NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

Nmb kitengo cha mikopo hongereni saana kwa huduma zenu nzuri
 
Haya malalamiko tunajisumbua tu, sio kwamba hawayajui! Wanayajua sana na hapa wanatuchora tu tunavyopiga makelele. Complains zinawafikia kila siku na ni hizi hizi ila hawazifanyii kazi.

Wanatuinjoi tu hapa wahuni hawa!

CC NMB Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Yaaani inasikitisha sana kuona watu wakipata kaz wanakuwa na viburi, dharau, uvivu, kupenda rushwa na ngono wakati kabla haujapata hyo kaz unakuwa unalalama hooo, jaman ajira ngumu mara unaanza kuomba Mungu sana n.k. Lakin ukishapata unageuka Mungu mtu, tunaumia sana aisee.

Haya mambo sio kweny mabank tu bali imeshakuwa fashion kila idara ya kuhudumia watu. Mi nilitaka kufungua akaunti NMB tawi la Bukoba mjin ila ilibidi niache baada ya kwenda customer care kuuliza taratibu alafu mhudumu anajibu kwa kiburi na dharau ndo nikaenda kufungua CRDB
 
Hawa NMB bure kabisa mi nshalalamika nshatuma e mail saana!! Kipindi naomba mkopo niliupata lakini ilibidi nihonge!! Sidhani kama ntakopa tena NMB, na msipojiangalia TPB atachukua wateja wenu. NMB itabak benk ya kuchukulia mishahara tu.
Malalamiko yangu ni NMB Shinyanga branch. Hamna customer care, wana mapozi sana kuchukua statement tu unaweza ukakaa hata masaa 3, wafanyakaz wako busy kwenda kunywa supu, sometime teller mmoja yaani kero tupu.
Ila ukiwa na vibuku tano tano wanakusaidia kupotisha slip kwa nyuma!! Kwa nini nihonge ili niwekewe hela fasta. Kwani mkiweka matteler madirisha yote mtakufa?? Kwa nini muentertain biashara ya kujuana?? Nmeandika barua kwenye suggestion box ila hamna changes.
Nmb Manonga Branch ni kero!! Hapo bado Kero za ATM

yaani wa shy hapo manonga wanajiskia jamani
wana dharau,jeuri sijui wanajionaje hao watu hapo.

kwa kweli mtwara wanajitahidi sana
kwazo foleni tu hasa kipindi cha mshahara
 
nimesoma uzi wote,ponge na malalamiko watu wanayotoa lakn hamjibu kitu kwenye uzi wenu,hii ni dalili yq dharau pia, mpaka naona nikitoa malalamiko yangu ni kama nitakuwa najisumbua tu wala hakuna msaada
 
Nmb kitengo cha mikopo hongereni saana kwa huduma zenu nzuri

Mkuu HoPage ingekuwa vizuri ukataja branch nadhani ukigeneralize utawachanya watu maana kuna wachangiaji hapa wamelalamikia hicho hicho kitengo cha mikopo
 
Last edited by a moderator:
Bora yenu huko shinyanga,huku mwanza buzuruga plaza unaweza ukapiga mtu, kuna kijana mmoja anaringa utadhani bank yakwao anaongea nakuchat wakati kunalifoleni, wanatabia mbaya sana wakiina foleni ndogo namuda wakufunga umekaribia wanaondika wanamuacha mmoja ndio atuhudumie sujui lengo ni kupata malipo ya ziada au
 
nimesoma uzi wote,ponge na malalamiko watu wanayotoa lakn hamjibu kitu kwenye uzi wenu,hii ni dalili yq dharau pia,mpaka naona nikitoa malalamiko yangu ni kama nitakuwa najisumbua tu wala hakuna msaada
kama hawa tu wanachelewa kujibu malalamiko wategemea nini!
 
Kumbe na NMB ni wale wale. Sasa wanasubiri nini kuja kujibu hoja za watu?
 
Nilisajili Account yangu ikiwa na vielelezo vyote per BOT requirements

Wame block account yangu bila maelezo ya
kutosha. Nimepeleka details zangu upya, hii ni wiki ya pili hazijafanyiwa kazi.

Ukichukua pesa dirishani utabambikiwa noti za mia tano tano mpaka utakoma! Imagine nilipewa Tshs 500,000 katika note za 500!

NBC ipo ICU kweli!

Mi pia waliwahi kunipa nikaomba muhudumu ahesabu kwa mashine akagoma akanambia nihesabu mwenyewe akijua sitafanya hivyo nilipohesabu 10000 ikawa hamna
 
Atm zenu songea mjini nijanga mumezijenga hovyo.mtu anatoa pesa anaonekana na kila mtu

Idara ya mikopo rushwa imetawala bandikeni namba za simu kila tawi mle ndani ili mtu akiombwa rushwa awapigie namba ziweke ssehem wazi
 
Nmb mbona mnawasanifu wateja wenu? Mmefungua kauzi haka watu wakadhani mtawajibu kumbe mambo ni yaleyale! Badilikeni kwa kweli.
 
Hii ni hatua muhimu nawaponfeza.
1. Kuna watu hupiga simu wakijitambulisha kuwa ni wafanyakazi wa NMB lakini huulizia habari nyeti.
Changamoto ni kujua kama kweli ni wafanyakazi wa NMB.

Mara moja mwaka juzi niliibiwa kiasi fulani cha pesa kwa njia hii.
Naomba wafanyakazi wenu wasikae kituo kimoja zaidi ya miaka 5.

Wanazoea na kuanza uzembe. Hata rushwa kwenye mikopo inatokana na hili.

Pale Muleba kuna wafanyakazi wako pale miaka zaidi ya mitano. Wana lugha mbaya na wanakwepa wateja.

Mwisho NMB inajihusishaje na international trade? Omugishagwe@yahoo.
 
Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.

Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe “Siri”)
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom

Vipi zile fedha zetu mlizotutoza kwa njia isiyohalali ya kukatwa shs 1000 wakati mtumishi/rafiki akiweka fedha kwenye account miaka ya nyuma, tena nikiwa nimekopa kutoka benki, lakini wanataka mimi mwenyewe nipeleke fedha beki. Je zile fedha mtaturudishia lini?
 
Kesho naenda kufunga akaunti yangu ya STANBIC hawafai pesambili!!
 
NmB Hai pale kuna jamaa mmoja anaitwa Dennis, kwanza mcheShi na kila mara mtani yani hadi unajiskia mwanafamilia. NmB muwaangalie hawa watu
 
Back
Top Bottom