Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

kaka we shika nilivyokuambia, kichwa kiangalie mnakotoka na miguu mnakokwenda. Nina mambo mengi tu kwa mfano ukitaka namna ya kumkamata mwanga ama mchawi akiingia nyumbani kwako sema tu nikumwagie hapa, dawa za kumvuta mwanamke ama mwanaume akufuate popote ulipo hata kama ni usiku ninazo pia, ila haifanyi kazi kwa mke / mme wa mtu - sina uchoyo na hii elimu maana na mimi nilipewa bure.

Masuala ya kazini pia yako - vyeo, mshahara nk
Bro... PM yangu ipo wazi
Hio dawa ya kumvuta dem yoyote ipo?😀
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A.

Mkichimba kaburi miminieni udongo mloleta kutoka eneo B, bakisheni kidogo. Jeneza likishawekwa chini kaburini ule muda wa kuweka udongo malizieni na ule mlobakisha.

Muhimu kukumbuka udongo ulioletwa ufike siku moja au zaidi kabla ya maiti kutolewa mortuary. Kwenyw udongo ule kuwe na mawe madogo madogo kadhaa. Chukueni jiwe moja miliweke kwenye gari itakayosafirisha maiti kutoka mortuary mpaka makaburini.

Baada ya shughuli yote kukamilika. Gari lililombeba marehemu lisiende nyumbani kabla halijaoshwa. Lioshwe na mtu/watu baki (wasio ndugu) prefferably kwenye Car Wash za mitaa jirani au mtoni. Yule ndugu aliefuata udongo eneo B asiende kwake moja kwa moja baada ya msiba, wengi hupitia Bar kuzuga zuga walau three hours hivi, ikiwezekana kulipia lodge akaoge huko kwanza itapendeza.
Duh! Aiseeee.
 
andaa mshumaa
andaa sindano
andaa kitambaa cheupe
andaa tunda unalolipeda sana kulila
andaa udi
andaa chumvi ya mawe

ukimaliza kuviandaa ni PM tumalize kazi.
Inafanya kazi kwa anayevutwa akiwa nje ya nchi? Nauliza tu jamani nataka kutesti mitambo
 
andaa mshumaa
andaa sindano
andaa kitambaa cheupe
andaa tunda unalolipeda sana kulila
andaa udi
andaa chumvi ya mawe

ukimaliza kuviandaa ni PM tumalize kazi.
Mishuaa kila Rangi nmeandaa
Sindano tayari
Kitambaa kipo
Parachichi tayari (au tunda la kimasihara?)
Udi zipo Aina nne tofauti
Chumvi tayari
Aya Twende kazi au na nyanyo za pisi pia zinahitajika??
 
wakuu sasa chagueni moja kwanza - tukimaliza tunaingia nyingine.

Ya kumteka boss:
Leta majina yake yote matatu
Ulete karatasi yoyote aliyoandika kwa mwandiko wake
kata kipande cha nyuzi ama kibao kidogo hata kwa wembe kwenye kiti chake anachokaa ofisini
mshumaa
Mafuta ya maiti... kumfanya ndondocha wako

Mengine ni siri -- Pm tumalize kazi

Baada ya hii kazi Boss atakuwa anakusalimu kwanza kila akifika asubuhi ofisini.
Mbna unaruka ruka mkuu tuanze na ile ya wanawake si ata Paula Kajala Dua tu au yule dawa haiswiii??
 
Mbna unaruka ruka mkuu tuanze na ile ya wanawake si ata Paula Kajala Dua tu au yule dawa haiswiii??
[emoji23][emoji23][emoji23]ni process ndefu japo ni jambo linalo fanya kazi kwa uhakika endapo likifanywa kwa usahihi
 
Asikudanganye Mtu popote pale ulipo kuwa kauli za Watu waliokufa namaanisha Marehemu wakizisema huwa hazitimii. Ni kwamba huwa hawatanii kabisa na wayasemayo hutokea na hutimia.

Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.

Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.

Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.

Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.

Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.

Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.

Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.

Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.
Kiufupi-Kuna taratibu ambazo watu hufanya ili marehemu akubali kuzikwa kule alipokataa pasipo changamoto yoyote.Binadamu anayeishi ana nguvu asikwambie mtu
 
Kabisa!

Niliona Live kipindi fulani marehemu alichotaka hakikusikilizwa ikawa balaa.Double coaster mpya ikafa engine njianiTukakokotwa na roli mpk kufika maiti ishaoza.Pale church anaombewa likatokea balaa gani sijui.

Mda wa kuzika jamaa wanashusha jeneza taratibu kamba ikakatika likaanguka ndani paaa.Ikabidi niwashtue marehemu kakasirika hataki kuzikwa hapa tieni udongo tutimke haraka sana.
Kuna watu ambao wana imani,kiasi akim-command marehemu hutulia.
 
wakuu sasa chagueni moja kwanza - tukimaliza tunaingia nyingine.

Ya kumteka boss:
Leta majina yake yote matatu
Ulete karatasi yoyote aliyoandika kwa mwandiko wake
kata kipande cha nyuzi ama kibao kidogo hata kwa wembe kwenye kiti chake anachokaa ofisini
mshumaa
Mafuta ya maiti... kumfanya ndondocha wako

Mengine ni siri -- Pm tumalize kazi

Baada ya hii kazi Boss atakuwa anakusalimu kwanza kila akifika asubuhi ofisini.
Naona umerithi mikoba ya mshana
 
kaka we shika nilivyokuambia, kichwa kiangalie mnakotoka na miguu mnakokwenda. Nina mambo mengi tu kwa mfano ukitaka namna ya kumkamata mwanga ama mchawi akiingia nyumbani kwako sema tu nikumwagie hapa, dawa za kumvuta mwanamke ama mwanaume akufuate popote ulipo hata kama ni usiku ninazo pia, ila haifanyi kazi kwa mke / mme wa mtu - sina uchoyo na hii elimu maana na mimi nilipewa bure.

Masuala ya kazini pia yako - vyeo, mshahara nk
mkuu tumwagia mchele basi nasi tutafune
 
Binafsi hatukuweka jiwe ila tuligehza jeneza mbele nyuma nyuma pakawa mbele ili marehemu asitusumbue napo cha moto tulikiona.Msiba ulifika kwa tabu sana na maiti ilikua inalia machozi kabisa ma shingo ilikua imeangalia pembeni.Kaburi lilichimbwa matatu maana mawe makubwa yalikua yanajitokeza kuzuia kuzikwa.ikafanyika mila ndio kaburi la nne likawa saaa akazikwa.Ila cha moto tulikiona
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A.

Mkichimba kaburi miminieni udongo mloleta kutoka eneo B, bakisheni kidogo. Jeneza likishawekwa chini kaburini ule muda wa kuweka udongo malizieni na ule mlobakisha.

Muhimu kukumbuka udongo ulioletwa ufike siku moja au zaidi kabla ya maiti kutolewa mortuary. Kwenyw udongo ule kuwe na mawe madogo madogo kadhaa. Chukueni jiwe moja miliweke kwenye gari itakayosafirisha maiti kutoka mortuary mpaka makaburini.

Baada ya shughuli yote kukamilika. Gari lililombeba marehemu lisiende nyumbani kabla halijaoshwa. Lioshwe na mtu/watu baki (wasio ndugu) prefferably kwenye Car Wash za mitaa jirani au mtoni. Yule ndugu aliefuata udongo eneo B asiende kwake moja kwa moja baada ya msiba, wengi hupitia Bar kuzuga zuga walau three hours hivi, ikiwezekana kulipia lodge akaoge huko kwanza itapendeza.
Duh,mitihani sana
 
Back
Top Bottom