Pambana nanhili kwanza; Marekani aliingilia kupigania haki za raia wa nchi hizi
1.) IRAQ
2.) LIBYA
3.) VENEZUELA
unajua nini hizi nchi wanacho in common?, unajua nini kimewatokea? Je, na sisi wanapigania haki zetu sasa? Nini mnataka kitutokee na sisi?
Huko wanatuhusu nini?
Tuanzie kwetu sisi tusiopendana kwa sababu tu ya madaraka na vyama.
Mkiambiwa Rais awe huru bila kujali vyama mnakataa kwa sababu mnataka kuteuliwa na uteuzi uwe wa chama kimoja.
Hivi Mtu wa Chadema au Cuf hawezi kuwa Balozi?
Je, Mabeberu wanateuliwa kwenda kwa mabeberu kufanya nini kama hawana jema la kujifunza kwao?
Kwenye Koran kuna Sura ya Wanafiki.
Hizo nchi ulizozitaja zina matatizo makubwa sana kutokana na kuwa na Viongozi wapenda madaraka.
Wanatumia ujinga wa watu wengi kubakia madarakani.
Hivi Gadafi kule Libya enzi zake alikua na sababu gani ya kuanza kutoa vitisho kwa Israel kuwa Ataiondoa kwenye Ramani ya Dunia?
Bila shaka alikua anajua kuwa Libya ni nchi ya Kiislam hivyo kuwahadaa kuwa unauwezo wa kuiangamiza Israel utapata uungwaji mkono mkubwa toka kwa wananchi ili hali akijua kuwa Marafiki wa Israel wakubwa ni Marekani!!
Kwa nini Gadafi asingeendelea kuijenga nchi yake iwe bora kuliko hizo za magharibi bila kuitishia Marekani na Israel.
Kwa nini Gadafi awe anatuhumiwa kuunga mkono makundi ya Kigaidi dhidi ya Nchi za Magharibi?
Unategemea nini kama utaanza kujiingiza kwenye vita baridi na moto kwa mataifa ya mabeberu?
Hivi kuna mtu aliyekua amewanyanganya Mali nyingi wazungu na wahindi kama Nyerere? Ni kwa nini hakuzuiwa kwenda Marekani au kokote duniani!! Ni kwa sababu hakuwa anatoa wito wa kuwashambulia Wazungu na wa Israel na Mali zao popote duniani kama hao uliowataja.
Iraki alijipambanua kuwa anajiandaa kuiangamiza Israel. Unategemea nini? Irani nao wanahangaika kutafuta maendeleo yao lakini kwa kujinasibu kuwa wataiangamiza Israel huku wakijua kuwa ni Marekani haiwezi kukaa kimya kuona Israel ikiangamizwa.
Kwa nini Kuweit ,Qatar, Falme za Kiarabu na Saudi Arabia hawavamiwi kama LENGO la mabeberu ni kuvamia tuu! Kwani Maisha ya Wairani ni mazuri kukiko ya watu wa Falme za Kiarabu.
Mbona Kuna waarabu wanaishi maisha kama Peponi bila kutoa vitisho dhidi ya Israel au nchi za magharibi?
Huku kila siku unasikia hao mashoga ,mabeberu ,wanyonyaji, wasitupangie, tunajitawala lakini asilimia kubwa ya ulinzi na mbinu za kujilinda tunajifunza kwao.
Tunaomba misaada ya elimu na madawa n.k.
Kwenye Koran kuna sura ya wanafiki.
Sent using
Jamii Forums mobile app