Nimeamini safari ya kuitafuta na kuishika ml 100 as cash ni ngumu mno. Najitaidi lakini yataka moyo!

Tuache kujifariji.
Sema usemavyo umasikini ni mbaya ndugu yangu
Mkuu fanya utafiti vizuri.
Ukifuatilia katika jamii utaona wenye vipato vya chini wana furaha zaidi kuliko wenye vipato vya juu.
Chunguza kwenye mitaa ya uswahilini utaona kila baada ya siku 3 kuna sherehe na watu wanajiachia halafu baada ya hapo nenda kwenye mitaa ya matajiri utakuta hata majirani hawasalimiani kila mtu anaugulia na stress zake kimyakimya.
Kwa mfano mimi zamani nilikuwa na mawazo kama yako kwamba nikijitafuta nikajipata nitakuwa mtu wa furaha lakini cha ajabu kadri ninavyozidi kupanda level ya maisha naona stress ndio zinaongezeka na amani ya moyo inapotea.
 
Mkuu unajua sana kucheza na saikolojia zetu.. yan unajua sana kutupa moyo masikin 😅
 
Umasikini unamfurahisha mtu mjinga.
Yaani uishi makazi duni, watoto wasome shule za kayumba, utembee Kwa mguu, mlo wa shida, ukiumwa huna pesa za matibabu, huna cha kusaidia.
Then upo tu eti umasikini ni mzuri kuliko utajiri halafu tukuone upo timamu kichwani
 
We uliweza vipi kukusanya vibunda vyote hivyo mpaka vifike 56 wakat mi 100k inasumbua kukusanyika?[emoji23]
Mkuu 56m sijawahi kua nazo cash na siwezi kwasbb nikipata tu kdgo lazima niwekeze kwenye biashara tena pesa halali mkui
 
Baada ya miaka 10, 2034 utakuwa tayari na 100M. Ukiziacha huko huko UTT

Kwa sasa hivi endelea na harakati nyingine. Hiyo 56M, achana nayo wala hutakiwi kuifikiria.
Hilo na mimi ndio linanisumbua kuna mzigo wa maana upo utt, kweli unaongezeka kila siku.. Shida zipo nyingi, najiuliza kila mara je nitoe kiasi fulani nisolve mambo yangu fulani.?.. Roho nyingine utapunguza ule mzigo.. Nipo njia panda
 
Mkuu unachanganya mada.
Hakuna mahali palipoandikwa umaskini ni mzuri kuliko utajiri,tunachofanya hapa tunalinganisha kati ya matajiri na maskini ni gani wenye furaha zaidi.
Lakini pia hakuna mahali tuliposhauri kwamba ikija fursa ya oesa au ya kutajirika uiachie makusudi la hasha hiyo ni mada tofauti kabisa
 
I am the chief comforter,
You are welcome😃
Ujue nilichokuja kugundua, kuwa na raha au furaha ni suala ambalo unaweza tu ukalitengeneza mwenyewe. Haijalishi una pesa au hauna japo ukiwa nazo hil zoez huwa rahis zaid.
Pia pesa au umasikin vule vile huweza kusababisha mtu kuwa na stress japo ukikosa pesa hil zoez huwa ni jepes zaid.

According to stoic wisdom ,furaha ya mtu/watu hujengwa na na ile hali ya utayari na kuridhika kwao kwa vile walivyo navyo on hand bila kutazama vitu gan wanataman wawe navyo au wanataraji wavipate au vitu vipi hawana. Uki focus kwenye gratitute and being content with whatever u have, being grateful , unaish maisha ya furaha sana. Nafikir hapa mdipo watu wa hali ya chini (masikini kama wanavyoitwa) huko uswahili ndivyo wanavyoishi na kuwa na amani na furaha kwa kile kidogo walicho nacho
 
Yeah upo kwenye point.
Kuna Boss wangu mmoja hivi mkenya alikuwa anapenda kunisisitiza hili jambo akawa ananipa mfano fulani hivi.
Alikuwa ananiambia kwa mfano wewe umeajiriwa mahali na mshahara wako ni wa kawaida tu siku ukishapokea mshahara ukachota kiasi fulani cha mshahara ukaenda kununua kuku utakuwa na furaha nyingi kumzidi mtoto wa Rais ambaye kwao kila siku mafriji yao yamejazwa kuku na vyakula vingine kila wakati kwake hakuna maajabu anaona kawaida tu.
Sijui huu mfano nimeeleweka
 
THERE IS ONLY ONE WAY WHICH MONEY MULTPLY, IS BY INVESTING. NOT SAVING
 
Nimekuelewa sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…