Pendekeza tozo nyingine Serikali ya Samia iichukue

Pendekeza tozo nyingine Serikali ya Samia iichukue

hakuna cha bure katika ulkmwengu huu, lazima tulipe tozo kwa maendeleo yetu.
unadhani maendeleo yataletwa bila tozo?! thubutu!!! hata hao wanao pinga tozo wanalifahamu hilo, ila nia yao ni kuona Serikali inashindwa kuleta maendeleo ya wananchi.

Watu hawana tatizo na kulipa kodi, tatizo lingine ni kuwa hizo kodi zinafanya nini ?

Yaani ukiacha vitu alivyofanya mwendazake, hawa wendawazimu wamefanya nini kwa matrilioni ya mikopo na hizo Tozo ?
 
View attachment 2327988

Humu ndani tunaye Ndugu Waziri Mwigulu Nchemba, tutumie fursa ya uwepo wake kumkumbusha tozo zingine ambazo amezisahau. Ni kama akiziota usiku tu kesho anakuja nazo.

Mimi naanza na tozo ya ugali, ugali utoe kodi. Mwaka huu kutokana na kupanda kwa bei za nafaka watu wengi sana watakula ugali. Piga idadi ya tonge mara idadi ya tonge kwa siku, kwa wiki na kwa mwezi. Tonge likiwekwa kishimo liwe na tozo kubwa kidogo. Hapo serikali itapata bilioni 900. Tozo nyingine ya haraka haraka ni Simba na Yanga, kila tukifanya utani wa jadi kuwe na tozo.
Kuna kiongozi mmoja 002 alipoambiwa kuwa Kuna pesa chache mtaani hivyo hakuna mzunguko.

Akashauri ,nendeni mkawaagize Benki kuu wakachapiche pesa ziwe nyingi!!!

Tangu lini green guard akajua Uchumi!!!
 
kanyegrin.png

Hafai huyo Waziri wa Asali.
 
Wahaya wote wapewe TIN number na machine ya EFD....waaanze kutupa risiti..
Barabara zote zianze kulipiwa kodi...watu watulie makwao..
Ndoa pia zilipiwe kodi, Kila mke alipiwe kodi..
Watoto pia tusiwasahau
 
Tozo maalum kwa great thinkers wote, vilaza tukaushiwe kwanzaa..
 
Tatizo linapokuja ni pale ambapo utasikia pesa zimetumika vibaya au zimeibwa sijui bilioni ngapi huko hiyo ndo hukatisha zaidi watu tamaa kabisa, ingekuwa leo hii tupo kwenye hatua nzuri ya kiuchumi naamini hizi tozo watu wasingeongea sana, ubaya unakuja unakamuliwa tozo ila output inaonekana kwa darubini...UFISADI.
 
Tatizo linapokuja ni pale ambapo utasikia pesa zimetumika vibaya au zimeibwa sijui bilioni ngapi huko hiyo ndo hukatisha zaidi watu tamaa kabisa, ingekuwa leo hii tupo kwenye hatua nzuri ya kiuchumi naamini hizi tozo watu wasingeongea sana, ubaya unakuja unakamuliwa tozo ila output inaonekana kwa darubini...UFISADI.
Hizi ni hisia tuu ila in most cases pesa inatumika vizuri..

Hata hivyo Ili kukabiliana na hilo kwani hikuona maelfu ya ajira za Takukuru na Wakaguzi wa ndani Ili kusimamia value for money?
 
Serikali ianzishe TOZO za:-
(a) Pumzi. Kila aliye hai alipe tozo hii.
(b) Usingizi. Kila alaye alipe tozo hii
(c) Ngono. Kila aliyebalehe alipe tozo hii
(d) Kuona. Kila mwenye macho alipe tozo hii.
(e) Kusikia. Kila mwenye masikio yanayofanya kazi alipe tozo hii.
(f) Shibe. Kila anayekula alipe tozo hii.

Stakayeshindwa kulipa tozo hizi ahamie Burundi.
Hii tozo ya kuona unamaanisha vile wanaume tunaangalia makalio sio ?
Hii Ni nzuri tukigeuka nyuma kuangalia makalio tutoe tozo
 
Hizi ni hisia tuu ila in most cases pesa inatumika vizuri..

Hata hivyo Ili kukabiliana na hilo kwani hikuona maelfu ya ajira za Takukuru na Wakaguzi wa ndani Ili kusimamia value for money?
Ndiyo hivyo mjue kabisa kuwa walipa Kodi tunakata tamaa sometimes kwa kuona pesa za serikali zinatumiwa hovyo...value for money ipi hiyo?, ina maana siku zote hizo serikali haikuwa na hao watu, kwa kweli Kodi na tozo laiti Kama zingetumika vizuri tungekuwa na taifa zuri sana...Kama huyu raisi akifanikiwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji tutafika mbali ila Kama ni porojo zinazoongelewa hapa basi muda utakuwa ni mwalimu mzuri, napenda zaidi kutoa muda.
 
Tozo ya kuingia hospital, iwe umeleta mgonjwa, kuona mgonjwa au unaumwa. Ni kama ilivyokuwa unaingia stendi ya ubungo kipindi kile.

Hapa serikali itakusanya pesa nyingi tu maana kila siku wagonjwa ni wengi.

Tozo nyingine ya kuingia benki, ukiingia tu benki au kwa wakala basi wawepo mawakala wa kukusanya tozo. Hapa napo serikali itakuwa imelamba dume.
 
Ndiyo hivyo mjue kabisa kuwa walipa Kodi tunakata tamaa sometimes kwa kuona pesa za serikali zinatumiwa hovyo...value for money ipi hiyo?, ina maana siku zote hizo serikali haikuwa na hao watu, kwa kweli Kodi na tozo laiti Kama zingetumika vizuri tungekuwa na taifa zuri sana...Kama huyu raisi akifanikiwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji tutafika mbali ila Kama ni porojo zinazoongelewa hapa basi muda utakuwa ni mwalimu mzuri, napenda zaidi kutoa muda.

Hawezi kufanikiwa, stop that optimism . She don’t have that cognitive capacity. Msimbebeshe mama mzigo mzito hivyo.
 
Back
Top Bottom