PICHA: Naombeni kujua huu ni ugonjwa gani unaotutesa hivi mimi na familia yangu

Asante mkuu nalifanyia kazi kesho
 
Hio itakua fangasi au bacteria infections,
Sikiliza wadau huko juu kwa uzoefu..

Nimepanda Uzi mpk hapo Wamechangia watu wanajielewa, hakuna Ma utani na lugha chafu.
 
Nyoosha maelekezo kaka shida ni nipone
Hahaha Mkuu Pole bana ,tatizo ni dogo Wala usipanick.

Tatizo lako Hilo dogo linaitwa SCABIES .

Huwapata zaidi watu walio kwenye eneo lenye uhaba wa Maji , na msongamano wa watu wengi na usafi duni kwa wanadamu na mazingira Kwa ujumla.

Hivo matibabu yake kwanza ni lazima yaanzie kwenye vichocheo vya tatizo Hilo pamoja matibabu husika ya tatizo .


Nunua Dawa zifuatazo.

1//Tetmosol Soap ( SABUNI ya Tetmosol) utakalokua Unatumia Kuoga, hivo Kila mwanafamilia awe nasabuni yake . Ukikoswa Haina shida.


2//Nunua dawa inaitwa Benzyl Benzoate Emulsion 10% BBE , ni Chupa yenye dawa asili ya kimiminika,, kabla ya kuitumia, KILA MMOJA AOGE KWA MAJI VUGUVUGU na ATUMIE SABUNI YA TETMOSOL KAMA UMEIPATA, , Kisha tumia Taulo safi ,ujifute maji mwili wote.

Baada ya hapo, PAKAA DAWA MWILI MZIMA , kuanzia miguuni Hadi Shingoni na kichwan nyuma ya masikio ,,ISIPOKUA USONI, USIPAKE DAWA HIYO USONI AU MDOMONI, AU UKENI AU HAJA KUBWANI, " ILA WAWEZA IPAKAA KWENYE UUME ULIOATHIRIWA.


Dawa hiyo unaipakaa mara Moja tu Ndani ya Masaa 24 tu basi.

3// Nunua Dawa inaitwa CALAMINE LOTION 8% au 15 % , hii utaipakaa Kila baada ya Masaa nane Kila siku mpaka muwasho utakapokua umeisha.

4//Kwakua hali hiyo inamuda mrefu ni wazi mmeshapata machafuko wa Damu, na hivo mnatakiwa mpate Dawa za Antibiotics kulingana nanyi angalau Kwa siku Tano.

5// Kwakua Ina muda mrefu, itakua vema pia mkipata dawa hizi za vidonge
---mojawapo ya Cetirizine , au Loratidine
Pamoja na Prednisolone Kwa dozi ya siku zisizopungua 5 na dozi ziendane na mtumiaji.


SASA , Ile ya kupakaa nmesema unaipakaa mara Moja tu Kwa siku Moja, inamaana kesho yake unaoga vizuri unaendelea kuoga Kwa SABUNI yako, kupakaa CALAMINE LOTION na dawa nyingine za kumeza.

IKIFIKA SIKU YA 4 , RUDIA TENA KUIPAKAA DAWA BBE HIYO KAMA MWANZO...Kwann urudie?? Ule mpakao wa mara ya kwanza Huwa HAUNA UWEZO WA KUUA MAYAI , hivo baada ya mpako wa kwanza Yale Mayai hujiangua na kuendeleza tatizo, Ivo MPAKO wa Pili ni lazima ., yaan Kwa Ufupi unaweza pakaa siku ya 1 Kisha ya 4 na malizia ya 7.

Mengineyo.

Toa nguo zenu zote nje, mashuka ,makava ya magoro , makava ya makochi .

Chemsha Maji ya moto,.Kisha loweka hizo zote kwenye maji hayo ya moto baadae uanikie juani .

Nunua Dawa za kuua wadudu ,hata hizi RUNGU AU HIT ,Puliza Ndani kote hasahasa kwenye Kona za nyumba, uvungu wakitanda , makochi n.k .


UTAPONA WEWE NA FAMILIA YAKO NA HAKUTAKUA TENA NA MAAMBUKIZI HAYO .
 

Pole sana.

Kwa maelezo yako na picha huenda ikawa ni ugonjwa wa ngozi ambao kitaalamu hujulikana kama Scabies.

Ugonjwa huu unatibika kabisa kwa hiyo ipeleke familia yako yote kwa daktari mfanyiwe uchunguzi kisha mpatiwe dawa.

Pia hakikisheni mnafanya usafi wa mavazi yenu na mazingira ya nyumba kwa ujumla. Hakika mashuka ya vitanda ni masafi na yanabadilishwa mara kwa mara.

Kila la kheri.
 
Reactions: LA7
Watoto wangu walijikuna na dalali zote za hili tatizo ni sawa kabisa na yaliyotupata kwa kuangalia picha
Kila dawa tulitumia wapi na kila Dr alichemsha
Huu ugonjwa upo na wengine walisema ni Scabies
Watoto waliteseka sana Kama miezi mitatu ila baadae uliondoka wenyewe
Hakuna matabibu huko bali waganga njaa tu hata pharmacy walichemsha wengi sana na hawajui
Ugonjwa upo na unaambukiza huenda watoto wameutoa shule au kwenye michezo na wenzao
Vumilia tu ila sidhani kama wanajua dawa
Watapona wenyewe ila jaribu sana kubadili nguo zao kila wakati na kuzifua kwa maji ya moto
Na hata mashuka na foronya za mito pia
Kila la kheri mkuu
Kujikuna kuna kera sana
 
Reactions: LA7
Kuna katoto kaliumwa kakijikuna vinatumbuka, kisha vinaweka kovu jeusi mda mchache tu

Baada ya kutumia dawa mda mrefu haimkumsqdia kumpeleka kwa mhindi mmoja daktari huyo akashauri apinwe minyoo. Akakutwa mtoto aba minyoo

Akichosema yule daktari muhindi, watu wanatumia dawa bila kupona kwa sababu ya minyoo.

Dawa unayotumia ni sahihi kabisa, shida inakuwa minyoo inasababisha usipone haraka

Thanks, hopeful unepata kitu cha ziada.
 
Hii ni aleji inayoeeza kutokana na chakula hasa aina ya samaki, dawa yake ni ya sindano, ninakushauri nenda hospitali ya serikali achana na za binafsi.
 
Inaweza kuwa minyoo pia, kuna mtu nae alihangaika navyo kwa muda mrefu mpk alipompata daktari mzoefu ndio kupima ikaonekana minyoo ndio chanzo cha tatizo lake.
 
Possible reasons
  1. Chips zilizokaangiwa mafuta mabaya (yaliyochanganywa na ya transfoma)
  2. Sabuni
  3. Maji ya kuoga
  4. Nyama, maziwa (nyama ya mnyama aliyedungwa sindano hakumaliza siku saba )
Minyoo itokanayo na minyoo hasa nguruwe
 
Minyoo itokanayo na minyoo hasa nguruwe
Ni kweli, ila kuna jamaa yangu ilikuwa akila chips sehemu fulani anadhurika, mwaka jana walipokamatwa watu na mafuta ya transfoma ikagundulika moja ya soko la mafuta hayo ilikuwa ni pale Ubungo Maziwa
 
Huu mwezi wa 3? Familia yote? mmetumia dawa sana? Mkuu Nenda kanisani kama upo DSM pale mwenge mpakani kwa Prophet Nyakia.Utapona wewe na familia yako na kuambiwa chanzo.
Nimeona na kushuhudia watu wakipona.
Kuna kitu hakipo sawa kwenye huo ugonjwa umepigana na mwilini umeshindwa Basi nenda ukatatuliwe kwa mambo ya rohoni.

Usidharau hii.!
 
Sintosahau ,ugonjwa huu chuoni! Niliumwa miezi 6
Nenda huku mara kule ngoma ngumu! Kuna dr akasema una allergy ko jitahidi kuji assess chakula au kitu gani hukuletea allergy

Kaka nouma sana
 
Sintosahau ,ugonjwa huu chuoni! Niliumwa miezi 6
Nenda huku mara kule ngoma ngumu! Kuna dr akasema una allergy ko jitahidi kuji assess chakula au kitu gani hukuletea allergy

Kaka nouma sana
Unawasha balaa yaani ,hizo rangi zenu nyeupe!
 
Hiyo inaweza kuwa alegy aisee ni hatar sana ila kuna dawa kidonge kinauzwa 100 inaweza kusaidia ngoja niitafute nitakuludia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…