Niliwahi kumwambia Hayati Magufuli, leo narudia kwa Rais Samia ili asipoteze muda wake

Niliwahi kumwambia Hayati Magufuli, leo narudia kwa Rais Samia ili asipoteze muda wake

Mkuu k
Huko Marekani sera za Bush Jr. na Obama zilikuwa zinafanana?
Kuna kitu ambacho hukijui kuhusu Marekani. Chochote kinachofanywa na Marekani au Rais wa Marekani ni kwa maslahi ya kiulinzi na kiuchumi kwa ajili ya Marekani.Hakuna Rais wa marekani anafanya jambo kwa ajili ya legacy yake km kiongozi bali ni maslahi ya marekani na Taifa linataka Nini.

Marekani akipigana Vita leo siyo mpango wa mwaka mmoja au mawazo ya kimaamuzi ya Rais yeye km yeye Bali Ni mpango wa muda mrefu wa vyombo vya kiintelijensia kukusanya taarifa.

Marekani kila kitu kipo ktk misingi ya kikatiba.Hebu angalia tarehe yao ya KUPIGA KURA ktk uchaguzi mkuu ipo ktk katiba.

Marekani Rais hawezi kuibuka leo anapeleka miswada bungeni kipuuzi puuzi tu kwa maslahi yake .

Mfano Rais yyte wa marekani anayeingia madarakani kwa Sasa anaikuta mezani Kwamba threat ya kiuchumi kwa marekani kwa Sasa ni nchi ya China.Na inaenda hivyo.

Hawabahatishi, consistency yao ni Kwamba Hakuna mtu anaweza kugusa misingi ya taifa sembuse katiba yenyewe.Sera yao ya kiuchumi,kijeshi nk Ni ya kitaifa siyo utashi wa Rais.Wanatembea kwenye mstari japo pengine wew unaweza usione.
 
Huyu jamaa usimsikilize mkuu infantry. Huyu jamaa ni very manupulative in a wrong way. Ni kama anajaribu ku misguide watu.
Anataka kutuaminisha hata ukoloni wa mzungu ulikua sawa tu. Afu intelligence haipimwi kwa kua mpole tu. Kuna njia nyingi za kupima intelligence. Cha msingi ni output. Jpm at the end of the day ametoa positive output na ameleta positive impact na amewaachia watu spirit. Kitendo cha huyu jamaa kuna ku misguide watu na kuwaambia mtu mwenye akili anatakiwa aweje ni kupotosha au kuendelea kushikilia agenda za watu unknown.
Mtu anaweza kua mbabe na bado akawa na akili vilevile kwenye huo ubabe.
Sawa mkuu JF kuna ndugu zetu wa kila namna. Ngoja twende nao hivyo hivyo tu.
 
Alikuwa mgonjwa sana watu walikuwa hawajui tu!! Ndio maana alikuwa anazungumzia kifo sana.
Tofauti na kuropoka. Lakini ni raisi alieleta impact kubwa sana in a long run. Spirit na discipline mindset alio iacha kwa watanzania na waafrika ni kubwa mno. Watanzania ni warahisi sana kuyumbishwa. Mtu akijua tu kupangilia maneno mnamuamini.
 
Umeongea ukweli,hii nchi imejaa watu dizaini ya mtoto wa kambo au yatima kulia Lia tuu na hakuna suluhu huku wakiwaza misaada ya serikali.

Mbaya zaidi kuna watu maskini wengi na wajinga si wanaojiita wasomi au hata wasio soma.

Mama fungua nchi tutoke tupate exposure na tukanyonye wengine nao waje kwetu ,maisha ya kujifunga funga ni kuwa maskini wa milele.

Pili pesa zielekezwe kwenye mambo yenye tija hii habari ya kufurahisha washabiki wajinga wa mwendazake ni wehu,hakuna haja ya kutekeleza miradi ya ma sgr na mingine ya dizaini hiyo kwa pupa
Naam mkuu
 
Uchambuzi mzuri sio haba
You are mis guided brother. True liberation haiitaji kubembelezana. Angalia true liberators wote kina gadafi, lumumba, kwame. Ni watu agressive lakini at the same time
Walikua na akili. Huyu jamaa inaonekana ana standard yake mwenyewe ya kupima intelligence ya mtu. Intelligence ya mtu haipimwi hivo. Inapimwa kwa output impact. Jpm amesababisha impact kubaa sana ndani na nje ya africa. Lakini jamaa anataka ku ignore kila alichokiwekea effort jpm.
 
Tanzania tuna kasumba ya kusapoti viongozi kuwa ndo uzalendo na kupinga sio uzalendo ,viongozi wa nchii hii mpaka wananchi hawajui wanataka nini kutwa nzima kulalamika tu
 
You are mis guided brother. True liberation haiitaji kubembelezana. Angalia true liberators wote kina gadafi, lumumba, kwame. Ni watu agressive lakini at the same time
Walikua na akili. Huyu jamaa inaonekana ana standard yake mwenyewe ya kupima intelligence ya mtu. Intelligence ya mtu haipimwi hivo. Inapimwa kwa output impact. Jpm amesababisha impact kubaa sana ndani na nje ya africa. Lakini jamaa anataka ku ignore kila alichokiwekea effort jpm.
Mbona kuna baadhi ya vitu ametoa pongezi mkuu
 
Jiwe angejua nchi inahitaji zaidi Helicopter za ambulance kuliko uwanja wa chato na mabombadia yake huenda ndugu yako bado angekuwa na mtoto wake mpaka leo.
Kuna ndugu yangu aliwahi kupoteza mtoto katika foleni ya ubungo wakati akiwa anampeleka hospitali. Jamaa ana pesa nzuri tu (maendeleo ya watu) lakini miundombinu mibovu (maendeleo ya vitu) ilifanya apoteze mtoto.
 
Na mabalozi wake wangetumuliwa pia, lakini hata kwa Kiduku Kim Jong wa Korea bado kuna mabalozi wa nchi nyingi tu za Ulaya.
Angekuwa hawapendi wazungu, angewafukuza mabalozi basi mkuu. JPM alikuwa anataka fair play kati ya Tanzania na nchi zingine.
 
Gaddafi na Kwame Nkurumah walikuwa madikteta na wote waliondolewa kwa aibu katika nchi zao.
You are mis guided brother. True liberation haiitaji kubembelezana. Angalia true liberators wote kina gadafi, lumumba, kwame. Ni watu agressive lakini at the same time
Walikua na akili. Huyu jamaa inaonekana ana standard yake mwenyewe ya kupima intelligence ya mtu. Intelligence ya mtu haipimwi hivo. Inapimwa kwa output impact. Jpm amesababisha impact kubaa sana ndani na nje ya africa. Lakini jamaa anataka ku ignore kila alichokiwekea effort jpm.
 
JPM hakuwa malaika yule. Yeye pia ni mwanadamu na ana mapungufu yake mengi tu.

Ww ndio unasema, dhalimu alikuwa anajiona kama masiha wa nchi hii. Wajinga, wasomi uchwara, wajasiriatumbo na makatili walikuwa wanamsifia ile mbaya. Na alishurutisha kuonekana kuwa ni mzalendo wa kweli, kumbe jizi la kura na ibilisi tu.
 
Angekuwa hawapendi wazungu, angewafukuza mabalozi basi mkuu. JPM alikuwa anataka fair play kati ya Tanzania na nchi zingine.
Hakuwa na uwezo huo. Hata wazungu walijua he was just stupid with no impact.

Na kuthibitisha hilo, Tundu Lissu ( Mwanasiasa ambaye Magufuli alimchukia to the moon ) alihifadhiwa kwenye ubalozi wa Ujerumani na badaye wazungu wakamsindikiza kwenda Airport kupanda ndege mchana kweupeee huku akihitajika mahakamani.

Hao wazungu baada ya kumsindikiza wakarudi ubalozi na wako hapa hapa na hakuna kitu Magu angeweza kuwafanya.
 
Pili mikodi mingi,mikubwa na ya kinyonyaji haiwezi kusogeza nchi mbele.

Ningekuwa kwenye nafasi ya kushauri mambo ya uchumi basi ningeshauri kupunguzwa kwa kodi hasa VAT na kufuta ushuru za kijinga mfano vitambulisho vya machinga na tozo za kwenye madini ya ujenzi kwa uchache tuu.

Ningewekeza zaidi kwenye miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege strategic huku Nikiviwekea miundombinu stahiki.

Ningeipa nguvu sekta binafsi yaani kiufupi ningejenga demand side Ili ichochechee production na kwa njia hiyo ndani ya miaka 2 ningeanza kupata pesa nyingi kwa njia ya kodi
Hapa nakataa mkuu. Jpm alikua anataka fair business kati ya tanzania na nchi nyingine. Alitaka wananchi wawe na thamani sawa na foreigners. Na kutoa dhana ya cheap labour.
 
Tanzania tuna kasumba ya kusapoti viongozi kuwa ndo uzalendo na kupinga sio uzalendo ,viongozi wa nchii hii mpaka wananchi hawajui wanataka nini kutwa nzima kulalamika tu
Jpm was in a right direction. Kubali tu mkuu. Hata kama hakua smart jinsi ulivotaka ww. Tofautisha kuwa evil smart na kua mzalendo. Its better kua mzalendo. No matter how much upo smart. Lakini kama una misguide wananchi bado hai count.at the end of the day wananchi watakudai basic needs, justice, employment, land
 
FIWAHI KUMWAMBIA HAYATTI MAGUFULI, LEO NARUDIA KWA RAIS SAMIA, ILI ASIJEPOTEZA MUDA WAKE.

Na, Robert Heriel

Niliwahi kuandika hapa miaka mitatu iliyopita, niliipa makala ile kichwa kisemacho "Rais Magufuli unapoteza muda wako tuu" katika makala ile watu wengi walinitukana, wengine walinitishia, sikuwalaumu kwani niliwaelewa lakini wao hawakuwahi kunielewa.

Leo hii narudia baadhi ya maneno yaleyale niliyoyasema siku zile.

Niliandika Magufuli anapoteza muda wake nikiwa na hoja zifuatazo;

1. Magufuli nilimuona anapoteza muda kwa sababu alikuwa na mtazamo kuwa, nchi ni tajiri na itapata maendeleo kwa sababu ina Rasilimali nyingi akizitaja kama madini, mbuga, ardhi kubwa yenye Rutuba, maziwa na mito yenye viumbe maji kama samaki, vivutio vya utaliii, bahari, kuzungukwa na mataifa mengi yasiyo na bahari, n.k.
Niliona anapoteza muda kwa sababu, nchi haiendelei kwa wingi wa Rasilimali isipokuwa inaendelea kwa ya kuwa na WATU WENYE AKILI. Watu wenye akili ndio wanaleta maendeleo nchini sio uwepo wa Rasilimali nyingi.

2. Magufuli aliamini, nchi itajengwa kwa kuwanyonya wananchi wake pekee, ndio maana alishindwa kuongeza mishahara miaka yake yote aliyotawala, pia akashindwa kutoa ajira mpya.
Kama hiyo haitoshi, sio ajabu aliongeza vikodi vya hapa na pale ili kuendesha serikali yake, lakini bado mambo yalimuwia magumu hali iliyomfanya ajiingize katika hatari ya kugombana na wafanyabiashara, wengi wao aliwaita wahujumu uchumi, wapo walioisoma.

Mimi nilimwambia nchi yoyote iliyoendelea haijawahi kuendelea kwa kutegemea unyonyaji kwa watu wake pekee, bali ni lazima ivamie mataifa mengine. Nilitoa mifano kwa baadhi ya mataifa yaliyoendelea yaliyojipatia utajiri kwa kunyonya watu wake na mataifa mengine.. Biashara ya utumwa, Ukoloni, na ukoloni mamboleo vyoote vinaangukia hapa.

Taifa kama la Korea ya kusini loo, liliamua kualika mataifa mengine hasa Mataifa ya Magharibi kuja kuwekeza Korea kusini. Kwa sasa Korea ni moja ya nchi zilizopo ulimwengu wa pili.

3. Magufuli aliamini kuongoza nchi kibabe ndio suluhu ya maendeleo, wakati mbinu hiyo ilishapitwa na wakati, na kwa vyovyote lazima ingelala upande wake na angeshindwa, licha ya kujitutumua kuchelewesha muda wa anguko lake.

Mimi nilimwambia kuwa kizazi cha sasa kinaongozwa kwa akili, ujanja, maarifa na mambo yote yahusuyo akili. Ubabe ungeweza kutumika machungani kwenye mbuzi, ng'ombe, na kondoo ambao hawana utashi kama binadamu.

Hakuna uhusiano wa karibu baina ya Ubabe na biashara, hivyo kivyovyote vile anguko la kiuchumi lilikuwa ni uhakika. Kwani hakuna mfanyabiashara ambaye angependa aishi kwa hovyo wakati pesa ni zake mwenyewe.

4. Magufuli aliamini kuwakaripia wengine mbele ya halaiki na wengine kuwatukana ndio namna ya kuleta nidhamu ndani ya serikali yake.
Wakati nidhamu ndani ya serikali hutokana na jinsi sheria zinavyofuatwa na kutelekezwa. Kama mtu ni mwizi basi sheria ingechukua mkondo wake,

Masikini wengi na watu walioshindwa walifurahishwa na magufuli kwa sababu ni kawaida ya masikini kuona mwenye nacho akianguka.

5. Magufuli aliwekeza zaidi kwenye matamko kuliko kuweka mfumo imara ili hata yeye akiondoka mambo yatajiendesha vyema.
Niliwahi mwambia kuwa One manshow ni kama mbio za sakafuni ambazo lazima ziishie ukingoni. Nilimwambia anapoteza muda wake.

Maendeleo ni mfumo kama mnyororo unaounganisha seti nyingi ya vitu.
Maendeleo ya nchi za Afrika niya kubahatisha kwa sababu hakuna mfumo unaoeleweka.

6. Magufuli aliwekeza zaidi kwenye kujipa promo kwenye vyombo vya habari na kujisifu, na kuwazima wengine ili kuchota akili za watu wenye upeo mdogo na kuzuia wale waliokuwa wanampa challenge kwa mitazamo yao.
Hii pekee ingetosha kuonyesha kuwa anapoteza Muda wake.
Hakuwa mtu kama Anthony Mtaka ambaye hafanyi manipulation lakini matendo yake yanaonekana.

7. Magufuli alifanikiwa zaidi katika kutekeleza na kusimamia maendeleo ya miundombinu, kwa hili nampa heko, lakini nilimuambia kuwa taifa masikini linawekeza kwenye watu na sio vitu,
Hii watu walinipinga lakini huo ndio ukweli mchungu, masikini kuwekeza kwenye vitu zaidi ya watu ni kupoteza muda na kuwatesa watoto.

8. Magufuli alijitahidi kujifanya hawapendi Wazungu na kila mara alitoa maneno ya kupata ushawishi kwa watu ili wawachukie wazungu. Ndio maana hata Mambo ya Corona aliyaona kama mchezo wa kuigiza na njama za wazungu kutuangamiza.

Jambo ambalo hata mtoto mdogo akifikiri anaona ni uongo wa mchana.
Nilimuunga mkono kwenye suala la kutokuweka Lockdown, lakini masuala mengine nilimpinga.

Magufuli angepoteza muda kwa vyovyote kwa kupinga mambo ya wazungu ambayo hata huo Urais aliokuwa nao ni mfumo wa kizungu, masuala ya jeshi ni mifumo ya kizungu, jina lake lakizungu, dini yake yakizungu na hata alipokufa alizikwa kizungu, hata elimu yake ni yakizungu, hata magari na vifaa vyote alivyokuwa akivitumia ni vyawazungu, achilia mbali madawa na miwani aliyokuwa akivaa. Sijazungumzia silaha na wana usalama waliokuwa wanamlinda ambao ili wawe wa kimataifa inapaswa wapewe mafunzo ya kizungu.

Kama wazungu wangetaka kutuua wangetuua tangu miaka ya 1900 huko walipokuja kututawala. na hata wakiamua kutuua uwezo huo wanao, na hatuna uwezo wa kufurukuta.

Sasa mambo hayo hayo, nayasema kwa Rais Samia, kuwa aangalie asije akapoteza muda wake kwa kushindwa kuendana na wakati.

Maendeleo ya nchi ya USA sio lazima yawe maendeleo kwa Tanzania. Hiyo ni muhimu kuzingatiwa.

Hata hivyo Rais Samia lazima azingatie haya ili naye asijikute katika kucheza Nage na kupoteza muda wake.

1. Maendeleo ni kuwekeza kwenye watu
2. Kuwekeza kwenye watu ni kuwapa Uhuru
3. Uhuru wa watu ni pamoja na kuwapa nafasi ya kuyafurahia maisha yao kwa kutumia rasilimali za nchi yao au kuvamia mataifa mengine. Passport zitolewe watu wakahangaike huku na huko.
4. Serikali isifikiri kunyonya wananchi wake pekee(kodi na ushuru) bali pia ifikiri namna ya wananchi wake kuenda nchi zingine kunyonya mali na utajiri wa nchi zingine.

5. SHeria na utawala bora zisiachwe
6. Ubabe wa kipumbavu uachwe maana palipo na ubabe au udikteta lazima kuwa na uasi/usaliti na palipo na usaliti lazima pawe na mapinduzi.

7. Serikali isijikite kwenye matamko ya kipuuzi puuzi. Kwani kwa kufanya hivyo itaathiri vijana wengi ambao wao kila kitu watataka tamko la serikali.

Sishangai kwa nini watu wanamlaumu Mama kuwa kwa nini ni mpole, ni kutokana na kuathiriwa na matamko yasiyo na kichwa wala miguu.

Sio kila kitu kitolewe tamko kwa kutafuta sifa za kijinga kwenye Kamera ili ionekane kazi inafanyika wakati hakuna kitu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa, Dar es salaam
Nilikuwa nakusoma Sana Ila ulipotea kwa ghafla mpaka nikadhani pengine ile timu ya Mwendazake ya WASIOJULIKANA imekupoteza. Karibu Sana ROBERT HERIEL
 
Tajiri muungwana kama MO Dewji au mzee Reginald Mengi wakianguki mimi masikini siwezi kufurahi hata kidogo.
Unesahau ile kauli "... matajiri wataishi kama mashetani ilivyowafurahisha maskini?" Umesahau waliokuwa wafanyakazi wa QG walivyoshangilia anguko la tajiri yao? Leo wengi wanalia na kusaga meno maana Bwana yule alifunga biashara zake na wao wakapoteza ajira... wengi wao wanapanga bidhaa barabarani siku hizi ili wajikimu...
 
Gaddafi na Kwame Nkurumah walikuwa madikteta na wote waliondolewa kwa aibu katika nchi zao.
waliondolewa kwa kupigania wananchi wao, je huo ni uovu? Kama fight against corruption and african enemies ni uovu then wema ni upi?
 
Back
Top Bottom