Hapa kuna vitu viwili: Msamaha na Ndoa.
Msamaha hauna maana kwamba nakubali, bali kutoa nafasi ya kujifunza na kuendelea. Na hii si kwa anae samehe au anae samehewa, ila wote.
Kwa maneno mengine, anae kataa kusamehe na anae kataa msamaha, wote wanafanya kosa na hivyo wanaharibu hali yao ya ndani. Kwa hiyo wana haribu uhusiano; uhusiano kwanza na Mungu na pili na jamii.
Kuhusu ndoa. Kwa uelewa wangu, ndoa ni jambo la akili, ambapo ikishafungwa haiwezi kufunguliwa kwa sababu yoyote; labda kama hakukuwapo na ndoa.
Kwa hiyo, kama hawa ndugu walikuwa kweli wana ndoa, itabaki hivyo daima kwenye akili na hilo haliwezi kubatirishwa.
Kitu ambacho tunatakiwa kujua ni kuwa, mambo yote mema au maovu, mazuri au mabaya yanayoweza kutupata kwenye ndoa, tunapaswa kuyapokea na kuyavumilia kwa unyenyekevu.