Ni kwanini wilaya ya Kigamboni maendeleo yapo taratibu sana?

Ni kwanini wilaya ya Kigamboni maendeleo yapo taratibu sana?

1.Kutoka Pugu-Pugu Kajiungeni-Majohe-Buyuni-Chanika-Mvuti hadi Msongola,
0.Barabara ya lami ni moja.
2.Hakuna hata stendi za mabasi
3.Hakuna connection ya maji safi ya Dawasco ipo chini.
4.Hakuna hospitali kubwa ya serikali wala binafsi.
5.Nyumba zimejengwa ovyo, nyingi zina nyufa.
6.Barabara za mitaa ni mbovu balaa,
7.Mmonyoko mwingi wa udongo
8.Hakuna sehemu nzuri za starehe.
9.Hakuna chuo hata kimoko.
10.Mahitaji makubwa katika maduka mpaka Gongo la Mboto.
11.matawi ya Benki ni mawili.
12.Kuna mashamba ya Mpunga, Mihogo na viazi vitamu.
13.kuna mapori kibao tu (Majohe,Buyuni,Zingiziwa,Mvuti)
14.Hata maeneo ya makabuli ni hayaeleweki.


Sasa mnaposema Kigamboni ipo nyuma, sijui Chanika pame endelea ,mtuambie na vigezo mlivyotumia.
 
Hapa nimekuelewa sana Kaka
Ni kweli hata mimi ningependa kufanya nachotaka kwenye nyumba yangu
Kama mie ninapoishi kuna eneo ndani la mita 15x15 limebaki nimeanzisha ufugaji wa samaki wa biashara na kuku pembeni nimepanda mbogamboga kama zote.
Hivyo about mboga hatuhangaiki familia nzima maana hii bongo kununua mabroiler waweza lishwa vibudu.
 
Wewe hujui Avic town iko wapi. Muongozo hapo hata Dege hujafika. Dege iko 20+km,ukitoka Dege unafika Mwembe mdogo, ukitoka Mwembe mdogo kuna Cheka ndio uifikie Avic town,hata lami haijafika. Over 30km from Feri.
Sasa watu wamejenga Bunju B,Ununio,Mbweni Teta ambako ni Km za kutosha tu kutoka Magomeni au Kariakoo.
 
Aisee kweli kumepangika, naona mitaa yote square, yaani barabara zinapita kimpangilio

1709500571201.png
 
Wewe hujui Avic town iko wapi. Muongozo hapo hata Dege hujafika. Dege iko 20+km,ukitoka Dege unafika Mwembe mdogo, ukitoka Mwembe mdogo kuna Cheka ndio uifikie Avic town,hata lami haijafika. Over 30km from Feri.
Unabishana na wenyeji mkuu??
Kutoka feri mpaka Avic ni 25kilometres.
Na pretoria Hotel hufiki hata Cheka.
Kama unaijua ilipo pretoria hotel basi ni karibu na Avic town.
Na Mwongozo ni kubwa sio ndogo.
 
Avic town nyumba zinauzwa 200m, hakuna chochote nje ya compound yao. Sasa Bunju na Mbweni kuko kama Avic town? Wewe unafikiri kwanini watu hawanunui hizo nyumba?
Sasa mkuu, kwa hilo tu ,nenda
-Palm village (kwa Warioba)
-Dar villa (Msasani near Mayfair)
-Morocco square (Mikocheni Morocco)
na Masaki kuna apartments kibao hazina wateja.
Mkuu soko la apartments ni Jiji zima halipo vizuri kwa miaka 7 hii.
Hata Majengo makubwa ya maofisi hayana wateja. Hata majengo ya Supermarket.
 
Kijana, nina viwanja na nimejenga nyumba kadhaa za wanafunzi wa chuo cha afya kigamboni. Naenda huko kila weekend. Ni 26km kutoka Feri. Chuo kiko mbele kidogo ya Mwembe mdogo kabla ya Cheka. Ukitoka Cheka ndio unaenda Avic town. Usibishe tu kutafuta kushinda.
Mie hiko chuo cha Kigamboni city college nakijua vizuri tu tena ni mbele kidogo ya mwembe mdogo.
Umezunguka njia ,njia ulopita ndefu.
Maana hiyo Somangira ni sehemu ya Gezaulole.
 
Mie hiko chuo cha Kigamboni city college nakijua vizuri tu tena ni mbele kidogo ya mwembe mdogo.
Umezunguka njia ,njia ulopita ndefu.
Maana hiyo Somangira ni sehemu ya Gezaulole.
Duh kazi kweli kweli.
Feri-Mjimwema-Kibugumo-Gezaulole-Mwongozo-Dege-Mwembe Mdogo-Cheka---Avic town sawa?
 
Duh kazi kweli kweli.
Feri-Mjimwema-Kibugumo-Gezaulole-Mwongozo-Dege-Mwembe Mdogo-Cheka---Avic town sawa?
Unazijua nyumba za Watumishi house zinazopakana na bahari zilizopo Mwongozo?
Asa kutoka pale na Avic sio mbali.
Mie nimezurura napajua mkuu.
 
Sasa watu wamejenga Bunju B,Ununio,Mbweni Teta ambako ni Km za kutosha tu kutoka Magomeni au Kariakoo.
Mi nipo kwenye Construction naizunguka sana Dar,,
Kuna maeneo bado nyuma sana, kuna maeneo huduma zake ni shida sana.
Maeneo kama Mbondole,Magohe,Majohe,Buyuni
Maeneo ya Makabe,Msakuzi,Mabwe Pande,
Maeneo ya Homboza hata huko Bunuju B huko mitaa ya ndani ni Vumbi tu.
 
Sasa mkuu, kwa hilo tu ,nenda
-Palm village (kwa Warioba)
-Dar villa (Msasani near Mayfair)
-Morocco square (Mikocheni Morocco)
na Masaki kuna apartments kibao hazina wateja.
Mkuu soko la apartments ni Jiji zima halipo vizuri kwa miaka 7 hii.
Hata Majengo makubwa ya maofisi hayana wateja. Hata majengo ya Supermarket.
Sawa.
 
Ukitaka ukae sehemu ambayo inakuwa haraka. Nenda sehemu ambapo watu wa kipato cha kati na maskini wanajenga.

Kigamboni viwanja vingi na maeneo vinamilikiwa na watu matajiri ambao hawana shida ya nyumba za kuishi.

Unakuta mtu ana nyumba mbezi beach ila amenunua kiwanja kigamboni.

Huyo mtu hawezi kujenga leo wala kesho.

Hao ndio wanachelewesha mji kukua.

Tofauti na maeneo kama chanika maana wanaonunua viwanja ni watu wenye shida ya nyumba za kuishi. Hivyo wanajenga fasta mji unajaa

Sehemu nyingi ziliopimwa maendeleo yanachelewa sana ,viwanja vilivyopimwa vingi vinamilikiwa na watu wenye vipato vya kati ambao kama ulivyosema wanamajumba mjini huko.

Lukuvi ndiyo alitaka kumaliza ilo tatizo ,just imagine mbweni mpaka leo bado kuna viwanja bado havijajengwa vipi kuhusu huko? Serikali isimamie ile sheria mtu kama hajajenga fensi au kuendeleza na kuacha pori anyang'anywe ardhi ,hiyo ndiyo itasaidia kuondoa mapori.

Skwata kuna maendeleo sana kwasababu jamaa wanajenga sana ila kulipopimwa tajiri anasikilizia kwanza ,anatafuta mabilioni aje kujenga hekali hivyo inachukua muda sana ,serikali isimamie sheria yake ya kuwanyang'anya kama hawajaendeleza ndani ya miaka mi3.
 
Back
Top Bottom