DOKEZO Ni kweli Hospitali ya Taifa Muhimbili kulala kwa siku ni gharama zake ni tsh 50,000?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hili suala linahitaji ufafanuzi hivyo kama watu wa Muhimbili wapo humu walitolee ufafanuzi kwa sababu hapo ukichanganya na gharama za dawa,consultation na vipimo inaweza kufika 200k kwa siku sasa wangapi tunaweza kumudu.
 
Hata wajawazito huku vijijini wanalipishwa pesa kujifungua wakati serikali inaseama ni bure! Tunapewa control namba kabisa tunalipia kujifungua kwa njia ya kawaida sio upasuaji!
 
Aisee Hawa ndio madaktari wetu....assume hapo unaumwa halafu malipo changamoto then unakutana na dokta kama huyu.
 
Kakate Bima ya Taifa hayo hutayajua na ukiyajua wala hutalalamika!
 
Aisee Hawa ndio madaktari wetu....assume hapo unaumwa halafu malipo changamoto then unakutana na dokta kama huyu.
Nope Tatizo watu hamtaki Kuambiwa Ukweli..
Hivi unajua Uendeshaji wa Hospitali Unachukua gharama Kiasi gani?
Unajua manunuzi ya Dawa yanachukua Gharama kiasi gani?
Malipo ya Vifaa tiba, Umeme, Maji na Bidhaa Vingine hospitali vinagharimu kiasi gani?

Tunapolalamika Tukumbuke Kuwa Hospitali Zinajiendesha Zenyewe na wala Hazina Ruzuku Kutoka Serikalini
 
Kananishangazaga sana tu kale kazee kanakotaka watz wote tule kama yeye sasa watz wote tukiwa kama janabi wageni si watatuogopo wakijua nchi ina raia mazombi kwa jinsi tulivyokondeana
 
Nakuelewa sana mkuu ila umejibu kifedhuli sana,na ndio maana swali langu limejikita kwenye hospital ya taifa ambayo pia ni ya serikali ambayo ndio kimbilio la mwisho kwenye maswala ya afya za watanzania wala sijawataja regency au aghakan na remind kuwa wanaofata huduma pale alisimia kubwa kipato chao ni cha chini ambao mchango huwa unapitwa kwa ndugu na jamaa.

Kiuhalisia hiyo pesa ni nyingi sana shukuru Mungu kama unaiona ndogo,serikali kukubali hili swala la walipa kodi wakamuliwe pesa hiyo sio sawa.
 
Mkuu Ungeelewa Usingeona Kuwa Jibu langu ni la kifedhuli!

Tatizo watu Wengi mnadhani Kuwa hospitali za Serikali.Huwa zinapewa Pesa ya Kujiendesha..
Lakini Ukweli utaujua kama Ukiwa ndani ya Field hii..

Nitarudia tena Serkali haitoi ruzuku wala offer ya pesa Kwa hospitali yoyote..

Watumishi Wa afya ,Madaktari l, Nurses na wafanyakazi wote wanao wahudumia Nyinyi Mnafikiri wanatoa wapi Posho?? Na Motisha?
Madawa ambayo mnatumia, Na vifaa mnavyotumiwa kuhudumiwa vinatoka wapi??
Mnafikiri uendeshwaji wa Hospitali, Ukarabati na Vitu vingine vyote kwa Ujumla Pesa zimatoka wapi?

Wakati mwingine ni vyepesi sana Kulaumu kwakuwa Haujui Hali ilivyo, Sisi tulio ndani ya Hiyo hali.tunajua Maumivu yake..

Na ndo maana Nikakwambia kwa huduma Unayopewa Humo na Hadhi ya Hospitali yenyewe gharama ya 50k Kwa Siku Ni ndogo sana...


kuna Kipimdi nilikuwa na Rafiki angu Mmoja ni Mbunge..
Kuna Muda tulikuwa Tukibishana sana Kuhusu haya mambo (Kama wewe Hivi) tulifikia Mpaka Kutukanana..

Alipopata Ubunge akapelekwa kamati ya Afya Baada ya Kujua Kuhusu Hospitali zinavyoendeshwa baada ya Miaka miwili ndani ya kamati ya afya aliniita na Kuniomba Msamaha..

Kuna Muda Ni vema Kufanya Research ya Kina Kuhusu Kitu kabla hujalaumu na Kubeza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…