Niskilizeni mimi, wachezaji hawa yanga waachwe/wabaki

Niskilizeni mimi, wachezaji hawa yanga waachwe/wabaki

Umesahau hata penalt tuliyopata ilitooka kwa musonda

Mimi naona kila MTU abaki na mtazamo wake tu
Mwisho tutaona yupi ataachwa
Kwahiyo inampa uhalali wa kumnyima nafasi ya wazi Mayele aliyekuwa peke yake na goli?
 
Anasahau Musonda aliwezesha timu kuvuka Makundi goli la TP Mazembe.
Anasahau goli alilowafunga Malumo Gallants kwao assist ya Mayele. Tungefikaje fainali?
CC: Nifah
Kwani nimesema Musonda hafai? Hiyo nimeiweka kama reference kwenye hoja yangu ya Mzize.
 
Mzinze ana mchango mkubwa kufika hatua ya Makundi CCL.
Ana mchango mkubwa kwenye FA Cup msimu uliopita na huu.
Ana mchango ligi kuu wa goals na assist. Kumbuka assist kwenye Derby ya kwanza ya 5-1.
Unapozungumzia point 6 na goli 7 dhidi ya Simba lazima umtaje Mzinze.
Mechi ya kwanza ya derby Pacome ndio aliibeba mechi yote, tusingezungumza goli 5 hapa bila yeye.

Mechi ya pili ni Aziz Ki, Mzize ana mchango ila sio kama hao wawili niliowataja.
 
Kwahiyo inampa uhalali wa kumnyima nafasi ya wazi Mayele aliyekuwa peke yake na goli?
Ujue
Mkuu Mimi naona unahukumu wachezaji kwa tukio moja moja

Mfano musonda kummyima nafasi mayele au hapo mzize kukosa goli dhidi ya mamelodi

Hapo hapo kuna mdau kasema muda aachwe ukadai asiachwe sababu kuna muda analikamata dimba .!

Ndiyo ujue sio kila game utapewa superb performance kama ambavyo muda juzi hakuwa kwenye ubora wake ndivyo kina musonda na mzize hawawezi kucheza vizuri kila match

Huyo mayele mwenyewe alikuwa anakosa sana magoli mepesi na kufunga magumu .

Mimi nimetolea mwamnyeto ajitafakari sababu ya makosa mfululizo .

Sasa ujue sikuelewi mkuu what do you mean?
 
Ujue
Mkuu Mimi naona unahukumu wachezaji kwa tukio moja moja

Mfano musonda kummyima nafasi mayele au hapo mzize kukosa goli dhidi ya mamelodi

Hapo hapo kuna mdau kasema muda aachwe ukadai asiachwe sababu kuna muda analikamata dimba .!

Ndiyo ujue sio kila game utapewa superb performance kama ambavyo muda juzi hakuwa kwenye ubora wake ndivyo kina musonda na mzize hawawezi kucheza vizuri kila match

Huyo mayele mwenyewe alikuwa anakosa sana magoli mepesi na kufunga magumu .

Mimi nimetolea mwamnyeto ajitafakari sababu ya makosa mfululizo .

Sasa ujue sikuelewi mkuu what do you mean?
Mkuu unajua maana ya mjadala? Hata wewe wachezaji uliosema hawafai waachwe mbona kuna jamaa wamekupinga? Kila mmoja ana mawazo yake na ndio maana ya mjadala.

Usingetaka mawazo mbadala ungekaa kimya, ila kwa kuwa umelileta hapa lazima tuchangie kwa maoni yetu na sivyo unavyoona au kutaka wewe.
 
Hata Mayele mwenyewe katunyima magoli mengi kwa ubinafsi wake! Musonda asiguswe huyo jamaa ana kismat sana angalia mechi zote ambazo amefunga hatujawahi kupoteza
Tena sana
Mayele alikuwa magoli mepesi ya tap in alikuwa anakosa sana ila anafunga magumu
Tena ule msimu alitakiwa amuache saido mbali sana ila ndiyo vile tena match sometime inakukataa kama muda juzi yeye
 
Hata Mayele mwenyewe katunyima magoli mengi kwa ubinafsi wake! Musonda asiguswe huyo jamaa ana kismat sana angalia mechi zote ambazo amefunga hatujawahi kupoteza
Mimi Musonda namkubali, na katika maoni yangu ya jumla nimesema abaki ila Mzize ndio aondoke.
 
Mkuu unajua maana ya mjadala? Hata wewe wachezaji uliosema hawafai waachwe mbona kuna jamaa wamekupinga? Kila mmoja ana mawazo yake na ndio maana ya mjadala.

Usingetaka mawazo mbadala ungekaa kimya, ila kwa kuwa umelileta hapa lazima tuchangie kwa maoni yetu na sivyo unavyoona au kutaka wewe.
Ndiyo na hakuna sehemu umetukanwa wala kubughudhiwa
Ila ni mjadala tu kuelezeana sasa kosa langu liko wapi?

Tena nimekumention tujadili

Kila MTU na mtazamo wake ila haina maana haipingiki ndiyo maana walionipinga sijakataa labda kuna kitu wanajua than Mimi hapa shida nini? Iwapo mtu akipinga hoja yako?

Hi ndiyo maana ya mjadala

Samahani sitakupinga
 
Mimi Musonda namkubali, na katika maoni yangu ya jumla nimesema abaki ila Mzize ndio aondoke.
Tatizo ni replacement yake, kumbuka wamepita washambuliaji wengi wazawa hakuna alieonyesha uwezo mfano Waziri Jr , Tariq Seif, Yusuf Athuman, Matteo Antony etc bado hakuna kitu afadhari kumvulia huyo dogo ata improve
 
Asante mwananchi kwa bandiko lako ya kuhusu maboresho ya timu, binafsi naona kwa hatua iliyofikia Yanga kwasasa inatakiwa isiwe na wachezaji wanaopishana sana viwango. Yanga msimu ujao wanataka kuprove watu kuwa walioonewa kuishia robo fainali ya klabu bingwa, wanatakiwa kushiriki AFL kama haitofutwa ( kuna tetesi kwamba wajumbe wamekataa CAFCC kufutwa ni bora ifutwe AFL) bado inabidi itete mashindano ya ndani, hivyo kutakuwa na mashindano mengi sana kushiriki hivyo kunahitajika uwiano uliokuwa sawa kati ya first eleven na wachezaji waliopo benchi. Kama wachezaji wanacheza timu kubwa ya Yanga lakini inafungwa na APR au Ihefu hawana maana.

Nkane, Faridi, Ngushi, Mauya, Sureboy, Metacha, Skudu, Mwamnyeto sijui ana shida ipi kwanza kujiamini kumepungua sana. Akipata mpira ni kubitua tu na akisema atoe pasi basi kachoma. Kwenye uwezo wa kukaba nako kapwaya kabisa kama sio kusababisha penati basi kashindwa ku win mpira. Nafasi ya Mwamnyeto inahitaji mtu.

Ma gap mengi kwa asilimia kubwa tunatakiwa tuyazibe kwa wachezaji wa ndani ukizingatia kuwa wachezaji wa nje ambao wanaostahili kupewa mkono wa baibai ni wachache sana binafsi naona ni Skudu na Lomalisa. Mzize ana tetewa ila ni moja ya wachezaji waliochangia kuichelewesha Yanga. Mechi dhidi ya Azam ilikuwa sio ya Yanga kupoteza ila kaipotezea Yanga. Mechi zote mbili dhidi ya Mamelodi Mzize kaikosesha Yanga nafasi ya nusu fainali hivyo kama ana bakishwa basi aje mtu wa kumpa changamoto hata akiwa usajili wa ndani maana Mzize sio wa kumtegemea kabisa.

Musonda mzee wa kazi huyu ukimpanga pembeni atakupa kinachostahili kwenye mechi ngumu yeyote. Anakaba na kufanya mashambulizi ni aina ya wachezaji wanaopendwa na Gamondi kama ilivyo kwa Max Nzengeli. Hivyo Musonda hastahili kuondoka.

Kazi kubwa inayofanywa na daktari bingwa wa upasuaji (Aucho) anatakiwa apate mtu wa kumsaidia kwasababu kuna kuumia na kadi na kuchoka kwa kutumika sana. Mkude alifanya kazi nzuri kwenye leg mbili za Mamelodi na ilikuwa ni sapraizi kwa wengi ila hili eneo linabidi liongezwe ingizo lingine kwavile sureboy kalishindwa hivyo imeshapunguza idadi ya viungo wenye ubora.

Yangu ni hayo
 
Kwahiyo inampa uhalali wa kumnyima nafasi ya wazi Mayele aliyekuwa peke yake na goli?
Hujacheza hata ndondo mkuu
Kwenye mpira kila kitu hakiwezi kwenda sawa
Kuna sehemu atapatia au atakosea
Kucheza nafasi ya striker hata kupata nafasi ya kushindwa kufunga ni ngumu
Musonda ni super striker
 
Back
Top Bottom