TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

Watu wanaandika kashfa kwa sababu tu alipendwa na Magufuli. Kusema ukweli mimi nilikuwa simjui na wala utendaji wake siujui lakini kwa kutumia hisia nadhani alikuwa mchapakazi na asiyependa kujikweza. Kwanini: Sijawahi kumsikia kwenye skendo au kujiona anajiweka mbele mbele kwenye media au mitandao au kuonyesha kwa namna yoyote kuwa ni msomi. Uzoefu unanifundisha kuwa watu wa aina hii huwa wachapakazi na wazalendo. Sijui huenda nimekosea lakini hisia zangu zinanituma hivyo.
Mkuu hujakosea, ulivyomuelezea ni kama alivyo.
Mfugale alikuwa mtu mwenye madaraka makubwa sana kutokana na kuendesha TANROADS, Shirika la umma lenye kutumia pesa nyingi za serikali kuliko hata wizara nyingi.

Namfahamu personally Mfugale , hakuwa mjivuni wala mtu kwa kujikweza au tamaa.
Na alikuwa makini sana kama mhandisi.
Pengine ndio maana alikaa cheo alivyokuwa nacho kwa muda mrefu.
RIP Eng Patrick Mfugale.
 
tulio baki hai tunajambo la kujifunza haswa viongozi/watendaji.

jueni kuwa cheo/vyeo ni dhamana, kamwe huwezi kuzikwa na cheo chako, uwe waziri, uwe mbunge, uwe diwani, uwe Jaji, auwe Hakimu, uwe mkurugenzi, uwe Dasi, uwe RASI, n.k n.k.

Jambo la msingi zingatieni kutenda Haki, acheni kuonea watu, fanyeni kazi kwa maendeleo ya wananchi.

R.I.P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*"Namjua Engineer Mfugale ni mzalendo wa hali ya juu. Nakumbuka mwaka 2008 Engineer Mfugale na Engineer Mvungi walitishiwa kufukuzwa kazi kwa kusimamia ukweli na professionalism na Wakatupwa Wizarani bila kupewa kazi yoyote ya kufanya. Jinsi ninavyowsjua Wahehe kwa kupenda kujiua nilifikiri Engineer Mfugale angejiua lakini hakujiua, alivumilia.

Mwenzake, Engineer Mvungi, akajipiga risasi na kupoteza maisha!. Leo Engineer Mvungi ni marehemu kwa kupigania ukweli na hiyo ndio saa zingine gharama ya kupigania ukweli. Nikamteua Engineer Mfugale kuwa Chief Executive Officer wa Tanroads. Amejenga madaraja mengi sana nchini"*_

Hayati Dr. JPM, 28.9.2018

R.I.P Wazalendo.
 
Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale amefariki dunia leo Jumanne Juni 29, 2021 jijini Dodoma.

Katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Joseph Malongo amesema Mfugale atakayekumbukwa kwa kusimamia ujenzi wa barabara na madaraja zaidi ya 1000 nchini amefariki dunia leo saa 5 asubuhi katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Amebainisha kuwa taratibu nyingine za msiba huo zitatolewa baadaye.

Taarifa zilieleza kuwa Mfugale akiwa katika moja ya kikao kazi alijisikia vibaya na kukimbizwa hospitalini ambako akiwa njiani hali yake ilizidi kuwa mbaya.

Awali Waziri wa Ujenzi, Dk Leonard Chamuliho na naibu waziri wa wizara hiyo, Mwita Waitara alieleza kuwa hawana taarifa za kifo cha Mfugale
 
Thanks, but it was a typo.
Grateful that at least there is another person apart from me who is proficient in the Queen's language in jf.
Cheers.
... inaeleweka Kiongozi. Nilitaka kucholaza tu. Typos ni kawaida sana; kuwa na amani.
 
Ila wafanyakaz wa tanrod Chini yake wanaukwasi mkubw mnoo sizani hata dereva wa tanrod tu c ajabu umkute nae anamiliki gorofa yaani
 
Patrick Aron Nipilima Mfugale mhandisi tajwa nchini Tanzania na alikuwa mtendaji mkuu wa Mamlaka ya barabara nchini Tanzania TANROADS.

Injinia Patrick A. N. Mfugale RIP

=====

Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Injinia Mfugale amefariki Jijini Dodoma.

Mfugale jana aliondoka na ndege akiwa na Katibu Mkuu ujenzi kuelekea Dodoma kwa safari ya Kikazi

Amezidiwa leo saa tano asubuhi na kukimbizwa Hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma, Tanzania ambapo ndipo Mauti umemfika muda mchache baada ya kufikishwa.

Tutaendekea kuwapasha kinachoendelea.

Apumzike kwa Aman

Wasifu:
Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Consalata Fathers Primary School mjini Iringa
-1975 Alimaliza elimu yake ya shule ya upili katika shule ya upili ya Moshi.
-1977-Mfugale aliajiriwa katika wizara ya ujenzi
-1983 alijipatia shahada yake ya kwanza katika chuo kikuu cha Rocky nchini India
-1991 Mfugale alisajiliwa kama muhandisi mtaalam.
-1992- Aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa barabara za mikoa.
-1994-1995-Alipokea shahada yake ya pili katika chuo kikuu cha Loughborough, nchini Uingereza
-2003-Alipokea tuzo ya Distinguished Engineering Accomplishment.
-Aliteuliwa kuwa muhandisi mkuu wa madaraja nchini Tanzania wakati huohuo na akiwa masomoni nchini Uingereza mwaka 1995 alitafiti na kutengeneza mfumo wa madaraja nchini.
-Alitengeza mfumo wa usimamizi wa madaraja kwa jina Tanzania Bridge Management System
-2014- Alisajiliwa kuwa muhandisi mshauri na kuwa mwanachama wa chama cha wahandisi Tanzania.
-Ametumia muda wake mwingi kama mtaalamu wa madaraja .
Alibuni daraja la Malagarasi lenye mita 178 kwa shilingi za Tanzania milioni 300.
-Baadhi ya madaraja aliyoweza kusimamia yakakamilika kujengwa ni:
  • Daraja la Mkapa Rufiji
  • Daraja la Umoja linalounganisha Tanzania na Mozambique huko Ruvuma.
  • Daraja la Rusumo
  • Daraja la Kikwete huko Malagarasi.
  • Daraja la Nyerere huko Kigamboni
- Mfugale akiwa mtendaji mkuu wa Tanroads amesaidia ujenzi wa madaraja 1400 nchini Tanzania.
Amebuni na kusimamia barabara za kitaifa zenye urefu wa takriban kilomita 36,258.
  • Alikuwa Mwenyekiti wa kikosi cha ujenzi wa Reli ya kisasa SGR inayoendelea kujengwa.
  • Alikuwa mjumbe wa timu ya majadiliano ya miradi mikubwa ya umeme.
-2018 Alituzwa tuzo ya uhandisi ya Engineering Execellency

Picha: Daraja la Kikwete mto Malagarasi Daraja la Kikwete lililopo Mto Malagarasi
Pamoja na mapungufu yake ila hili jamaa lilikuwa na akili mingi sana.
 
Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale amefariki dunia leo Jumanne Juni 29, 2021 jijini Dodoma.

Katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Joseph Malongo amesema Mfugale atakayekumbukwa kwa kusimamia ujenzi wa barabara na madaraja zaidi ya 1000 nchini amefariki dunia leo saa 5 asubuhi katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Amebainisha kuwa taratibu nyingine za msiba huo zitatolewa baadaye.

Taarifa zilieleza kuwa Mfugale akiwa katika moja ya kikao kazi alijisikia vibaya na kukimbizwa hospitalini ambako akiwa njiani hali yake ilizidi kuwa mbaya.

Awali Waziri wa Ujenzi, Dk Leonard Chamuliho na naibu waziri wa wizara hiyo, Mwita Waitara alieleza kuwa hawana taarifa za kifo cha Mfugale
Mbona habari haijawekwa Tag ya Tanzia kama toka asubuhi imetangazwa rasmi?
 
Yaani wewe usiku huu ndio umejua? Halafu unakimbilia hapa ku-post bila kusoma post za watu wengine! Kwa taarifa yako, hii siyo habari ngeni hapa JF.
Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale amefariki dunia leo Jumanne Juni 29, 2021 jijini Dodoma.

Katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Joseph Malongo amesema Mfugale atakayekumbukwa kwa kusimamia ujenzi wa barabara na madaraja zaidi ya 1000 nchini amefariki dunia leo saa 5 asubuhi katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Amebainisha kuwa taratibu nyingine za msiba huo zitatolewa baadaye.

Taarifa zilieleza kuwa Mfugale akiwa katika moja ya kikao kazi alijisikia vibaya na kukimbizwa hospitalini ambako akiwa njiani hali yake ilizidi kuwa mbaya.

Awali Waziri wa Ujenzi, Dk Leonard Chamuliho na naibu waziri wa wizara hiyo, Mwita Waitara alieleza kuwa hawana taarifa za kifo cha Mfugale
 
Jamaa alikuwacna kisu kikali. Sijui kama ameacha kabinti nikasaidie kulinda mali alizoacha.
 
Back
Top Bottom