Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
LE TENANT DU TITRE wa JB Mpiana na Bendi yake nzima Kipenzi changu ya Wenge BCBG ambapo Mghani / Rapa kwa Kiswahili au Atalaku kwa Kilingala au Animateur kwa Kifaransa ninayempenda kuzidi maelezo na niliyechukua jina lake na kulitumia rasmi humu JamiiForums aitwae GENTAMYCINE ( majina yake halisi Pitshou Lisimo ) alifanya Kazi ya ajabu humu huku akisaidiana kwa karibu sana na Baba wa Marapa / Waghani wote Congo DR Tutu Caludgi ( majina yake halisi Yombo Lumbu ) na pembeni yao wakimtambulisha Rapa / Mghani Kijana kabisa ila bahati mbaya sasa hivi ameshatangulia mbele za haki CELLULAIRE Mokili Mobimba ( majina yake halisi Faustine Nzinga Yankobo ) Kwa mpenzi yoyote wa Nyimbo za Kikongo akiusikiliza huu Wimbo hasa sehemu ile ya Sebene lake nina uhakika hata akiwa anambaiolojia Mkewe au anabaiolojiwa na Mumewe ataacha Kwanza ili aserebuke nao kwani ni moja ya Wimbo mtamu na umejaa kila kitu huku Vyombo vyote vikitulia kabisa. Nautafuta sana mwenye nao aniwekee hapa tafadhali na nitamshukuru mno / sana tu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] siujui ila ikiwa kweli unaweza kumfanya mtu akaacha kufanya biology, then na mimi nautafuta. Itasaidia kunifanya nipinguze vipindi vya biology [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Betty.......imeimbwa na Zahir Zorro na bendi yake baba yake Banana Zorro kwa anayefahamu jina kabisa la nyimbo anisaidie
 
Mwenzenu nimekumbwa na kimbunga
Si kimbunga cha upepo Bali kimbunga
Cha mapenzi mama
Toka siku ile ya kwanza nilipomuona
Msichana mrembo jully nilishindwa kujizuia nikamweleza wangu ukweli yakua
Nimpenda nae akanijibu jully asante kwakunipenda.dah wakuu hii ngoma hatari aliimba Bob ludara jina silijui nisaidieni niupate
 
Back
Top Bottom