Polisi Dodoma: Mwenye taarifa kuhusu waliompiga Lissu risasi apeleke polisi

Polisi Dodoma: Mwenye taarifa kuhusu waliompiga Lissu risasi apeleke polisi

Kutokana na kile kinachoitwa watu wasiojulikana kumshambulia kwa risasi Rais wa TLS, MBUNGE/SINGIDA MASH.. na MWANASHERIA MKUU wa CHADEMA, Mh. Tundu Antipas Lissu.. (Allah ampe shifaa, Apone haraka!! AMINA.)
Iko haja kwa vyombo vya ulinzi na usalama kumhoji yule jamaa aliyeomba ruksa ya kutaka kumuua Mh. Tundu Lissu. Huyu mtu si wa kubezwa wala kupuuzwa, UHAI ni haki ya msingi ya kila binadamu na viumbe vingine, inapotokea mtu aliyetimamu anatishia uhai wa mtu mwingine tena hadharani na akionesha wazi hatanii, hilo si jambo la kubeza. Tena muda mfupi baada ya tamko lake hilo ambapo ni takribani wiki mbili tu, kunatokea jaribio la kuuawa mtu yule yule!! Hapana, huyu si wa kuachwa hivi hivi, haraka iwezekanavyo Jeshi la polisi limshikilie huyu mtu kwa mahojiano wakati upelelezi ukiendelea kuwabaini wahusika halali..!!!

SIASA SIO VITA, TUNATAKA AMANI YETU IENDELEE KUDUMU..!!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unadhani hizo kazi mtu anapewa kama keki.....

Wewe umemuamini kwa kuwa kaaandika mtandaoni na FAKE ID......,!!??

What if na yeye ni mwanausalama wa tiss...!!?

Acha mihemko
Mkuu Chadema nao wana akili zao... kuna taratibu za kufuata kabla ya kumpa mtu kazi kiongozi..
 
Kugeuza tukio baya na Unyama aliofanyiwa Wakili Msomi Tundu Lissu kuwa MTAJI WA KISIASA ni mtindio wa Akili na Upuuzi unaopaswa kupingwa na kila anayejitambua.

Lissu sio Chadema tu Lissu ni Mtanzania na kila mtanzania atakayeonewa na kufanyiwa dhulma awe mwanasiasa asiwe mwanasiasa wote wanastahili huruma yetu na sauti zetu kuwalilia , na kuwapigania katika uzito sawa.

Lissu anatetea maslahi ya Tanzania yote kwa Ujumla hivyo ni haki ya kila mtanzania kumlilia na kumuombea. Kuleta chuki zenu au tofauti zenu za Vyama kipindi ambacho taifa limeungana kumlipa fadhila mtu aliyejitolea muda na maisha yake kulipigania ni Ujinga na Upumbavu unaokera sana.

Tukio la Lissu linapaswa kuchukuliwa kama chachu ya mapambano dhidi ya Waovu na Madhalimu wa haki za Binadamu na utu kokote kule walikojificha.

Unyama huu haukuanza na LISSU wengi tumewazika waliuawa kwa dhulma na kwa kuonewa tu bila kosa lolote.

Watu wengi ndani ya taifa hili wamepotea, wameuawa, wametekwa, wamefungwa Jela kwa dhuluma na Uonevu, na wengine maiti zao zimeokotwa kando kando ya mito, maziwa nk baadhi yenu hamkutaka kabisa kuongea na mliona hayawahusu.

Tulichukulie tukio hili kama kengere ya kuamsha mapambano dhidi ya Wahuni waliogeuza Taifa hili kuwa ni sehemu ambayo ukifumbua mdomo kuisemea haki unatafunwa. Tupambane na Wahuni wawe katika kichaka chochote walikojificha tukichome moto watoke angalau nasisi tuwe tunajiamini katika taifa letu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA

Sent using Jamii Forums mobile app
Maskini hii nchi sijui tunaelekea wapi!
Alianza Ben saa8, wakaja wengine tusiowajua, leo hii tena Lissu, sijui ni nani anafuatia!
 
Kutokana na kile kinachoitwa watu wasiojulikana kumshambulia kwa risasi Rais wa TLS, MBUNGE/SINGIDA MASH.. na MWANASHERIA MKUU wa CHADEMA, Mh. Tundu Antipas Lissu.. (Allah ampe shifaa, Apone haraka!! AMINA.)
Iko haja kwa vyombo vya ulinzi na usalama kumhoji yule jamaa aliyeomba ruksa ya kutaka kumuua Mh. Tundu Lissu. Huyu mtu si wa kubezwa wala kupuuzwa, UHAI ni haki ya msingi ya kila binadamu na viumbe vingine, inapotokea mtu aliyetimamu anatishia uhai wa mtu mwingine tena hadharani na akionesha wazi hatanii, hilo si jambo la kubeza. Tena muda mfupi baada ya tamko lake hilo ambapo ni takribani wiki mbili tu, kunatokea jaribio la kuuawa mtu yule yule!! Hapana, huyu si wa kuachwa hivi hivi, haraka iwezekanavyo Jeshi la polisi limshikilie huyu mtu kwa mahojiano wakati upelelezi ukiendelea kuwabaini wahusika halali..!!!

SIASA SIO VITA, TUNATAKA AMANI YETU IENDELEE KUDUMU..!!


Sent using Jamii Forums mobile app
Mnataka kwenda mbio wakati hakuna break..... Funzo sio tabia nzuri kutengeneza maadui bila sababu.... Ulimi uliponza kichwa!
 
Yule aliyemtishia nape mpaka leo hajakamtwa sembuse huyo wa Lissu
 
WATU WASIOJULIKANA.

Nimekaa nikijifikiria juu watu hawa ambao tumekuwa tukiwaita ama wakijiita "watu wasiojulikana"

Inasikitisha kuona kwamba pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia lakini bado tumeendelea kuandamwa na kuumizwa na watu hawa "wasiojulikana"

Hawa watu wasiojulikana wamefanya matukio mengi, wameua ,kujeruhi na kufanya uharibifu mkubwa lakini cha kusikitisha ni kwamba jeshi na serikali kiujumla limeshindwa kuwachukulia hatua kwa kisingizio kwamba ni "watu wasiojulikana"

Watu wasiojulikana umekuwa ni msamiati unaopendwa sana na jeshi letu la Polisi lakini tujiulize hao watu hawajulikani kwa nini?, watajulikana lini? Pamoja na jeshi kuwa na vifaa mbalimbali vyenye kuliwezesha kuwabaini wahalifu mbali mbali lakini linegonga mwamba kwa watu hawa wasiojulikana.

Mpaka Leo hii hatujui alipo kada wa CDM Beni saanane kisa alitekwa na watu wasiojulikana.
Ofisi za IMMA zililipuliwa na watu wasiojulikana, miili ya watu imekuwa ikiopolewa mara kadhaa baharini ikiwa kwenye viroba , Msanii Roma mkatoliki alitekwa na kuteswa na watu wasiojulikana,

Leo hii mh. Tundu Lissu amepigwa risasi na hao hao ambao polisi huwaita watu wasiojulikana.Ikumbukwe mh Lissu ameshawahi kulalamika kufuatiliwa na vijana wanaokuwa kwenye gari ambalo hadi plate number alizitaja ,, je Leo hii anapigwa risasi mnasemaje no watu wasiojulikana?

Kwa nini hawa watu wasiojulikana wamekuwa wakiwaandama wakosoaji wa serikali na si watu wengine ? Aliyemnyooshea bastola mh.Nape Nnauye amefanywa nini au hajulikani ilihali tukio alilifanya hadharani?
Kwa nini watu hawa wasiojulikana wamekazana sana awamu hii ya uongoz na sio hapo kabla? Imefikia mahali nchi ina watu wengi wasiojulikana kuliko wanaojulikana. So sad.

Kwa kumalizia tu niseme kwamba hao wanaojiita wasiojulikana pamoja na washirika wao watambue kwamba nothing last forever na mwisho was ubaya ni aibu. Vilio na majonzi ya wapenda amani nchi nzima havitaenda Bure
Nikisikia tu watu wasiojulikan imani ya kuwapata wahalifu huuwa nakosa kabsa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usipoteze mda wako hao ni majambazi sugu wa lumumba walitaka kupora uhai wake,majibu yao jana kua tuwasaidie ni tosha kabisa kujua

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi wewe kwa akili ya kawaida tu, ikiwa aliyevamia clauds fm na silaha, aliyemtishia Nape bastola mchana kweupe Serikali haikusema chochote, hivi Lissu ni muhimu kuliko Nape na clauds fm? Siwezi hitimisha matendo na hatua zitakazochukuliwa zitathibitisha hilo.
 
Hii picha ishaishia hapa mkuu hakuna kitakachoendelea,toka yule mtu ameandika aruhusiwe amuue uliona vyombo vyetu vya Usalama vikimuhoji,ila angetukanwa/Kutumiwa huo ujumbe Sizonje wao ungeshangaa mara moja mtu angeshakamatwa, nadhani tuweke maisha yetu kwa Mungu basi ila sio kwa Polisi wetu
 
Very true, hata hapa Jukwaani kulikua na Wapuuzi wengi wengi sana waliotaka na kuhamasisha Tundu Lissu auwawe, maandiko yapo hapa na maandiko yanaishi.
 
WATU WASIOJULIKANA.

Nimekaa nikijifikiria juu watu hawa ambao tumekuwa tukiwaita ama wakijiita "watu wasiojulikana"

Inasikitisha kuona kwamba pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia lakini bado tumeendelea kuandamwa na kuumizwa na watu hawa "wasiojulikana"

Hawa watu wasiojulikana wamefanya matukio mengi, wameua ,kujeruhi na kufanya uharibifu mkubwa lakini cha kusikitisha ni kwamba jeshi na serikali kiujumla limeshindwa kuwachukulia hatua kwa kisingizio kwamba ni "watu wasiojulikana"

Watu wasiojulikana umekuwa ni msamiati unaopendwa sana na jeshi letu la Polisi lakini tujiulize hao watu hawajulikani kwa nini?, watajulikana lini? Pamoja na jeshi kuwa na vifaa mbalimbali vyenye kuliwezesha kuwabaini wahalifu mbali mbali lakini linegonga mwamba kwa watu hawa wasiojulikana.

Mpaka Leo hii hatujui alipo kada wa CDM Beni saanane kisa alitekwa na watu wasiojulikana.
Ofisi za IMMA zililipuliwa na watu wasiojulikana, miili ya watu imekuwa ikiopolewa mara kadhaa baharini ikiwa kwenye viroba , Msanii Roma mkatoliki alitekwa na kuteswa na watu wasiojulikana,

Leo hii mh. Tundu Lissu amepigwa risasi na hao hao ambao polisi huwaita watu wasiojulikana.Ikumbukwe mh Lissu ameshawahi kulalamika kufuatiliwa na vijana wanaokuwa kwenye gari ambalo hadi plate number alizitaja ,, je Leo hii anapigwa risasi mnasemaje no watu wasiojulikana?

Kwa nini hawa watu wasiojulikana wamekuwa wakiwaandama wakosoaji wa serikali na si watu wengine ? Aliyemnyooshea bastola mh.Nape Nnauye amefanywa nini au hajulikani ilihali tukio alilifanya hadharani?
Kwa nini watu hawa wasiojulikana wamekazana sana awamu hii ya uongoz na sio hapo kabla? Imefikia mahali nchi ina watu wengi wasiojulikana kuliko wanaojulikana. So sad.

Kwa kumalizia tu niseme kwamba hao wanaojiita wasiojulikana pamoja na washirika wao watambue kwamba nothing last forever na mwisho was ubaya ni aibu. Vilio na majonzi ya wapenda amani nchi nzima havitaenda Bure

Kabila la watu wasiojulikana sijui wnatokea mkoa gani yawezekana Polisi wetu wanajua KABILA hili linatokea mkoa gani
 
Suala la Lissu naliona kwa macho mawl tu. Mosi, kukubalika kwake kuliko mtu yyte ndani ya cdm ili hari c takwa la mbowe. Pili, njama za mafisadi, drug dealers, waiba madini kwa lengo la kumchafua Rais aonekane ndo mhusika. Vita ya uchumi ni mbaya kuliko vita yyte duniani. Taarifa nilizo zpata toka kwa ndg yang aliepo nje ni kuwa uchumi wa mataifa yoooote duniani yaliyokua yananufaika kwa wizi wa madini na mali zngne toka Tz umeanza kuyumba. Hivyo wanatumia kila mbinu kuhakikisha Magu anachafuka sana kitaifa na kimataifa. Kisha wanatengeneza uadui mkubwa kati ya raia na serikali then vita inaanza chn ya ufadhili wao wanaanza kuyapola upya. Rejeeni what eventuates in Congo. The only way, tushikamane wahusika wa tukio hili la zaidi ya ushetani alilofanyiwa Lissu wapatikane na kunyongwa hadi kufa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na hii thread imendikwa na mtu asiyejulikana!

POLISI na WATU WASIOJULIKANA WANAHUSIKA HAPA!
 
Back
Top Bottom