Pendekeza tozo nyingine Serikali ya Samia iichukue

Pendekeza tozo nyingine Serikali ya Samia iichukue

Tozo ya kuingia hospital, iwe umeleta mgonjwa, kuona mgonjwa au unaumwa. Ni kama ilivyokuwa unaingia stendi ya ubungo kipindi kile.

Hapa serikali itakusanya pesa nyingi tu maana kila siku wagonjwa ni wengi.
😂😂😂😂 Hii tozo ya wagonjwa nimeielewa sana, waziri aichukue hii nchi itapiga pesa na tutakua dona kantri
 
Mfumo wowote ule wa kukusanya kodi unaowekwa na serikali unapaswa kuzingatia vigezo muhimu vya kiuchumi ambavyo vimeainishwa.

A good tax system should meet five basic conditions:
1. Fairness
2. Adequacy
3. Simplicity
4.Transparency 5.Administrative ease

Waziri Mwigulu katika hoja zake, naona kwa makusudi anakwepa vigezo vya 'haki" na kile cha "uwazi" na kujikita zaidi kwenye vigezo vitatu vilivyobakia. Akiwa ni mbobezi wa fani ya uchumi ni lazima aviweke katika uwiano unaokubalika vigezo vyote vitano.

Hawezi kujificha katika urahisi wa kukusanya, utoshelezaji wa mapato yanayohitajika na mambo ya utawala na kuacha kusikiliza vilio na machungu ya watu kutokana na kodi alizozibuni.
 
Alisema Professa Assad... hii nchi kunaviongozi weeengi sana hawana uwezo kabisa wakazi walizopewa!!!! Mwigulu ni moja yamfano wao ndomana tukasema mawaziri waajiriwe wasivutwe kiuchama tuu ikosiku tutaletewa wendawazimu (kamabado).
Walitakaga tozo ya visima vyamajo hawa wajinga:::mtu ajichimbie kakisima nyumbani kwake ww serikali uloshindwa mpelekea maji safi na salama unataka kumpelekea eti tozo!! Stupid nonsense
 
Kweli watz wengi ni vichwa matikit mwenye nchi hii ni Nan mwigulu au uyo mama yenu ujinga afanye yeye lawama atupiwe mwigulu kweli ebu tujaribu kutumia kidogo hata ubongo wetu acheni kufanya uyo bibi hausiki ye ndo mkuu wa serikali
Mwenyewe nashangaa sana wa kutupiwa lawama ni huyo bibi kizee kilichokosa huruma na aibu nchi kimeivuruga vuruga sijui kimeumbwaje kipo km kopo hakijali Wala kushtuka, haramia la kizanzibari pambafu kabisa
 
Tozo ya kusoma story za " Kula tunda kimasihara" naona Kuna billions of money Mwigulu atamake!
 
Humu ndani tunaye Ndugu Waziri @Mwigulu Nchemba, tutumie fursa ya uwepo wake kumkumbusha tozo zingine ambazo amezisahau. Ni kama akiziota usiku tu kesho anakuja nazo.
Namshauri aweke kadi ya pumzi kabisa ili atumalize kabisa hadi Burundi tushindwe kwenda
 
View attachment 2327988

Humu ndani tunaye Ndugu Waziri Mwigulu Nchemba, tutumie fursa ya uwepo wake kumkumbusha tozo zingine ambazo amezisahau. Ni kama akiziota usiku tu kesho anakuja nazo.

Mimi naanza na tozo ya ugali, ugali utoe kodi. Mwaka huu kutokana na kupanda kwa bei za nafaka watu wengi sana watakula ugali. Piga idadi ya tonge mara idadi ya tonge kwa siku, kwa wiki na kwa mwezi. Tonge likiwekwa kishimo liwe na tozo kubwa kidogo. Hapo serikali itapata bilioni 900. Tozo nyingine ya haraka haraka ni Simba na Yanga, kila tukifanya utani wa jadi kuwe na tozo.
Ndugu mara ingine unapofungua thread, reason yourself. JF inatambua capacity yako, unapokuja ba junk kama hii unakuwa kwenye level ya Jumalokole.
 
Katika waziri wa fedha wa hovyo kuwahi kutokea ni huyu, Mwigulu sijawahi kumwelewa Kila wizara anazopitia, Sijui Samia anamenelea nini, Shime Shime maamuzi yetu na Hasira yetu tuihifadhi tukaitumie kwenye sanduku la Kura 2025. Tuitoe lichama hili Madarakani akili iwakae sawa.
Mkuu maamuzi tunayo tayari, binafsi nilimpenda sana mama SSH lakini kwa sasa sio kabisa!
 
Kinachouma zaidi mabilioni wanayokusanya kwa tozo yanaishia matumboni mwao walionacho. Kuna siku tutagawana mbao.
 
Tozo za nini wakati raslimali tele zimejaa hazitumiki kuendesha nchi.
Tunaambiwa pia Royal Tour imechangia ongezeko kubwa sana la watalii.
Sasa kwa nini wanatuvizia tena kila tukitoa hela zetu benki wanazifyeka?!
 
View attachment 2327988

Humu ndani tunaye Ndugu Waziri Mwigulu Nchemba, tutumie fursa ya uwepo wake kumkumbusha tozo zingine ambazo amezisahau. Ni kama akiziota usiku tu kesho anakuja nazo.

Mimi naanza na tozo ya ugali, ugali utoe kodi. Mwaka huu kutokana na kupanda kwa bei za nafaka watu wengi sana watakula ugali. Piga idadi ya tonge mara idadi ya tonge kwa siku, kwa wiki na kwa mwezi. Tonge likiwekwa kishimo liwe na tozo kubwa kidogo. Hapo serikali itapata bilioni 900. Tozo nyingine ya haraka haraka ni Simba na Yanga, kila tukifanya utani wa jadi kuwe na tozo.
1. Tozo ya kodi ya visima irudishwe, serikali inakosa mabilioni kwa kuondolewa kodi hii.
2.Serikali ianzishe 'tozo ya maji ya mvua' ambayo iwe inakua calculated kila mwaka kwa kupima mm³ za kiasi cha mvua ambayo mkoa umepata kila mwaka, na ilipwe na kila mwananchi kutokana na kiasi cha mvua cha mkoa aliopo.
3.Serikali ianzishe tozo ya maji ya umwagiliaji kwa wakulima wote kwa kukisia kiasi cha maji ambayo yanatumika kukuza mazao yao kwenye mashamba yao.
4.Serikali ianzishe tozo ya maji ya mifugo kwa wafugaji wote kwa kukadiria kiasi cha maji ambacho mifugo ya mkulima inakunywa kwa mwaka.
 
Mimi wakati mwingine naona bora nitoe rushwa afaidike mtanzania mwenzangu kuliko kulipa faini wakafaidike wa kwenye kiyoyozi
 
hakuna cha bure katika ulkmwengu huu, lazima tulipe tozo kwa maendeleo yetu.
unadhani maendeleo yataletwa bila tozo?! thubutu!!! hata hao wanao pinga tozo wanalifahamu hilo, ila nia yao ni kuona Serikali inashindwa kuleta maendeleo ya wananchi.
Maneno yako sio kweli. Dubai ni mfano mmoja mzuri. Hawana Mali ghafi yoyote, hawana hata mafuta, hawana utalii, hawana chochote zaidi ya viongozi bora. Miaka 50 iliyopita ilkuwa ni jangwa tupu la vumbi na mawe. Hawakuwa na tozo wala kodi ya aina yoyote kwa miaka 50 na zaidi. Leo itazame hatua iliyopiga ndani ya 50yrs.

Nchi inahitaji kuwa na viongozi bora kwanza ili iwe na maendeleo. Nchi ikiwa na viongozi hovyo ni sawa na ndoo iliyo na matobo mengi yenye ukubwa tofauti. Hata ukijaza maji vipi hiyo ndoo haitojaa. Viongozi wakiwa hovyo tozo na mikodi mikubwa inakuwa mzigo tu kwa wananchi kwani taifa halitanufaika chochote bali viongozi ni wanufaika na hizo tozo. Kwa hiyo kabla ya kufikiria tozo kwanza tufikirie uongozi.
 
Tozo za nini wakati raslimali tele zimejaa hazitumiki kuendesha nchi.
Kweli kabisa. Nchi hii tuna Almasi, Dhahabu, madini aina zote, Makaa ya mawe, Copper, Uranium, na mengine chungu nzima. Tumezungukwa na Maziwa makubwa ya Africa, Tuna Mito ya kutosha, ardhi yenye rutuba kubwa, vivutio vya utalii chungu nzima na vyenye kuongoza ulimweguni. Tuna Bandari zaidi ya 4.

Leo kila Mtanzania alitakiwa aishi katika nchi yake kwa raha na alitakiwa alipwe na Serikali kila mwezi kama benefits za mapato ya Mali ghafi zetu. Sisi sio watu wakukamuliwa na kulipishwa mikodi na mitozo. Serikali iwajibike kufanya kazi yake na kuhudumia wananchi. Sio yenyewe itake wananchi waihudumiye Seriali. Mpaka lini????

Ni nani anayenufaika na hizo tozo na kodi??? Kila kitu tunakopa, sasa tozo na kodi zinafanya kazi gani??? Hatuna uongozi bora huo ndiyo ukweli wenyewe. Tusidanganyane kabisa. Tokea uhuru hadi Leo ni miaka 60 na zaidi. Hivi tunaweza kujivunia kuwa tumeendelea??? Tutazame nchi kama Singapore, hawana chochote zaidi ya Bandari. Leo wako wapi?? Miaka 50 iliyopita sisi tulikuwa na uchumi mzuri kushinda wao, leo tazama wao wako wapi na sisi tuko wapi?? Tofauti ni sawa na Mbingu na Ardhi.
 
Back
Top Bottom