Nina Mgogoro kwenye ndoa, kila pesa anayopata Mke wangu anaenda kujenga kwao. Naomba msaada

Nina Mgogoro kwenye ndoa, kila pesa anayopata Mke wangu anaenda kujenga kwao. Naomba msaada

Mleta uzi wewe ni fala, na umedanganywa na mkeo, na ameshakudanganya vitu vingi, na alitengeneza mazingira ya wewe kumuamini, kapata alichokipata sasa ni muda wako kuisoma namba, hiyo nyumba anayojenga ni ya kwake kala njama na mama yake kukutapeli, nenda wachunguze na hao watoto kama ni wako

Haya maneno ni ya mzee kitombile huwa hakosei, shauri yako....KATAA NDOA NDOA KWA AFYA YA AKILI NA MWILI.
 
Unafikiri ndio.ukioa wa hivyo utamkontrol!?

Atakuigizia tu muda ukifika atakuonyesha upande wa pili!!

Nakuambia siri wanawake wasomi huzitafuta ndoa kwa nguvu sana na huzipata wakishazipata ndio utashangazwa na sarakasi zao zao!!!
😂😂😂😂eti sarakasi zao🙌
 
Nipo kwenye ndoa nimekuwa nikisoma tu lakoni naona na mimi limenikuta.

Iko hivi wife na mimi tulifahamiana kijijini. Nilikuwa f6 yeye akiwa f4 leaver. Nilimsaidia akapata chuo cha takwimu akaenda akafanya akapata cheti. Wakati akiwa chuo nliamua kudate nae tukaoana (marriage) nikiwa nafanya kazi na yeye akiwa chuo.

Miaka mitatu baadae tulijaaliwa watoto wazuri. Maisha yaliendelea nikiwa kazini na yeye akiwa ofisi moja masuala ya takwimu nchini.

Mambo ya ndoa yalikuwa safi sana nilii injoi ndoa labda kwa sababu ilikuwa ya kusafiria. Maana yeye mkoa mimi mkoani.

Nilifanikiwa kumuhamishia mkoani kwangu yeye na watoto. Tuliishi vizuri kwa wastani wa miaka 5. Baadae mzazi wake yaani mkwe aka experience wakati mgumu (code). Tukashauriana tumjengee kibanda. Kwa kuwa wapo watoto wakubwa wakaona washirikiane wote. Kwa kuwa wife nde mwenye kipato kizuri akakopa banki 27M lakini nyumba haijaisha.

Kero ikaanza sasa. Kila wakati anataka pesa ya ujenzi kwa mama mkwe. Kumbuka yule ni mzee ile nyumba watakuja kugombana watoto nikamwambia ujenzi hauishi siku moja. Buy time.

Majuzi alipata bingo ofisini kwao 20 Mil ni pesa ya offer ya Serikali yenye riba kidogo.

Lahaulaaa si akaipeleka yote kwenye ule ujenzi.

Wana JF wenzangu, kumbuka si kwamba sisi na watoto wetu hatuna mahitaji, hapa ada, nyumba haijaisha asilimia Mia. Why apeleke 20 kwao? Mwanamke kiumbe wa ajabu sana.

Hivi? Hajui ile nyumba hawataishi watoto wake? Hivi hajui ile nyumba watagombea vidume?

Ndani ni kuchuniana. Najuta sana kuoa mwanamke huyu.

Niko puzzled. Epuka kusomesha mchumba.
Huu ni mwanzo wa maafa, Kila jambo huanza taratibu na likianza kukomaa manun'guniko huanza. Kumbuka kuna habari nyingi za watu kuumizana hata kufikia kutoana uhai sasa swala lako umelileta hapa je huko mbele unaona kinacho jiri? Upande wangu nahisi kuna ulemavu + damu. Uwe makini.
 
Wazee hawapo? Je hao washenga huna habari nao? Vipi kuhusu wazazi wenu? Usimweke mkeo humu ni sawa na wewe kuvua nguo mbele ya mkweo wa kike. Futa hii kitu ulio weka.
Huu hajafika kiwango cha kuitwa mgogoro ila ni mitazamo na kama Mwanaume umeshidwa kuongoza vyema sasa jifunze darasa la uongozi wa ndoa halafu rudi kuongoza familia. Jua resources ulizonazo na unazoweza kuwa nazo zigawanye sawasawa. Muonyeshe uongozi naye atafuata
 
Pole mkuu, nakushauri tu muache mkeo ajenge kwao! Na wewe Jenga kwako! Mwanaume hudumia familia yako kwa kuhakikisha wanaishi pahala pazuri na panapofaa!

Acha na hela ya mkeo maana SIYO YAKO

Mimi nilikopa fedha nikajazia ujenzi wa nyumba anayojenga mume wangu maana ni familia moja, matokeo yake amekuja kunitemgenezea maneno ya kashfa machafu yasiyo faa!

Mkopo ukiisha, nachukua mwingine na NITAJENGA KWETU ili siku tukiachana niende kwetu kwa raha! Wanaume mna matatizo sana ACHA MKEO AJENGE KWAO, wewe Jenga KWAKO.

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
Na yeye ajenge kwao, sio kwake. Akijenga kwake patakua pa wote. Ajenge kwao na sio kwake
 
Nimeona wengine wakimtetea mke wengine mume

Iko hivi kipato cha mke na mume ni cha familia au wanandoa sio cha wazazi, ndugu au wanaukoo

Kihalisi pesa yoyote ya familia (ya mke au mume) hasa kiasi kikubwa kabla hakijatoka na kufanyiwa matumizi lazima mume na mke wakae washauriane na kukubaliana

Hii ndio silaha pekee ya kuepuka migogoro ya pesa kwenye ndoa
Nami nakuunga mkono ktk hili nashangaa kuona wanaomuunga mkono mwanamke.
Kwa hili wanaume tumebaki wachache. Sikatai mwanamke kutuma fedha kwao lakini si kwa kiasi kikubwa kama alivyotuma mke wa mtoa mada.
Kwangu binafsi siwezi kukaa na mwanamke wa namna hiyo ni bora na kutokuwa na mke
 
Nami nakuunga mkono ktk hili nashangaa kuona wanaomuunga mkono mwanamke.
Kwa hili wanaume tumebaki wachache. Sikatai mwanamke kutuma fedha kwao lakini si kwa kiasi kikubwa kama alivyotuma mke wa mtoa mada.
Kwangu binafsi siwezi kukaa na mwanamke wa namna hiyo ni bora na kutokuwa na mke
Anafaa afunguliwe macho ya rohoni kabla hajatolewa roho na mtoa roho anae lala nae kwa kitanda 1.
 
Kama anajenga kwa pesa yake ni sawa,huo mkopo atalipa yeye..wewe pesa yako jenga hiyo yako,ingekua ni mimi ningemwacha ajenge kiroho safi
Umeona ee kama pesa ni yake amwache ajenge tu
 
Nimeona wengine wakimtetea mke wengine mume

Iko hivi kipato cha mke na mume ni cha familia au wanandoa sio cha wazazi, ndugu au wanaukoo

Kihalisi pesa yoyote ya familia (ya mke au mume) hasa kiasi kikubwa kabla hakijatoka na kufanyiwa matumizi lazima mume na mke wakae washauriane na kukubaliana

Hii ndio silaha pekee ya kuepuka migogoro ya pesa kwenye ndoa
Siku hiz hamna ndoa. Ni kusogezana tu muishi siku ziende ndio maana haya yanatokea. Mnapokua mume na mke ni mwili mmoja ki roho. Linapokuja mke anafanya yake bila mume kukubaliana, ndoa inakua ndiano.
 
Wewe unaGombana na mkeo kwa jambo la kijinga sana,unataka asijenge kwao!? Ishini na wake zenu kwa akili,mimi mke wangu juzi kakopa milioni 10 akaenda kukarabati nyumbani kwao ilikhali sisi tuko katika nyumba ya kupanga.
Pigia mstari neno ishini nao kwa akili.
Poleni sanaa
 
Af,ukute kijijini kwenu kuna kamdada kalikuwa kakikulilia usiku kucha,kanakuja kwenu kusomba maji na kufagia uwanja,ukakaona kanini. Kanaishi maisha ya kifukara,lakini kamerishika kana raha. Wewe umetafuta pisi kali,eti imesoma. Haya,ona sasa. Na bado. Ngoja kesho utaambiwa anataka kwenda saluni,vyupi vimechakaa. Ukitoa ya mboga tu,inaenda saloon anao wanalala njaa. Dadeki.
Na kugawa utelezi Kwa masela huu! Dadeki.
 
😂😂😂pole Mkuu,ndoa nyingi zimegeuka msiba sikuhizi....wanaume kwa wanawake wapo katika mateso makali sana
Dawa ni moja tu kuwazalisha halafu unamwambia ndoa itafungua tukizeeka!!Kwa sasa tuna nguvu tutasumbuana!!

Unamuacha njia panda TU!!
 
Sikilizeni nyie na ujinga wenu wewe na mkeo mnaandalia hao watoto maisha magumu na mtawapa tabu hapa duniani kwa ujinga wenu.

Kama mnapenda watoto wenu basi jengeni kwenu kama familia kwanza halafu ndio mfuata ndugu na wazazi...Mkianza kushindana hapo ndoa inavunjika watoto wanapata tabu kwa ujinga wenu.
 
Hela yake mwenyewe muwache atumie anavyotaka
 
Nimeona wengine wakimtetea mke wengine mume

Iko hivi kipato cha mke na mume ni cha familia au wanandoa sio cha wazazi, ndugu au wanaukoo

Kihalisi pesa yoyote ya familia (ya mke au mume) hasa kiasi kikubwa kabla hakijatoka na kufanyiwa matumizi lazima mume na mke wakae washauriane na kukubaliana

Hii ndio silaha pekee ya kuepuka migogoro ya pesa kwenye ndoa
Wachache wataelewa mkuu.
 
Back
Top Bottom