Nini chanzo cha wazazi wa kiafrika kuwaandaa watoto ili waje wawasaidie?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Mpja kwa moja kwenye mada
Wazazi wengi wanakomaa kulipa ada kubwa na kujitoa muhanga kiuchumi ili watoto wao wasimame. Kusudi lililojificha nyuma ni ili mtoto wao akifanikiwa awasaidie kimaisha.

Wazazi wanavizia mahari za watoto wao wa kike. Wanapambana watoto wa kike waolewe na wenye uwezo ili na wao wanufaike na sadaka za mkwe.

Mzazi mmoja nimemuona hadi anafukuza mke wa mtoto wake akidai huyo dada anania ovu za kutaka kuchukua mali za mtoto wao.

Hii tabia kwa mtazamo wangu ni miongoni mwa chanzo cha umasikini.

Sisi watumishi tunaamini ni Jukumu la mzazi kuacha urithi kwa watoto na wajukuu wake na sio kuvizia urithi wa watoto wake.
Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.
Mithali 13:22


Wazazi tubadilike. Tuanze kupambana kutafuta mitaji ya watoto wetu sio kusubiri mahali za watoto.

Tupambane kutafutia watoto makazi bora sio kuvizia waje watupe makazi bora.

Huu utegeaji unarudisha nyuma maisha. Simba anamuandaa mtoto wake kuwa mfalme wa nyika sisi tunaandaliwa kuwa chanzo cha mapato na unafuu wa waliotulea.

Hii haijakaa sawa.
Nini maoni yako.

Mtumishi Matunduizi.
 
Kwenye hizi jamii zetu ambazo social status inathaminiwa sana ni ngumu mkuu.

Mzazi anataka zile sifa atakazopata mtoto wake akifanikiwa.

Visa vya 'flani alisomeshwa kwa shida, sasa hivi anamsaidia mama yake' vinapendwa sana.

Ni tamaduni tuseme.
Inasikitisha sana wazazi wanawageuza watoto ndio retirement fund! Sasa mtoto ahudumie familia yake halafu akuhudumie na ww uliyekula bata miaka 40 bila kufikiria fainali uzeeni ipo kweli. Tunahitaji kubadirika sana
 
Kwenye hizi jamii zetu ambazo social status inathaminiwa sana ni ngumu mkuu.

Mzazi anataka zile sifa atakazopata mtoto wake akifanikiwa.

Visa vya 'flani alisomeshwa kwa shida, sasa hivi anamsaidia mama yake' vinapendwa sana.

Ni tamaduni tuseme.
Matatizo mengi yanayotusumbua ni ya kiutamaduni.
Mtoto kumsaidia mzazi ninwajibu wa asili. Ila mzazi kumuandaa mtoto kuna udhaifu. Ni haki ya mzazi kumsaidia mtoto alitmemleta duniani bila kujali atakusaidia au la. Anaweza kuwa msaada kwa watu wengine wenye shida kuliko wewe.

Tusizae watoto tukisukumwa na ubinafsi na kujipendelea. Hiki ndicho nimejifunza.
 
Umasikini ndio unaleta hayo mawazo, ndio maana watoto wa matajiri wao wanajiandaa kurithi, hawawazi kuhusu kusaidia wazazi wao;

Na pia ni chanzo cha umasikini kwa familia nyingi, mshahara wa mtumishi wa halmashauri hautoshi kutunza familia ya kijana na bado uje kutunza wazazi wale milo mitatu kwa siku
 
Umasikini ndio unaleta hayo mawazo, ndio maana watoto wa matajiri wao wanajiandaa kurithi, hawawazi kuhusu kusaidia wazazi wao;

Na pia ni chanzo cha umasikini kwa familia nyingi, mshahara wa mtumishi wa halmashauri hautoshi kutunza familia ya kijana na bado uje kutunza wazazi wale milo mitatu kwa siku
Nina rafiki yangu mmoja huwa anasema yeye ameshakubali maisha yamemshinda majukumu na ukepteni wa familia amemvalisha mtoto wake wa kike. Anapambana sana kuhakikisha huyo dogo aje awe majibu ya kufeli kwake kiuchumi.
Hii inamfanya mtoto anaanza kuwaza mawazo ya kizazi wakat8 bado yuko shule. Umasikini unashambulia kutoka angle zote.
 
Mpja kwa moja kwenye mada
Wazazi wengi wanakomaa kulipa ada kubwa na kujitoa muhanga kiuchumi ili watoto wao wasimame. Kusudi lililojificha nyuma ni ili mtoto wao akifanikiwa awasaidie kimaisha.

Wazazi wanavizia mahari za watoto wao wa kike. Wanapambana watoto wa kike waolewe na wenye uwezo ili na wao wanufaike na sadaka za mkwe.

Mzazi mmoja nimemuona hadi anafukuza mke wa mtoto wake akidai huyo dada anania ovu za kutaka kuchukua mali za mtoto wao.

Hii tabia kwa mtazamo wangu ni miongoni mwa chanzo cha umasikini.

Sisi watumishi tunaamini ni Jukumu la mzazi kuacha urithi kwa watoto na wajukuu wake na sio kuvizia urithi wa watoto wake.
Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.
Mithali 13:22


Wazazi tubadilike. Tuanze kupambana kutafuta mitaji ya watoto wetu sio kusubiri mahali za watoto.

Tupambane kutafutia watoto makazi bora sio kuvizia waje watupe makazi bora.

Huu utegeaji unarudisha nyuma maisha. Simba anamuandaa mtoto wake kuwa mfalme wa nyika sisi tunaandaliwa kuwa chanzo cha mapato na unafuu wa waliotulea.

Hii haijakaa sawa.
Nini maoni yako.

Mtumishi Matunduizi.
background ya kimasikini, na stanard ya kimasikini ya nchi. kwanza, hiyo kuandaa mtoto aje akusaidie ipo tu huko mbagala, watoto wa masaki na oysterbay hawaandaliwi kuja kuwasaidia wazazi, wanaandaliwa wawe viongozi, wawe wafanyabiashara n.k na mzazi anajua hadi anakufa hatahitaji sent yao. pia, kwa utamaduni wa kiafrika mzazi akizeeka unamlea, ulaya kuna nursing home, unampeleka akalelewe huko na wewe utapeleka tu pesa kugarimia, though wengi pesa yao binafsi waliosave ndio huwa wanaitumia nursing homes na wachache wanapelekwa na watoto wao. africa ukizeeka unalelewa na mtoto wako, ndio maana hata kuzaa watu wanaona kama ni lazima ulaya watu wengine wanaamua hatutazaa kwasababu hata wasipokuwa na mtoto uzeeni wataishi nursing homes, bongo usipokuwa na watoto ukapata shida ya ulemavu au uzee, imekula kwako.
 
background ya kimasikini, na stanard ya kimasikini ya nchi. kwanza, hiyo kuandaa mtoto aje akusaidie ipo tu huko mbagala, watoto wa masaki na oysterbay hawaandaliwi kuja kuwasaidia wazazi, wanaandaliwa wawe viongozi, wawe wafanyabiashara n.k na mzazi anajua hadi anakufa hatahitaji sent yao. pia, kwa utamaduni wa kiafrika mzazi akizeeka unamlea, ulaya kuna nursing home, unampeleka akalelewe huko na wewe utapeleka tu pesa kugarimia, though wengi pesa yao binafsi waliosave ndio huwa wanaitumia nursing homes na wachache wanapelekwa na watoto wao. africa ukizeeka unalelewa na mtoto wako, ndio maana hata kuzaa watu wanaona kama ni lazima ulaya watu wengine wanaamua hatutazaa kwasababu hata wasipokuwa na mtoto uzeeni wataishi nursing homes, bongo usipokuwa na watoto ukapata shida ya ulemavu au uzee, imekula kwako.
Ni kweli
 
Back
Top Bottom