Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Ukipata mtu ukamuuzia hiyo smartphone unayoitumia...utaweza kulipia watoto chumba chao...japo kwa miezi miwili huku ukiendelea kujipanga...itakuwa imekusogeza mahala....
Watu wengine mna kejeli zisizo na maana kabisa. Atauza simu mara ngapi? Huyu msaada mzuri ni kuwa na chanzo cha kipato amabcho atakigemea. Wewe hujui smartphone siku hizi ni kifaa muhimu sana kwenye maisha?
 
Kuwasaidia watoto ni mpaka akutane na mimi faragha? Mwenye nia ya kuwasaidia watoto angewasaidia tu, ndio maana nikikataa analeta maneno kama nilyosema kuwa nina jeuri, kiburi, nitakuwa na mwanaume ambaye ananipa kiburi, na kusema hatawasaidia kwa kuwa nakataa.

Nadhani hamjaelewa, lengo la msaada wake ni mpaka akumbushie na mimi maana yake apashe kiporo, nimeandika bila kufunguka nikajua mnaweza kuelewa.

Mimi na yeye tulishamaliza safari, siwezi kuruhusu hicho kitu kitokee abadani asilani eti ili watoto wapate matunzo.
Pole sana. Usikubali ukutane naye kwa faragha. Mlifunga ndoa? Nadhani ni vizuri kama mtamaliza mambo kisheria kwa kwa vikao.
 
SIKUZOTE USIMUAMINI MWANAMKE hasa anapojieleza kuhusiana na misukosuko ya ndoa yake au mahusiano au na mume/mpenz wake... Ni waongo wanafki watafuta huruma tu...
Kwa kweli uyo jamaa sio bwege kiasi icho aondoke kwa staili iyo kuna kitu uyu mama aja sema ila kwa upande wake ame tueleza yanayo tia huruma tu basi .kufikia hapo hii mada bila kupata story ya upande wa pili tuishie kusema pole tu
 
Hapa kuna vitu viwili: Msamaha na Ndoa.

Msamaha hauna maana kwamba nakubali, bali kutoa nafasi ya kujifunza na kuendelea. Na hii si kwa anae samehe au anae samehewa, ila wote.

Kwa maneno mengine, anae kataa kusamehe na anae kataa msamaha, wote wanafanya kosa na hivyo wanaharibu hali yao ya ndani. Kwa hiyo wana haribu uhusiano; uhusiano kwanza na Mungu na pili na jamii.

Kuhusu ndoa. Kwa uelewa wangu, ndoa ni jambo la akili, ambapo ikishafungwa haiwezi kufunguliwa kwa sababu yoyote; labda kama hakukuwapo na ndoa.

Kwa hiyo, kama hawa ndugu walikuwa kweli wana ndoa, itabaki hivyo daima kwenye akili na hilo haliwezi kubatirishwa.

Kitu ambacho tunatakiwa kujua ni kuwa, mambo yote mema au maovu, mazuri au mabaya yanayoweza kutupata kwenye ndoa, tunapaswa kuyapokea na kuyavumilia kwa unyenyekevu.
Unajua watu wengi huwa mnaongelea kitu kinachoitwa msamaha ila hamkijui maana yake. Kulingana na story ya huyu dada tayari amekwisha samehe na ndio maana ameendelea na maisha bila huyo jamaa yake.

Sasa wengi hudhani msamaha ni kudeal na huyu mtu ambaye ameleta kadhia yote hii.

Sio lazima kuendelea kudeal na mtu ambaye amekuletea shida eti muishi vizuri kama mwanzo ndio uite msamaha HAPANA.

Kusamehe haina uhusiano na kuishi tena mkicheka. Ukinikosea naweza kuamua kutocheka na wewe tena na tukionana nakukunjia ndita kabisa. Huo ni ukurasa mpya ambao nimechagua kuishi na wewe kutokana na namna ulivyonifanyia na nimeamua kukuona ni adui na sio rafiki na tutaishi kwa sura hiyo kwa maisha yaliyobakia.

Usihisi nikicheka na wewe basi ndio nimekusamehe, la hasha. Naweza nikakununia na nikaacha kuongea na wewe, nikakublock kabisa ili usiwe sehemu ya maisha yangu.
 
Baba Yao kasema yupo tayari kulea watoto wake na kuwahudumia so Cha muhimu watu mlio Katika ndoa wake kwa waume tulize de libolo kwa mke mmoja mlee watoto wenu na sio kila siku mnawaza uzinzi tu mwisho mnawatesa watoto kisa ndoa zenu fake
Kabisa. Kabisa. Unajua vijana wa siku hizi shida sijui ipo wapi.

Unamkuta binti wa watu njiani, unamsimisha mwenyewe unamtupia mistari it means umemchagua.

Then anakukubalia baada sasa ya kujenga kitu kizuri kati yenu unaanza kumsumbua na vituko vya hapa na pale mara ugombane nae, mara umpe ujauzito halafu uanze kusumbua malezi.

Mara uanze kukimbizana aiseee. Hii kitu inasikitisha sana ujue.
 
Kuwasaidia watoto ni mpaka akutane na mimi faragha? Mwenye nia ya kuwasaidia watoto angewasaidia tu, ndio maana nikikataa analeta maneno kama nilyosema kuwa nina jeuri, kiburi, nitakuwa na mwanaume ambaye ananipa kiburi, na kusema hatawasaidia kwa kuwa nakataa.

Nadhani hamjaelewa, lengo la msaada wake ni mpaka akumbushie na mimi maana yake apashe kiporo, nimeandika bila kufunguka nikajua mnaweza kuelewa.

Mimi na yeye tulishamaliza safari, siwezi kuruhusu hicho kitu kitokee abadani asilani eti ili watoto wapate matunzo.
Jamaa anakudharau sana aiseee. Usije ukaruhusu hata akuguse. Akikugusa m'babue bonge la m'bao wa shingoni pale chini ya kidevu usawa wa kolomelo na kifua vinapokutana katika collar bone.
 
Mimi sina tatizo na yeye, nilisha yaacha yapite ndio maana sijihangaishi hata kutaka chochote kutoka kwake wala kujua anakoishi. Na kuhusu watoto wake wala sijawaambia ubaya wowote na wala hawaulizi chochote. Ila mimi kumsikiliza kwa namna ya kuyajenga haitakaa itokee chini ya jua hili hata kwa bahati mbaya.
Labda kwa asiewajua nyie,ushindwe kuwalisha sumu watoto kama hupo tayari kumsikiliza mzazi mwenzio anataka muongee kuhusu nini?
Akija nae kutoa ushuhuda wake apa tutabaki midomo wazi.[emoji19][emoji19]
 
Pole sana dada!

Ninaomba kukushauri. Kama mume wako amekutafuta na ametaka mzungumze, msikilize.

Kwa uelewa wangu, kukataa kumsikiliza unafanya kosa, kosa zaidi. Kwa kusema hauwezi kuonana nae unaharibu akili yako; unajiadhibu mwenyewe.

Kwa hiyo, kwa msimamo huu, kama ndio dhamira yako, unashiriki kwenye makosa yaleyale; nawe unakuwa mkosaji hata kama haukuwa na kosa.

Msamaha sio kusema nimekusamehe au nimesahau nilitendewa au kutenda, bali hali hiyo ni lazima uifanye iwe vitendo au matendo.

Dada, msamaha ni mlango wa mema yote, ni nguvu ya kupata chochote; ni pia uponyaji.

Anae samehe anamkaribisha Mungu ndani yake.
Anaonekana ana kiburi sio cha nchi hii japo hatufahamiani but i can smell it[emoji3]
 
Baba yao kama walivyo wababa wengine wapuuzi, alikua anatafuta njia ya kujirudi Kwa mwanamke aendelee kupasha viporo.


Lkn pia inawezekana mpaka akataka kujirudi nisababu alipokuja mambo yalibadilika.


Ni chaguzi sahihi sana ALOFANYA mtoa Mada hata kama ana shida ya Uchumi.



Kuhusu wababa kutulia kwenye Ndoa zao, hapa suala ni Akili ya Mwanaume mwenyewe , Kuna hao wanachepuka na kusahau familia, alafu Kuna Mimi, nachepuka lkn Huniambii kitu Kwa Wife na wanangu na wanangu wengine.
Katika hiyo paragraph ya mwisho sasa hapo ndipo umemwaga madini. Na huo ndio UANAUME. Fanya uasherati wako vizuri tu ila linapokuja swala la familia yako hebu jitahidi sana kuwapa heshima yao na hadhi wanayostahili.

Ukidharau familia yako kwa maana ya ubavu wako yaani nusu yako ya nafsi na mabao yako yaani watoto then umejidharaulisha mwenyewe hapa duniani na hakuna mtu atakayewaheshimu katu.
 
Bibie ukipata mtu mzima mwenzio upo tayari kuishi naye?
Maana sipati picha miaka yote 5 umeishi bila kunyanduana kweli inawezekana?
Kama hutajali karibu inbox tushauriane maana mm ni mstaafu kwa hiyo hekima ninazo na kutosha.
Pole bibie ndio maisha.
Hebu acha Unyanduzi wako hapo.
 
Ukipata mtu ukamuuzia hiyo smartphone unayoitumia...utaweza kulipia watoto chumba chao...japo kwa miezi miwili huku ukiendelea kujipanga...itakuwa imekusogeza mahala....
Sasa kwan Smart phone imeingiaje hapa?! Mbona waafrika huwa tunapenda sana kuwaona watu at their lowest ndipo tunaona wanaweza saidika ila sio kuwasaidia bila kuwakagua.
 
Watu wengine mna kejeli zisizo na maana kabisa. Atauza simu mara ngapi? Huyu msaada mzuri ni kuwa na chanzo cha kipato amabcho atakigemea. Wewe hujui smartphone siku hizi ni kifaa muhimu sana kwenye maisha?
Wabongo wanataka wakati anakusaidia ume haujachana nywele, upo vululu vululu, manguo machafu, umechafuka haujaoga mwezi mzima, umeshinda na njaa ziku mbili, umekondeana hapo ndipo atakusaidia ile ya kinafiki.

Ila umuombe msaada upo na muonekano mzuri hiyo hawakubali. Kama ni mwanamke ataomba mchezo kama ni mwanaume atakupotezea.
 
Amekufanyia ukatili sana, usimsamehe na uzidi kumuombea laana juu yake, waambie na wanao baba yao ushenzi alioufany. Umepitia wakati mgumu sana haileti maana leo kirahisi umsamehe, achana na ushauri wa wapuuzi humu eti msamehe. Achana na huo ushauri.
Tunaangamizwa kwa kukosa maarifa.
Ushauri gani huu
 
Wabongo wanataka wakati anakusaidia ume haujachana nywele, upo vululu vululu, manguo machafu, umechafuka haujaoga mwezi mzima, umeshinda na njaa ziku mbili, umekondeana hapo ndipo atakusaidia ile ya kinafiki.

Ila umuombe msaada upo na muonekano mzuri hiyo hawakubali. Kama ni mwanamke ataomba mchezo kama ni mwanaume atakupotezea.
Mkuu asante. Umesme akweli na umenikumbusha kitu. Nikusahihishe kidogo. Hata ukiwa na mwonekano unaosema hupati msaada. Mbongo anatoa msaada pale anapoambiwa zinatakiwa fedha za jeneza na kusafirisha marehemu.
 
Back
Top Bottom