Nimeshaanzisha kampuni yangu, nataka niwe napata tender za serikali nifanyeje?

Cheki kwanza tender kwenye mashirika na asasi mkuu kama mtaji wako upo reasonable. Shida ya serikali pesa hukaa kwao muda mrefu, serikali usiiweke sana kwenye shabaha zako, inakopa sana watoa huduma na makandarasi.
Kama unataka ugavi au ujenzi nakushauri anzia Kigoma kambi za wakimbizi, kuna mashirika siyataji kule tenda zipo kibao uwe na mtaji tuu mzuri na connection ambayo utaitengenezea kule kule.
Nimetokea kule binafsi wakati najitafuta back in the days baada ya chuo.
Hongera kwa kupata maono ya kuwa na kampuni, hatua kubwa.
 
Pamoja sana mkuu, nitakupm
 
Azingatie sana huu ushauri.
Maana anaweza akawa anaomba ushauri kwa watu ambao hata kazi hawana wala ajira wala biashara wapo wapo tu.
 
Hii nimeipenda
 
Kuna kamsemo kamoja kutoka Kwa gwiji Mmoja wa siasa za bongo kanafanana na "Liwa kwanza ndio ule"

Huko lazima uwe na pesa na uwezo wa kisaamehe madeni pia, huko sio kama biashara za sokoni lipa kwanza ndio update huduma au bidhaa. Huko toa huduma tukutane mwakani na Chao walishachukua mapema.

Kila mkuu akibadirika utaanza kudai Mwanzo Kwa kuonesha vielelezo unaweza kwenda Hata miaka mitano. Ila uhakika serikali haidhurumu mtu.
 
Tuanze na haya maswali hapa:
1. Kwanini mmesajili kampuni?
2. Hao wamiliki wenzako mmekosa mawazo yakujua muanzie wapi?

Ila naona kama mmekimbilia mbali sana kusajili kampuni, wengi wanafikiri tenda za serikali lazima kuwe ni kampuni ila bado zipo tenda wanaingia proprietors na partnerships pia. Kampuni ni gharama zisizo na ulazima hasa kwa wanaoanza.

Samahani mchango wangu upo nje kidogo ya uhitaji wko ila nimeona nikupe alarm kichwani Mkuu.
 
Hukuwasikia wazabuni wakilialia mbele ya Makonda wakurugenzi wameatamia mapene yao hadi benki zinapiga minada mali zao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…