozi anayewajibika kwake, haya yasingetokea
Tanganyika hiyo hiyo ndiyo imebeba gharama za muungano 100%!
 
Mkuu Allen Kilewella , kwanza kazi ni kazi, hakuna kazi ya mtu, hivyo hakuna kazi za Mtanzania wala kazi ya Mzamzobari, kazi ni ya wote. Pili hiki ulichokileta ni ubaguzi wa kutaka kuwabagua Wazanzibari!. Mwalimu Nyerere alisema hii ni dhambi!. Kiukweli somo la uraia linahitajika sana Tanzania kwa watu kama wewe!. Tanzania ni nchi moja, ya JMT, yenye uraia mmoja tuu wa Tanzania, kila Mtanzania ana haki sawa na haki zote za raia wa Tanzania.

Ndani ya uraia wa Tanzania kuna uraia mmoja tuu wa Mtanzania.

Kwa vile Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndani ya JMT kuna sehemu moja ya Zanzibar ina utawala wake wa ndani ambao Wazanzibari licha ya kwanza kuwa ni raia wa JMT wenye haki zote za uraia wa JMT, hawa wamepewa haki za ziada za ukaazi wa Zanzibar. Kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar sio kitambulisho cha uraia, hakuna uraia wa Zanzibar kuna uraia mmoja tuu wa JMT na ziada ya ukaazi wa Zanzibar.

Hivyo Wanzanzibari wana haki zote za uraia wa Tanzania na ziada ya haki za ikaazi wa Zanzibar.

Lile jambo langu likitimia, nafungua darasa la bure la Haki, kuwaelimisha Watanzania haki zao mbalimbali zikiwemo haki za uraia.
P
Kama ni hivyo kwann mtanzania bara haruhusiwi nunua ardhi Zanzibari kama kweli sisi wote ni uraua mmoja ambao ni JMT????
 
Nguruvi3 wakati mwingine nikiwaza nguvu ya waziri mkuu huwa najiuliza nguvu yake bungeni. Ukiangalia hakuna wakati Bunge la Tanzania linajadili mambo mahsusi ya Tanganyika. Kila wakati wakati tunajadili mambo ya Nanjilinji Kilwa, na mbunge wa kiembesamaki naye anachangia. Ila wao kwenye baraza la wawakilishi hakuna Mtanganyika anayejadili mambo yao.
 
Kama ni hivyo kwann mtanzania bara haruhusiwi nunua ardhi Zanzibari kama kweli sisi wote ni uraua mmoja ambao ni JMT????
Tatizo linaanza pale mnapojiita watanzania bara badala ya watanganyika.
 
Ulinzi ni jambo la Muungano. Kaa kimya.

Huku bara hakuna anayehoji makamanda na maaskari toka Zanzibar walioko Tanganyika. Tunachohoji ni kwa nini Mambo na kazi za Watanganyika zifanywe na wanzibari?
Nenda Jozani pale utakutana na kina Sara na Josephu wanafanya kazi kwenye taasisi ya utalii. Mambo ya muungano hayajulikani tena, but I hope Jozani sio taasisi ya muungano.
 
Back
Top Bottom