Mjadala Wa hovyo sana huu. Hivi Samia ashindwe kwa tume ipi ya uchaguzi? Kura za nani zitakazohesabiwa za kumuondoa Samia madarakani. Polisi gani atakayesimamia vituo vya uchaguzi kuwazuia CCM kufanya wanavyotaka?. Samia labda akataliwe na CCM wenzie lakini siyo kwenye sanduku la kura. Tena, kwa taarifa yenu, kutokana na hizo kasoro mlizosema anazo, cjui, mwanamke, mzanzibar, ameuza Loliondo na Bandari, mnampa hasira tu za kushinda kwa kishindo kikuu km Kagame. Mana ni kuamua tu ngapi zitangazwe. Atangatazwa ameshinda kwa 99.9% ili kuwafunga midomo watu waliofikiria hatachaguliwa na CCM itatamba vibaya kwa ujambazi huo ktk uchaguzi. Mnaishi humu humu na hamuoni hali iliyopo, tena ni ya muda mrefu tu?