Ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu?
Tokea mnadhimu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni T Lisu apigwe risasi mchana kweupe kuna nadharia kadhaa zimeibuka kujaribu kuelezea huo upigwaji risasi wa Lisu.

Lisu mwenyewe alipotembelewa na makamu wa rais akiwa Nairobi alikiri wazi kuwa hawajui waliompiga risasi na kuviachia vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake.
Ingawa hivi majuzi akiwa ubeligiji ameibuka na kuihusisha serikali na upigwaji wake risasi.

Nadharia nyingine inatokea ndani ya chama cha chadema ,gazeti la Jamvi la habari wameelezea A to Z kuwa Lisu alipigwa risasi baada ya kutishia uenyekiti wa Mbowe. Wameeleza siku chache kabla ya kupigwa risasi kulikuwa na vikao kadhaa vya wanachadema wakimtaka Lisu agombee uenyekiti.

Pia aliyekuwa mbunge wa Ukonga na mjumbe wa kamati kuu ya chadema naye alinogesha nadharia hii baada ya kuelezea namna watu wanavyopata misukosuko wakitangaza kugombea uenyekiti ndani ya chadema.

Waitara alihusisha kufa kwa Chacha Wangwe ,kutaka kulishwa sumu kwa Zito Kabwe ,kupigwa risasi kwa Lisu na yeye mwenyewe kutishiwa kushughulikiwa iwapo atagusa kiti cha mwenyekiti ndani ya chama..

Kama kweli Mbowe anasingiziwa kwenye tuhuma hizi za kuuwa watu wanaotaka kugombea uenyekiti ndani ya chama basi aende mahakamani kutaka kusafishwa na tuhuma hizi.
Mbowe akiendelea kukaa kimya bila kuwaburuta mahakamani wanaomtuhumu basi , mamilioni ya watanzania watajua ni kweli View attachment 829281View attachment 829284
Lissu mwenyewe amemtaja aliyepanga, mbona mnahaha sana?
Mwambieni huyo aliyetajwa na lissu ndiye yeye aende kama amesingiziwa...
 
Lisu mwenyewe alipotembelewa na makamu wa rais akiwa Nairobi alikiri wazi kuwa hawajui waliompiga risasi na kuviachia vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake.

Aliposema hawajui alikuwa anamaana hawajui individuals kwa sura. Hiyo haimaanishi kuwa hawajui waliomshoot ....... ndiyo maana kaamua kusingle out anayefikiri aliwatuma!!

Anyway, kuamini gazeti la Tanzanite kuwa wanaweza kuja na credible info kuliko vyombo vyetu vya usalama amabo wameamua na kulifunga file ni kuidhalilisha Tanzania kama nchi!!
 
Tume Huru mmezikataza ''Independent Inquires Are Not Allowed'' Mbwa Hawezi ................Mkia wake hata awe Mkali Vipi
 
Kwa nini aende Mbowe na siyo hao waliotwambia wanawatafuta wasiojulikana? Sasa si amejulikana? Wamkamate sasa. Unasemaje hajulikani na bado unasema aliyefanya haya ni Mbowe? Kwani Mbowe hajulikani? Hivi mbona kwa Mbowe mnapata Tabu sana namna hii? Aliwafanya au anawafanya nini hadi kupata sana tabu naye namna hii?
 
Vyombo vya dola vimefunga upelelezi? Kama bado,hicho kipeperushi hakiwezi kuwa moja ya chanzo cha upelelezi wao?
Waitara amejitokeza, kwanini asiitwe kuhojiwa ili aeleze analolijua?
Kumtaka Mbowe kwenda mahakamani ni upuuzi, tuache kuruhusu siasa zitawale maisha yetu.
 
Kwa nini aende Mbowe na siyo hao waliotwambia wanawatafuta wasiojulikana? Sasa si amejulikana? Wamkamate sasa. Unasemaje hajulikani na bado unasema aliyefanya haya ni Mbowe? Kwani Mbowe hajulikani? Hivi mbona kwa Mbowe mnapata Tabu sana namna hii? Aliwafanya au anawafanya nini hadi kupata sana tabu naye namna hii?
Kwa hiyo waitara amesingizia?
 

Maskini CCM,hawa ndio watu waliobaki kuipigania mitandaoni. Inasikitisha sana!

Vijana waliotulia kiakili wamenyamaza kimya,wale bongolala ndio wamejaa mitandaoni kukitetea chama na kueneza propaganda. Inasikitisha!

Kama Mbowe anahusika kwanini hakamatwi na kupandishwa kizimbani,au hujui hata kuwa kazi ya kushtaki jinai ni ya jamhuri/serikali?

Mbona nyie watu mnatia aibu kwa kasi ya ajabu?
 
Mmejitahidi kupotosha kifo cha Chacha Wangwe kwakuwa kafa. Lakini Mungu mkubwa Lissu yupo hai na anamtaja muhusika kabisa. Ingetokea Lissu afe mngepotosha umma. Huyo anayetajwa na Lissu ndio muhusika. Halafu kuna nyuzi zaidi ya tano zenye maudhui sawa na huyu mleta uzi. Hicho ninkiashiria kwamba ni mkakati maalum wa kumsafisha mtajwa. Na huu utetezi wenu wa kupotosha ndio unamuanika muuaji vizuri.
 
Tokea mnadhimu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni T Lisu apigwe risasi mchana kweupe kuna nadharia kadhaa zimeibuka kujaribu kuelezea huo upigwaji risasi wa Lisu.

Lisu mwenyewe alipotembelewa na makamu wa rais akiwa Nairobi alikiri wazi kuwa hawajui waliompiga risasi na kuviachia vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake.
Ingawa hivi majuzi akiwa ubeligiji ameibuka na kuihusisha serikali na upigwaji wake risasi.

Nadharia nyingine inatokea ndani ya chama cha chadema ,gazeti la Jamvi la habari wameelezea A to Z kuwa Lisu alipigwa risasi baada ya kutishia uenyekiti wa Mbowe. Wameeleza siku chache kabla ya kupigwa risasi kulikuwa na vikao kadhaa vya wanachadema wakimtaka Lisu agombee uenyekiti.

Pia aliyekuwa mbunge wa Ukonga na mjumbe wa kamati kuu ya chadema naye alinogesha nadharia hii baada ya kuelezea namna watu wanavyopata misukosuko wakitangaza kugombea uenyekiti ndani ya chadema.

Waitara alihusisha kufa kwa Chacha Wangwe ,kutaka kulishwa sumu kwa Zito Kabwe ,kupigwa risasi kwa Lisu na yeye mwenyewe kutishiwa kushughulikiwa iwapo atagusa kiti cha mwenyekiti ndani ya chama..

Kama kweli Mbowe anasingiziwa kwenye tuhuma hizi za kuuwa watu wanaotaka kugombea uenyekiti ndani ya chama basi aende mahakamani kutaka kusafishwa na tuhuma hizi.
Mbowe akiendelea kukaa kimya bila kuwaburuta mahakamani wanaomtuhumu basi , mamilioni ya watanzania watajua ni kweli View attachment 829281View attachment 829284
Ha ha haaa! Watetezi wa bichwa mmeshaanza kuweweseka. Mhutu analo hili; na bado mpaka nywele zote zinyonyoke. Dadadeki.
 
Yaani MBOWE ana mambo ya "ajabu" kweli kweli, apange kumuua LISSU, halafu aondoe ulinzi wote wa kiserekali kwenye eneo husika na kama haitoshi akazipotezesha kamera za CCT (kwa waziri nani sijui) kutoka eneo husika. Halafu akaenda na LISSU Nairobi na huko akashindwa kum-maliza mlengwa wake. Kana kwamba haitoshi akalipiga ganzi jeshi la polisi lisijue la kufanya hata kupata taarifa za kilichotokea toka kwa LISSU na DEREVA wake. HII SINGLE YA CCM IMECHUJA WATAFUTE NYINGINE.
 
Back
Top Bottom