Mkuu vitu viwili vibaya,havileti kitu kizuri kimoja,morals zimepotelea wapi?Bro raisi wa Naijeria wa sasa alifoji vyeti vya elimu. Kule kuna wasomi wengi sembuse Makonda aka Bashite
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu vitu viwili vibaya,havileti kitu kizuri kimoja,morals zimepotelea wapi?Bro raisi wa Naijeria wa sasa alifoji vyeti vya elimu. Kule kuna wasomi wengi sembuse Makonda aka Bashite
Umeishiwa pumzi naona?
Uko sahihi kabisa, anafanya siasa za publicity kwa kuteka wasiojielewa eti anafanya alichokuwa anafanya Magufuli. Lakini ukweli unafahamika huo umati ni wa kutengeneza kwa gharama kubwa, na ndio maana ilipofika uchaguzi wa 2019 & 2020 ilibidi wanajisi uchaguzi, maana walikuwa wanajua umati wao ni nguvu za Dola na Wala haukuwa na uhalisia.Pascal Mayalla
Hakuna amsha amsha ni kutafuta umaarufu kwasababu maalumu, kuficha maouvu
Publicity unaoyoiona si kwa ajili ya chama ni kujisafisha akijua ananuka dhulma na mikono imejaa damu!
Huyu bwana anafahamu aliumiza Umma, hakuna alichokifanya kikafanikiwa isipokuwa kusimamia mabaya. Amejaza vijana mitandaoni wana post upuuzi ili umma usahau au afiche maovu aliyotenda zama zile
Pili, anafanya kazi bila kufikiri kwasababu tu ya kutafuta umaarufu. Si mara ya kwanza kumbuka!
Mfano, juzi kaambiwa kuna maiti imezuiliwa Hospitali ya Sekotoure.
Bila kuuliza au kuwasiliana na Hospitali, mwenezi akaagiza ambulance ikachukue mwili kwenda kuzika
Hospitali ni institution (Taasisi) inaongozwa kwa procedures na guidelines. Maiti kuzuiliwa kuna sababu.
Inawezekana kuna deni la matibabu linalopaswa kulipwa. Mambo ya hovyo kama haya yanaua taasisi kwasababu zinashindwa kujiendesha. Ndiyo yale ya amri za kutoa pesa za mwenge kwenye mashirika, yakafa
Ningemuelewa kama angesema atalipia gharama hizo , mwili utolewe.
Kutoa amri tu ni kukurupuka na kuitia taasisi hasara. Nani atafidia deni hilo kama lipo?
Unaweza kuona hajabadilika, ndio yale ya wanaume kutelekeza watoto, madawa ya kulevya mkoa mmoja kana kwamba Dar ni kisiwa n.k.
Hajui mipaka ya kazi au tofauti ya uenezi na u-RC wala hajui 'coordination and engagement''
JokaKuu
Babu Sihasa.Anachokifanya ni Swahihi.CCM NI TAASISI.Wanabodi
Huu ni wito kwa Katibu Mwenezi mpya wa CCM, Comred Paul Makonda, kwanza kwa kumpongeza kwa kuifufua hamasa ya CCM kupendwa upya na kukubalika sana kupitia amsha amsha zake za Magufuli type (populist na populism) kila anapopita, tatizo lake ni moja tuu, anaipiga hii ngoma kwa nguvu mno, hivyo kuirindimisha kwa mlio mkubwa sana. Tatizo la ngoma inayovuma, ni ukiisikia ngoma inavuma sana, ujue inakaribia kupasuka!. Ili twende salama na kufika salama 2025, sisi watu wenye jicho la tatu, tunampa ushauri wa bure Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo ili tufike salama, kwa speed aliyoanza nayo, kama ataendelea kwa kasi hii, asije kushangaa hii ngoma ikampasukia njiani kabla hatujafika safari yetu!.
Rule No. 1. Never Outshine Your Boss
Mwenezi hawezi kumuagiza Waziri Mkuu na kuonya mawaziri, kwa kuwapa ultimatums!. Makonda aishie kwenye kusisitiza utekelezaji tuu wa ilani, na sio kutoa amri kuwaamuru na kuwaamrisha mawaziri!. Makonda hawezi kum summon Waziri Mkuu au mawaziri kwasababu yeye sio mamlaka yao ya uteuzi wala ya nidhamu. Mawaziri hawawajibiki kwa chama, wanawajibika kwa rais. iwapo kuna Waziri yoyote hajatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kikamilifu, chama kinamshitaki kwa rais ndie mamlaka pekee inayoweza kuwa summon na sio Mwenezi!. Waziri Mkuu wa JMT hawezi kupewa maelekezo ya chama na mwenezi kwasababu PM ni mjumbe wa CC ya CCM. Huwezi kuwapigia simu mawaziri na kuwapa maelekezo kwasababu wewe sio rais wa JMT. Magufuli alikuwa anafanya hivyo kwasababu yeye ndio bosi wao!, Makonda asijifanye Magufuli!, huku ni kumu outshine his boss!.
Konda Boy ana overdo bila kujua!. Asioverdo ngoma ikipigwa sana, huwaga haichelewi kupasuka!.
Wito huu ni kwa wanaomtakia mema Paul Makonda na ili kulithibitisha kuwa tunamtakia mema, angalia tumeanza nae wapi.
Mimi nilianza nae hapa Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
Nikaja hapa Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni
Alipopitia misukosuko tukasimama nae kwanza kwa kutoa wito Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... kisha tukamshauri Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .
Kuna watu wenye roho za kwanini tukawaambia Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!
Na mwisho nikapendekeza Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze...
Hivyo mheshimiwa sana Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo, hii duniani ni tambara bovu, tembea nayo taratibu!.
Wish you all the best
Kakayo
Paskali
Na waliomuweka hapo wanajua ni mropakaji, ila wamemuagiza afanye siasa kama za awamu ya Tano, wakiamini siasa zile zilipata uungwaji mkono, lakini hawakuwa tayari siasa nyingine kufanyika, na wakahakikisha vyombo vya habari vinahubiri watakacho. Ni kama vile unatengeneza uongo kisha inafikia mahali unauamini mwenyewe, kisa tu hutoi ruhusa ya wanaokwambia unasema uongo kuweka uongo wako hadharani!Sio kwamba ana lengo la ku outshine mabosi wake, ni kwamba hajui mipaka na wigo wa kazi zake
Bosi wa zamani alimpoteza kwa kumfanya aamini kwamba yeye ni mtu mkubwa na muhimu sana nchini
Hajui kuchagua maneno ya kuongea . Mfano, majuzi amewashambulia wastaafu na tunajua alimshambulia Warioba.
Leo JK ambaye ni mstaafu anamwakilisha Rais huko Finland, sasa sijui alimaanisha wastaafu wapi wakae kimya
Anapenda sana kufungua kinywa bila kupima uzito wa maneno yake.
By the way hajui kiswahili vizuri, utamsikia ''afazali, tahazali n.k. ''
Ngoja chadema waje waseme hy picha yao imepigwa kwenye angle ambayo haina watu wengi 😂Hapo juu ni watu waliohudhuria kutano wa mwenyekiti wa Chadema taifa mh Mbowe.
Na chini ni watu waliohudhuria mkutano wa katibu mwenezi wa CCM mh Makonda.
Picha zinajieleza zenyewe, alaf 2025 kuna watu wadai eti wameibiwa kura na wakati mwenyekiti wao mwenyewe ameuona moto akaamua kusanda na mikutano yake aliokuwa amepanga kaivunjilia mbali 🤣🤣🤣
HahahaKawe alumni na Bia yetu ndio nyakati zao za kurudi wakati wa kampeni.
Ingekuwa ni kwenye mahakama za kimataifa Leo hii Makonda angekuwa ndani. Lakini kwa hizi mahakama zilizo na kesi ya kina Mdee mwaka wa nne huu na ushahidi wote upo, utakuwa mjinga kwenda kupoteza muda wako mahakamani kumshtaki muhalifu aliyetumika na kiongozi dhalimu wa awamu iliyopita.Hizi tuhuma ulizoporomosha kwa kuwa mnawanasheria nguli na ni za uhakika bila chenga,nilitegemea kesi ziwe nyingi dhidi yake hasa amekaa benchi miaka mitatu bila kuwa na Godi faza,mkashindwa,mlijua mmemmaliza kisiasa
Kaibuka kwa upya mmeanza tena ngonjera zenu,
Watanzania sio mafala
Ni kweli, na ccm ni taasisi ya wahalifu, hivyo sio ajabu kuona wahalifu wakitumika kuifufua.Babu Sihasa.Anachokifanya ni Swahihi.CCM NI TAASISI.
Huyu bwana anachokifanya ni kutumia siasa chafu za wakati wa JPM, ni uongo mtupu .Uko sahihi kabisa, anafanya siasa za publicity kwa kuteka wasiojielewa eti anafanya alichokuwa anafanya Magufuli.
Umati unaouona ni maagizo anayotoa kwa viongozi wa CCM Wilayani na vijijini . Hawa wanamuogopa sana kwasababu ana nguvu hata za kumkaanga Waziri mkuu hadharani. Juzi alikuwa mgeni rasmi daraja la Busisi na Waziri anatoa taarifa kwake! Hata waziri hajui anawajibika kwa nani kwasababu ya hofu.Lakini ukweli unafahamika huo umati ni wa kutengeneza kwa gharama kubwa, na ndio maana ilipofika uchaguzi wa 2019 & 2020 ilibidi wanajisi uchaguzi, maana walikuwa wanajua umati wao ni nguvu za Dola na Wala haukuwa na uhalisia.
Ni kweli kabisa afanyacho Makonda ni kujifanya anaieneza ccm, lakini kwa wakati huo anajisafisha kwa kufanya siasa za maigizo. Anajua ni kwa kiwango alifanya uhalifu, Sasa anapima ni kwa kiwango gani watu wamesahau. Cha ajabu Kila mahali anatoa maagizo ya jukwaaani, lakini hakuna uhakika wala mrejesho wa utekelezaji wake, zaidi ya kufurahisha genge.
Mahakama ilikuwa 'msemaji wake' kwa kesi pale kinondoni. Yaani ilimtetea si kusikiliza kesiIngekuwa ni kwenye mahakama za kimataifa Leo hii Makonda angekuwa ndani. Lakini kwa hizi mahakama zilizo na kesi ya kina Mdee mwaka wa nne huu na ushahidi wote upo, utakuwa mjinga kwenda kupoteza muda wako mahakamani kumshtaki muhalifu aliyetumika na kiongozi dhalimu wa awamu iliyopita.
Huwa nawaelewa sana wazungu kwenye mikataba ya raslimali zetu kuamua mashauri Yao yaamuliwe kwenye mahakama za kimataifa. Wangekosea watumie mahakama za humu nchini, leo hii wangekuwa kama wamasai wa Loliondo.
Makonda ameibuka upya sio kwamba tumesahau uovu wake, bali tunaonyesha kuwa Yale yaliyoitwa maridhiano ilikuwa ni utapeli ili mama atawale bila pressure ya wapinzani. Lakini kiukweli bila wahalifu ccm haiwezi kufanya siasa.