Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Hatuna cha kupoteza eti kwa kumzuia RC Makonda kwenda Marekani. Kwanza wajiulize tangu Rais wetu John Pombe Magufuli aingie madarakani alishawahi kwenda ubarozi wa Marekani nchini kuomba Viza ya kuingia Marekani? Ukweli ni kwamba hajawahi kwahiyo RC Makonda aende Marekani kutafuta nini ambacho bosi wake haoni haja?
 
Nimeshangazwa sana kuona Leo hii RC Makonda kashindwa kujitokeza kujibu tuhuma nzito zilizotolewa na Marekani dhidi yake.
Kuhusu kuzuiwa kwenda US hata mimi namuunga mkono kupotezea kwani sio lazima kwenda huko maana mie binafsi huu ni mwaka wa NNE sijakanyaga US na sioni tatizo maisha yana songa, lakini tuhuma nzito kama kukatisha maisha ya watu hasa wapinzani kisiasa sio za kukaa kimya.
Jee hajui kuwa sasa hivi wenye ndugu zao walio potea kwa hisia kuwa sababu ni za kisiasa wamesha muweka kuwa yeye ndio kawateketeza? Maana US hawana sababu ya kumzushia Makonda tuhuma nzito kama hizo.
Hajui kuwa tuhuma hizo nzito zinamuweka mashakani maana hakuna atakaye jitokeza kumsemea zaidi yake mwenyewe na watu tayari wamemuweka kwenye kundi la wauaji?
Ajitokeze akane au atamke kuwa alikuwa naye anatumwa tuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani wanamzuia mtu mwenye maslahi yake nchini mwao. Pesa za jiwe za manunuzi mabovu makonda ndio alikuwa anazisimamia huko.
 
Ukiunganisha dots ina-make sense!Wakati Lissu anashambuliwa Makonda alionekana Dodoma na siku hiyo kulikuwa na shughuli ikulu ambapo ilishangaza wengi Makonda kutokuwepo!
Kuwaondoa walinzi wa Suma JKT pale getini kupisha wauaji,wadau wengi walisema lazima alihusika mtu mwenye nguvu na madaraka!
Picha inaanza kukamilika!
 
Ukishaelewa TAASISI YA URAIS basi utaelewa maana ya kutuma uwakilishi. Kabudi & Co wanapopishana kwenye korido pale white house ni kwa ajili ya Rais.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ana subiri Mh. Spika jumatatu awapange wabunge wa Ccm kusema Zitto sio mzalendo ndie kawaambia Wamarekani wamseme vibaya mtoto wa baba..
Na huu ni mwanzo tuu wa picha. Soon watawataja na vinara wakuu. Kabudi atoe macho kama kabanwa na mlango awape karipio kama alivyo zowea asikie moto wake..
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kesho aende kanisani akalie atubu dhambi zake. Jumatatu ajiuzulu. Dunia inaweza kumsamehe.
RIP Akwilina.
 
Kiutaratibu ofisi za ubalozi ni nchi. Kwa hiyo Makonda marufuku kuingia ofisi za ubalozi wa usa nchini? Kama ni kweli. Hii ni dharau kubwa. Mkuu wa mkoa asiyekuwa huru aliye wekewa mipaka.

Haikubaliki kabisa.

Kwani tangia lini Tanzania imewahi kuwa juu ya Marekani? Hivi kama wameshakuzuia kwenda nchini Kwao ' Logically ' tu wanaweza Kukuruhusu kwenda katika Ubalozi wao ambao una Hadhi na Thamani Kubwa pengine kuliko hata Ikulu yako? Hivi kulijua hili Jambo jepesi kulihitaji Mtu uwe na Certificate au Diploma au Degree au Masters au Doctorate kweli?
 
Tabia kuu ya mpumbavu ni kukosa hoja!
 
Ruhusu kidogo kufikilia kwa akiliyako.makabrasha ya darasani achana nayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwezenu daktari wamkewe yuko dar ili mbegu ipandikizwe kwenye yai lamkewe lazima awepo sasa hii nitabu pia
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…