Ni lini Rais Samia ataanza ziara kusikiliza kero za Wananchi?

Ni lini Rais Samia ataanza ziara kusikiliza kero za Wananchi?

Aliyekuambia kazi ya Rais ni kusikiliza kero amekuingiza chaka. Kuna wakuu wa wilaya na mikoa hao ndiyo wa kusikiliza kero za wananchi. Wahutu mwacheni Rais wetu afanye kazi tumewachoka sasa rudini kwenu Burundi.
 
Sasa hiv tunajua sio kazi yao Ndio si wapo madarakan , uchaguz ukifika ndo itakua kazi yao sasa kutafuta wananchi had mapangon na kuwachezea viduku wawapigie kura, ***** zao wataioata fresh mbwa hawa
utatukana sana bro. ila nikwambie tu hiyo 2025 utakuwa dissapointed the way ccm itapigiwa kura again kirudi madarakani.

maana ccm inayumba. upinzani hawaeleweki. kura zitaenda ccm tena
 
Ile misafari ya magari wakati wa awamu ya 5,ilitumia gharama na fedha nyingi.Ajabu msafari ulikuwa unatembea na Fedha taslimu,na kugawa fedha njiani(utaratibu ambao wengi tuljiuliza fedha zinapatikanaje,au zinatolewaje benki au hazina na kwanini msafari unatembea na fedha nyingi )
Unaweza kukuta walionufaika na kuwa kwenye msafara wa ziara,ndio wamekuja kuanzisha huu uzi.
 
Ila mama anasafiri sana,tangu aanze urais hajatulia kabisa sijui muda wa kufanya maamuzi sahihi anaupata sangapi,muda wa kufikiria changamoto za wananchi na namna za kuzitatua,hata muda wa Ibada na Mwenyezi Mungu anaupata kweli,kila leo safari,events....na ndo ameanza tu majukumu
Anasafiri kuzurura au kufanya kazi? Acha uzushi wa kipuuzi
 
Akisema warumi ataonekana ana mdomo... hata msiba haujaisha vizur huyo kashaanza kukimbilia nchi za watu Sijui anatafuta nini

Magu alikua ana mapungufu yake ila ulikua unaona kabisa he was dedicated in serving the people of Tanzania, alikua na uchungu na nchi yake, ila huyu mama yupo kimaslahi, yani tutalia na kusaga meno had miaka minne iishe
Utalia wewe..Kama hutaki kufanya kazi kwa bidii..sisi wenzanko tunaimani na mama SSH..na aliyekuambia mama Ni minne tu ni Nani..yupo Sana..kikubwa tumuunge mkono na serikali yake..tumuombee Allah ampe hekima ya kuongoza nchi yetu..na Watanzania tufanye kazi kwa bidii
Kumi Tena kwa mama SSH
 
Kwani kuna kero? Shujaa si alishamaliza kila kero
 
Ila mama anasafiri sana,tangu aanze urais hajatulia kabisa sijui muda wa kufanya maamuzi sahihi anaupata sangapi,muda wa kufikiria changamoto za wananchi na namna za kuzitatua,hata muda wa Ibada na Mwenyezi Mungu anaupata kweli,kila leo safari,events....na ndo ameanza tu majukumu
JK si yupo nchi inakwenda sawa usiwe na wasiwasi
 
Utalia wewe..Kama hutaki kufanya kazi kwa bidii..sisi wenzanko tunaimani na mama SSH..na aliyekuambia mama Ni minne tu ni Nani..yupo Sana..kikubwa tumuunge mkono na serikali yake..tumuombee Allah ampe hekima ya kuongoza nchi yetu..na Watanzania tufanye kazi kwa bidii
Kumi Tena kwa mama SSH

Utamuunga wewe na familia yako, hatutaki raisi mzembe
 
Hana wasaidizi ?

Au unataka yeye afanye kazi ambazo wasaidizi wanaweza kuzifanya na zile za kimataifa zinazomuhitaji zaidi atume wengine ?

Hizo Kero hamna wabunge ? (Wawakilishi wa Wananchi) ?
 
Hana wasaidizi ?

Au unataka yeye afanye kazi ambazo wasaidizi wanaweza kuzifanya na zile za kimataifa zinazomuhitaji zaidi atume wengine ?

Hizo Kero hamna wabunge ? (Wawakilishi wa Wananchi) ?

Sasa kama kuna wawakilishi kwa nini wakati wakuomba kura Ndo wanapeleka makalio yao kwa wananchi ? Si pia wapeleke wawakilishi?
 
Sasa kama kuna wawakilishi kwa nini wakati wakuomba kura Ndo wanapeleka makalio yao kwa wananchi ? Si pia wapeleke wawakilishi?
Kuna kitu kinaitwa effective na efficiency

Bosi wa hoteli kuosha vyombo (inawezekana ikawa ni effective na akaviosha vizuri sana) ila kutumia muda wake ambao angekuwa anaongea na suppliers au kuangalia jinsi ya kuboresha hoteli yake kwa kuosha vyombo ambavyo kuna kitchen porter (muosha vyombo) sio efficient use ya muda wake.

Wawakilishi wapo pale kwa kazi za kufanya mara nyingi kiongozi anayeingilia kazi za wengine sio utendaji pekee bali ni propaganda na kupiga kampeni na kujionyesha anafanya kazi (Unadhani hizo Kero huwa hawazifahamu mpaka wakipita na kujifanya kuyaona hayo mabango)?
 
Kuna kitu kinaitwa effective na efficiency

Bosi wa hoteli kuosha vyombo (inawezekana ikawa ni effective na akaviosha vizuri sana) ila kutumia muda wake ambao angekuwa anaongea na suppliers au kuangalia jinsi ya kuboresha hoteli yake kwa kuosha vyombo ambavyo kuna kitchen porter (muosha vyombo) sio efficient use ya muda wake.

Wawakilishi wapo pale kwa kazi za kufanya mara nyingi kiongozi anayeingilia kazi za wengine sio utendaji pekee bali ni propaganda na kupiga kampeni na kujionyesha anafanya kazi (Unadhani hizo Kero huwa hawazifahamu mpaka wakipita na kujifanya kuyaona hayo mabango)?

Whatever the case , ziara ya raisi kutembelea wananchi wake iwe ni lazima kama alivyokua anafanya magufuli, kumbuka raisi amechaguliwa kuwatumikia wananchi na sio vinginevyo, Sasa kama raisi hana utaratibu wa kutembelea raia wake na kusikiliza kero zao kazi yake ni nini ?

Kama raisi lazima apitie sehemu mbali mbali kuhakikisha kama kweli hao wabunge wanatimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi ipasavyo au lah.

Kwa mfano mimi ni Boss wa hotel , halafu eti naamua tu kukaa nyumbani kisa kwenye hotel kuna wasimamizi wananisimamia kila kitu , unadhan Biashara itaenda? Tusipende kushabikia vitu vya ajabu
 
Whatever the case , ziara ya raisi kutembelea wananchi wake iwe ni lazima kama alivyokua anafanya magufuli, kumbuka raisi amechaguliwa kuwatumikia wananchi na sio vinginevyo, Sasa kama raisi hana utaratibu wa kutembelea raia wake na kusikiliza kero zao kazi yake ni nini ?
Kwahio unadhani Rais bila kutembelea na kusikiliza watu live Kero hazimfikii ?, Magufuli alitembelea mikoa mingapi na watu wangapi ? Unadhani ni possible kutembelea wananchi kila sehemu ?
Kama raisi lazima apitie sehemu mbali mbali kuhakikisha kama kweli hao wabunge wanatimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi ipasavyo au lah.
Rais anaweza kumwajibisha mbunge ?,
Mambo yote ni system na kila mtu ana system yake kwa taarifa yako efficient system sio Rais kupita kila sehemu ili tu aonekane anafanya kazi wakati ule ule anaweza kujua kinachoendelea sio mpaka uwepo pale live (its impossible kuwepo pote wakati wote)
Kwa mfano mimi ni Boss wa hotel , halafu eti naamua tu kukaa nyumbani kisa kwenye hotel kuna wasimamizi wananisimamia kila kitu , unadhan Biashara itaenda? Tusipende kushabikia vitu vya ajabu
Ukikaa nyumbani utakuwa mjinga unacheki daily reports unaangalia mapato yaliyopo na yaliyopita pia unafanya kazi ambazo hao wasaidizi ni vigumu kuyafanya, sidhani kama ku-expand hoteli yako watakufanyia ila kila wakati itabidi kufanya nao mikutano ili kuendeleza vizuri hoteli yako (na sio kufanya kazi ambazo wao wapo capable kuzifanya)
 
Ndugu , Key performance Indicator ni Rais kuzunguka nchi nzima na kusikiliza kero za wananchi?
Naomba uwe muelewa , usilete cheap politics katika awamu hii ya sita.
Wateule wapo kwa ajili ya nini?
Wananchi wanaishi kwa kero tu?
Hawana shida na maendeleo?

Zungumzia tunawezaje kuipaisha nchi kiuchumi, acha blaah blaah hapa.
Keshazoea aina ya uongozi wa hayati sasa anataka wa awamu ya sita nae apite mule mule.
 
Sasa kazi ya wakuu wa mikoa, wilaya,watendaji wa kata,wabunge,TISS n.k itakuwa ni nini.

Kweli kichaa alifanikisha kuwabrainwash wapumbavu wengi.
Hata mie sioni haja ya raisi kupita mitaani na kuanza showing off kwenye TV kama raisi anatatua kero. Napendelea zaidi mifumo, sheria kubadilika na kuadress kero kwa kupitia mifumo yaani systematic approach.
 
Mie naomba asifanye ziara, zile za mwendazake hazijakutosha? Huyu afanye mengine, matatizo anayajua, kwenye kampeni alizunguka, pia naona hata kuapisha wateule angeacha tu, ye awataje tu halafu wakatimize majukumu, kwa hata wakiapa wengine sugu awajali viapo, mkapa alimteua gama kuwa RC na hakumwapisha!
 
Kwahio unadhani Rais bila kutembelea na kusikiliza watu live Kero hazimfikii ?, Magufuli alitembelea mikoa mingapi na watu wangapi ? Unadhani ni possible kutembelea wananchi kila sehemu ?

Rais anaweza kumwajibisha mbunge ?,
Mambo yote ni system na kila mtu ana system yake kwa taarifa yako efficient system sio Rais kupita kila sehemu ili tu aonekane anafanya kazi wakati ule ule anaweza kujua kinachoendelea sio mpaka uwepo pale live (its impossible kuwepo pote wakati wote)

Ukikaa nyumbani utakuwa mjinga unacheki daily reports unaangalia mapato yaliyopo na yaliyopita pia unafanya kazi ambazo hao wasaidizi ni vigumu kuyafanya, sidhani kama ku-expand hoteli yako watakufanyia ila kila wakati itabidi kufanya nao mikutano ili kuendeleza vizuri hoteli yako (na sio kufanya kazi ambazo wao wapo capable kuzifanya)

Wakati pekee unaowezekana kutembelea mikoa yote tunajua nj wakati wa kuomba kura tu , hadi vijiji vya wachawi wataenda kuomba kura, ila wakishatimiza malengo yao , ndo visingizio sasa vitakuja mara ooh kuna wawakilishi, mara ooh haiwezekan kutembelea mikoa yote, ila wakati wa kuomba kura, kila kitu kinawezekana.
 
Wakati pekee unaowezekana kutembelea mikoa yote tunajua nj wakati wa kuomba kura tu , hadi vijiji vya wachawi wataenda kuomba kura, ila wakishatimiza malengo yao , ndo visingizio sasa vitakuja mara ooh kuna wawakilishi, mara ooh haiwezekan kutembelea mikoa yote, ila wakati wa kuomba kura, kila kitu kinawezekana.
Kwangu mimi binafsi (In my Humble Opinion) ingawa simpangii mtu nitashukuru na nitaona ni matumizi mazuri ya Kodi zetu kama Kiongozi Mkuu atatumia huo muda kutatua na kuunganisha wote na kuwaongoza kutatua Kero kuliko kutumia muda mwingi kujifanya anasikiliza (wakati popote pale anaweza kuzisikia na anazisikia) kwa kujifanya ndio mtendaji mkuu wakati akiondoka hapo hakuna kinachofanyika...

Yaani kufanya afanye kazi hata behind the scenes sio kuonekana anafanya kazi (kupiga siasa) wakati hakuna kinachofanyika zaidi ya propaganda.... (Atumie muda mwingi na hao wasaidizi wake kwa kuwafuatilia na kuwahoji na kwa kufanya mikutano lukuki ya tumepanga nini / tumefanya nini / tumekosea wapi / turekebishe wapi / tuanze kutenda tena...., (Continuous Improvement)
 
Japokua hayati alikua anaendesha nchi kibabe, lakini kuna baadi yamambo aliyafanya yalitupendezea hata sisi wananchi wanyonge tunaoshi chini ya dola moja kwa siku.

Ziara za sehemu mbalimbali kusikiliza kero za wananchi zilitufariji sana.

Kwa heshima na taadhima tunakuomba mama yetu, Amiri jeshi mkuu, President material mweshimiwa Rais samia suluhu uanze ziara za kusikiliza kero za wananchi wako wanyonge na kuzitafutia ufumbuzi.

Tunakupenda sana

Asante sana

Mitano tena✋


Hakuna haja, akitembea barabarani atakutana na wale walioandaliwa anatawapa papo kwa papo, inatosha. Hii ni nchi tajiri.
 
Back
Top Bottom