Leo nimekutana na mdau flani toka wizara flani ya serikali ya Tanzania, tulikuwa tukipata chakula cha mchana sehemu flani hapa dar, sitaitaja jina kwa Sababu flani.akaniambia mdogo wangu shambulizi la Lissu serikali haihusiki hata kidogo, wanaionea bure kabisa, siasa inatupeleka vibaya. Kaniambia unajua shambulizi hili limetokana na kudhulumiana pesa, jamaa zangu walikua wananyofoa nyaraka wizarani wanampa kwa makubaliano ya ujira, tatizo la Lissu Kila alipopewa pesa na wazungu aliwaeleza wale jamaa kwamba bado malipo yanashughulikiwa Kumbe alikua analipwa kwa instalment , wakimsumbua Sana anakata kiwango kidogo Sana, akidai yeye ndo master plan wasiwe na Shaka , sasa jamaa wakaona huyu tunamtajirisha yeye huku Sisi Kazi zetu zipo hatarini, ndo maana wakaona dawa ni ku revenge, jamaa Kaniambia wazungu walimtegemea Sana Lissu , na yeye aliwaambia wasiwe na Shaka kwa kua ametengeneza mtandao mpana kuhakikisha serikali haifurukuti kwa Mikataba iliofungwa hapo nyuma.
Tuwe na subra, mengi tutayasikia, yatabadilisha mitizamo yetu kabisa