Nifahamishe kituo cha watoto yatima chenye uhitaji mkubwa sana

Nifahamishe kituo cha watoto yatima chenye uhitaji mkubwa sana

Uhitaji unatofautiana jamani, mjitahidi sana kufanya charities mjionee, kuna vituo mfano dogo dogo center wale wako mbali sana, ufadhili wao ni mkubwa, watoto wanaishi kishua.... kuna kituo kipo Kisarawe ukifika tu chozi litakutoka mazingira ya pale hadi watoto wanakuomba uwachukue, nawapenda walivyo na upendo na ukarimu tho [emoji847][emoji3059]..... so yupo sahihi kuulizia hivyo
Naomba jina la hicho kituo cha kisarawe
 
Na sijasema mpaka ujitosholeze. Kwa taarifa yako kujitosheleza ni neno relative na kuna watu wanaweza wasijitosheleze kamwe. Nimesema wale ambao hawakumbuki kabisa walio karibu na kuzingatia walio mbali. Watu wa aina hii wako. Unakuta mtu wazazi wake au ndugu zake wako hohehahe lakini hana habari nao na badala yake anaonekana kwenye social media akisaidia watu wa mbali.
Sasa huo utakuwa ni "ukafiri", ingawa ni kweli watu wa aina hiyo wapo pia.
 
Uhitaji unatofautiana jamani, mjitahidi sana kufanya charities mjionee, kuna vituo mfano dogo dogo center wale wako mbali sana, ufadhili wao ni mkubwa, watoto wanaishi kishua.... kuna kituo kipo Kisarawe ukifika tu chozi litakutoka mazingira ya pale hadi watoto wanakuomba uwachukue, nawapenda walivyo na upendo na ukarimu tho [emoji847][emoji3059]..... so yupo sahihi kuulizia hivyo
Kuna wengine wana njaa nafsini mwao ambayo haitoshelezwi na kitu chochote isipokuwa "upendo".

Kuna ambao hawahitaji hata pipi, ila wampate tu mtu atakayewaita "mwanangu", au "mdogo wangu" au "rafiki yangu", n.k. kwa upendo.

Kuna watoto ambao ukiwaonesha upendo, hata kama hutawapa kitu, utakuwa umewasaidia pakubwa sana.
 
Huyu jamaa kuna fursa anataka kuitumia kupitia kituo hicho ,kama una uwezo wa kuwasaidia bila kuwa na manufaa yako binafsi sidhani kama unashindwa kujua pakusaidia bila kuomba huku,wewe huna tofauti na wale "tuma kwa namba hii"
Mkuu unanikosea sana. Ni kwa nini uniwazie hivi? Hapa JF ni wangapi nimekutana nao na kufanya nao kazi? Kama upo Dar katibu DM ili siku hiyo twende woote sehemu husika.

Sijui ni kwa nini watu tunapenda kuwawazia wengine vibaya.
 
Uhitaji unatofautiana jamani, mjitahidi sana kufanya charities mjionee, kuna vituo mfano dogo dogo center wale wako mbali sana, ufadhili wao ni mkubwa, watoto wanaishi kishua.... kuna kituo kipo Kisarawe ukifika tu chozi litakutoka mazingira ya pale hadi watoto wanakuomba uwachukue, nawapenda walivyo na upendo na ukarimu tho [emoji847][emoji3059]..... so yupo sahihi kuulizia hivyo
Mawasiliano na location ya kilipo tafadhali. Naweza nisifike mimi lakini mwingine akahitaji kufika
 
Unahisi anataka aombe michango ya kununulia vitu vya kuepaelekea watoto wahitaji?

Mimi sidhani kama hiyo ndiyo nia yake. Shauku yake ni kupata mahali sahihi pa kuupeleka msaada uliopatikana. Si unajua JF ni mahali unakoweza kupata taarifa sahihi? Naamini ndicho kilichomvutia mdau kuuleta Uzi wake humu. Anajua atapata taarifa zisizoghushiwa.
Hakika mkuu, umenena sahihi sana. Watu wamekua wakizungumza kuwa kuna vituo ni makanjanja na ndio hasa sababu ya kuja humu ili nipate taarifa sahihi kwani huku wajuzi wa mambo ni wengi
 
Wazo Zuri Sana mkuu..
Kwani 99% ya vituo vya kulea watoto yatima ni wapigaji..


99% wamefungua vituo kwa ajili ya maslahi yao binafsi...
Wazo Zuri Sana mkuu..
Kwani 99% ya vituo vya kulea watoto yatima ni wapigaji..


99% wamefungua vituo kwa ajili ya maslahi yao binafsi...
99% ni wapigaji? Mkuu una uhakika na usemalo? Unataka uniambie Serikali imelala kiasi hicho?

Kama huo ndiyo mtazamo uliopo kwa Watanzania wengi, basi sitashangaa tena kufahamu kuwa vituo vingi vinawategemea wafadhili wa nje(Wazungu) kwa kila kitu, mpaka chakula cha watoto.

Ni kweli kuna vituo vya "kinchongo", lakini siamini kama ni vingi kwa kiwango hicho.

Ni kweli kuna hayo katika baadhi ya vituo, lakini mimi naona bado ni afadhali kuliko maisha ya mtaani!

Kituoni, mtoto ana uhakika wa kulala ndani ya jengo hata kama ni sakafuni kuliko kulala barazani mjini!

Kituoni, kuna uhakika wa kula kila siku hata kama si mlo mzuri sana kuliko mitaani ambako wasipifanikiwa kupata kwa kuombaomba, huishia kula vya kuokota majalalani!

Mtoto akiwa kituoni, ni rahisi zaidi kuepushwa kujiingiza kwenye tabia hatarishi kama uvutaji fundi na utumiaji wa madawa ya kulevya!

Kituoni kuna uwezekano mkubwa wa mtoto kusoma kuliko akiwa mtaani!

Ukiona mtoto wa mtaani kakubali kukaa kituoni, ujue na yeye kagundua utofauti. Kunaweza kujazwa hakiwahudumii vizuri sana lakini kina uafafhali kuliko kuhangaika maishani. Mkuu, hao watoto nao wana akili ujue! Wakiona kituo "kinazongua", hawakai.

Nisemalo ni hili, HATA KAMA KUNA VITUO VYA KIMCHONGO, BADO NI AFADHALI KULIKO VISINGEKUWEPO.

Ubinafsi wa waliovianzisha hivyo vituo vina msaada zaidi kuliko upendo wa wengi ambao hawajauweka katika vitendo! Vituo vya watoto vinastahili kusaidiwa.
 
Kwani unajuaje hali ya mtu na familia yake mpaka umshauri aisaidie kwanza familia yake.

Kuna wengine wameumbwa matajiri wao, Vizazi vyao na kila kitu kiwahusucho.
Na wewe umejuaje hayo wakati hajatueleza hali ya familia na nduguze?Hayo ni mawazo yako kama vile alivyotoa mawazo yake.Mawazo ya kila mmoja yaheshimiwe.
 
Hongera sana mkuu, nilikua na huu Utaratibu kituo fulani huko moshi , nilikua nanua nguo za watoto kila baada ya miezi 6 nawaletea kuja kusikia mama mzimamizi wa hao watoto kafungua soko la nguo za watoto huko meimoria nilichoka.
Mkuu, mama msimamizi ndiye mmiliki wa kituo au ni mfanyakazi?

Kama ulibaini kuwepo kwa dalili ya ukiukwaji wa haki kwa nini usingetoa taarifa kwa mamlaka za Serikali hata kama ni kwa siri?

Mkuu, uhitaji wa watoto wanaoishi kwenye makao ya watoto hawahitaji vitu vyako tu, wanakihitaji pia kinywa chako! Jizoeshe kuwa msemaji kwa ajili ya "wasiokuwa" na sauti. Ni vyema ukaanza kulifanya hilo sasa.
 
Hongera sana mkuu, nilikua na huu Utaratibu kituo fulani huko moshi , nilikua nanua nguo za watoto kila baada ya miezi 6 nawaletea kuja kusikia mama mzimamizi wa hao watoto kafungua soko la nguo za watoto huko meimoria nilichoka.
Choka tena
 
Kwahiyo wakristo hapo hawahitajiki, hakifai hicho.

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
Sidhani kama wana ubaguzi huo. Wanaweza wakawa hawahitaji taratibu za Kikristo kituoni kwao, lakini hawawezi kuvikataa vitu vinavyotolewa na Wakristo kwa ajili ya watoto.

Vipo pia vituo vinavyosimamiwa na Makanisa lakini vinapokea msaada kwa watu wote wenye mapenzi mema bila kujali itikadi zao za kidini.
 
mfano dogo dogo center wale wako mbali sana
Hawa mradi wao ni wa kitambo na wasimamizi wao wamesimama haswa kuangalia michongo kutoka kwa wafadhiri wa nje, kuna kipindi walikua wanafanya vipindi vya watoto wakaacha mpaka wakawa wanafunga nyimbo za watoto kwa hio sio was kuwafananisha na vituo vingine vinavyochipukia in short vituo ni mradi sio matoleo au kujitolea na mradi wowote unakua na proposal plus business plan
 
Habari ya wakati huu wakuu. Ninaomba msaada wa taarifa ya kituo chochote cha kulelea watoto yatima ama watoto walio katika mazingira magumu ambacho kiuhalisia kina hali ngumu ya kimahitaji ya kawaida.

Kituo kiwepo Dar es salaam na nitaomba kama utaweza unisaidie mahali hasa kinapopatikana na mawasiliano ya namna ya kufika.

Asante.
Mkuu peleka Msaada wako Kituo Cha Seiiali Kurasini ,huki Intergrity ni 100% v.Vituo vingine ni vile wmaolea Watoto Wachanga....0_6month ..wale watu wanahitaji materials na moral support Si Mchezo!Hivi ni kama vile Msimbazi na Mburahati.
 
Kuna kimoja kipo Madale mama wa kihaya alitoa wakfu nyumba yake kwamba akifa iwe center ya yatima.
Na kweli kituo kinapata sana watu wa kusaidia. Changamoto inakuja kuna sista wa katoliki pale ana roho mbaya sana anawatesa watoto na kuwanyima chakula. Wale watoto wana maisha magumu sana.
Kwani hicho kituo kina ukuta mrefu kama wa Magereza?

Labda kama ni watoto wadogo sana, lakini kama wameshajitambua, hawawezi kukaa kwenye kituo chenye mateso. Huwa wanatoroka.

Hata hivyo, mateso si jambo jema. Ni vyema kuwaripoti kwenye mamlaka husika watumishi wenye kasumba ya aina hiyo.
 
Back
Top Bottom