Prof. Assad: Mfumo wa Siasa una shida. Huwezi kuzungumzia Kilimo wakati huna Mabwawa

Prof. Assad: Mfumo wa Siasa una shida. Huwezi kuzungumzia Kilimo wakati huna Mabwawa

Bongo kipaumbele,platform kubwa sahv wanapewa wasanii wakata mauno

Ova

Basi
Hilo tu ndio wanajua kwa kweli
Yaani tunahitaji mabadiliko ya kiakili hata kama tuna viongozi wa ajabu itabidi tujiongeze sasa maana kwa hali hii hata miaka 200 bado tutakuwa hivi hivi
 
View attachment 2065734

Prof.Assad ametoa maoni yake kuhusu mfumo wa siasa wa nchi yetu. Siasa yetu inatufanya tusiwe na malengo yanayopimika. Anashangazwa na waziri kuzunguka kuchukua kero za wananchi wakati Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya wapo huko. Anasema labda sababu ni kupata posho tu.

Anasema watu wanazunguka kutaka ku score point za kisiasa tu.

Amegusia kuhusu kilimo. Anasikitika sana kuona kilimo kinaimbwa wakati hakuna mabwawa ya kutosha. Anashangaa serikali imeacha maji yaende baharini/ziwani kama vile bahari ndio ina shida na maji kuliko sisi 🤣🤣🤣🤣
Hivi huyu mzee hakuwahi kuajiliwa serikalini enzi ya ujana wake?
Huko nyuma serikali hazikua zinakosea na yeye hakuzisaidia wala kuwashauli kipindi hicho na amekuja kuyaona kuanzia enzi ya magufuli tu na wakati akiwa nje ya uwanja?

Kwa kuonyesha mfano hata wa maendeleo kwa sasa si aanzishe shule au hata mladi ili tuone utendaji wake na atakua amesaidia hata ajira na kuchangia uchumi wa nchi kuluko kila siku kurukaruka tu bika kutoa njia ya kusaidia hao anaowaona ni vilaza ila alipokuwa madalakani hakujiona pia ni kilaza.

Maana nchi iliyumba kuanzia huko nyuma.
 
Hivi huyu mzee hakuwahi kuajiliwa serikalini enzi ya ujana wake?
Huko nyuma serikali hazikua zinakosea na yeye hakuzisaidia wala kuwashauli kipindi hicho na amekuja kuyaona kuanzia enzi ya magufuli tu na wakati akiwa nje ya uwanja?

Kwa kuonyesha mfano hata wa maendeleo kwa sasa si aanzishe shule au hata mladi ili tuone utendaji wake na atakua amesaidia hata ajira na kuchangia uchumi wa nchi kuluko kila siku kurukaruka tu bika kutoa njia ya kusaidia hao anaowaona ni vilaza ila alipokuwa madalakani hakujiona pia ni kilaza.

Maana nchi iliyumba kuanzia huko nyuma.
mzee mbona povu? relax,mbona ushauri mzuri tu umetolewa? au nyie ndo wale wanaoitwa hawashauriki?
 
Nchi hii kweli ngumu sana Yan kuna baloz kuna mjumbe kuna mwenyekit ,mtendaji, kuna katibu tarafa, kuna diwan, kuna mkurugenzi, kuna mkuu wa wilaya kuna mbunge hiyo n ngaz ya wilaya tu halafu bado anakuja wazir na mkuu mkoa mpaka mkuu wa nchi Hawa viongoz wengine huwa wanafanya kaz gan
 
Huwa inauumiza sana,kuona namna tunavyo ongozwa na watu wasio na Vision,hawana ubunifu wala sera.
Wanawaza per diems pekee..wananchi wanaogelea kwenye UMASKINI wa kutupwa..
Hayo mabwawa kujengwa kwa Kila kijiji n muhimu sana unaweza ukajenga lakwako private wakaja viongoz wakakuweka ndan wanakwambia unakausha mto ukisema uingize mipira mton uvute maji pia n kosa nchi hii kilimo kiko nyuma viongoz ndohao
 
Kuna DAS, RAS, Mwenyekiti wa Halmashauri au Meya.Bado Kuna mameneja lukuki wa TANESCO, EWURA, TRA, TARURA, Idara za maji ngazi za mikoa pia!
Nchi hii kweli ngumu sana Yan kuna baloz kuna mjumbe kuna mwenyekit ,mtendaji, kuna katibu tarafa, kuna diwan, kuna mkurugenzi, kuna mkuu wa wilaya kuna mbunge hiyo n ngaz ya wilaya tu halafu bado anakuja wazir na mkuu mkoa mpaka mkuu wa nchi Hawa viongoz wengine huwa wanafanya kaz gan
 
Wakulima wanachukiliwa kama ni Watanzania wa daraja la mwisho. Nobody cares about them zaidi ya kuwaimbia mapambio ya kisiasa tu.
Kijijini kwetu Kuna mto mkubwa ambao haukauki miaka yote,na ulikuwa hauna matumuzi yoyote zaidi ya kuvua visamaki vidogo godo, na maji ya kutumia majumbani. Baadae wakulima kidogo kidogo wakaanza kuweka pump ili waweze kulima nyanya, vitunguu na mazao mengine ya mboga mboga ili wajipatie fedha badala ya kutegemea mahindi ya mvua za msimu. Kiukweli vijana wengi wakaingia huko, wananunua water pumps na vifaa vingi vya umwagiliaji na wakaanza kubadilika kimaisha kwani fuso toka mjini zikawa kila siku zinakuja kubeba mazao. Lafla from no where usiku watu wa maji bonde wakavamia mashamba ya watu na kung'oa water pumps na kuondoka nazo kwa maelekezo kwamba ni marufuku kuvuta maji mtoni daah
 
Asante Prof. Huwa simkubali,lkn nikiondoa Personalities zangu na yeye, kaongea pointi tamu sana.
 
Nchi hii kweli ngumu sana Yan kuna baloz kuna mjumbe kuna mwenyekit ,mtendaji, kuna katibu tarafa, kuna diwan, kuna mkurugenzi, kuna mkuu wa wilaya kuna mbunge hiyo n ngaz ya wilaya tu halafu bado anakuja wazir na mkuu mkoa mpaka mkuu wa nchi Hawa viongoz wengine huwa wanafanya kaz gan
Saivi anaitwa AFISA TARAFA(DO-Division Officer)
 
Hili suala la mawaziri kuzunguka mikoani mfano stendi za mabasi kukakugua tiketi lidhibitiwe kupunguza matumizi ya serikali hasa kipindi hichi ambapo kuna mjadala mkali kati ya kukopa zaidi au kuongeza tozo.
Imagine wilayani Kuna : DED na full team ya wataalamu kwa kila Idara, Kuna DC, Kuna DAS, Kuna WEO, Kuna afisa Tarafa... Bado mkoani hapo but still waziri anazunguka kwenye vijiji kukagua madarasa, miradi ya maji, barabara, stend, masoko etc... Huwa Najiuliza ni lini waziri anapata muda wa kukaa na timu yake Wizarani ku review Sera na mipango mbali mbali ya wizara? Mfano haya madarasa mapya, zahanati na vituo vya afya vipya nini plan za wizara kuhusu watumishi wapya? Vifaa tiba?? Madawa??
 
Imagine wilayani Kuna : DED na full team ya wataalamu kwa kila Idara, Kuna DC, Kuna DAS, Kuna WEO, Kuna afisa Tarafa... Bado mkoani hapo but still waziri anazunguka kwenye vijiji kukagua madarasa, miradi ya maji, barabara, stend, masoko etc... Huwa Najiuliza ni lini waziri anapata muda wa kukaa na timu yake Wizarani ku review Sera na mipango mbali mbali ya wizara? Mfano haya madarasa mapya, zahanati na vituo vya afya vipya nini plan za wizara kuhusu watumishi wapya? Vifaa tiba?? Madawa??
Tutachelewa sana kwa mtindo huu na maendeleo tutaendelea kuyaona kwa wenzetu kwenye TV.
 
Tulishasema,serikali ingejikita kwenye kuwezesha sekta ya kilimo,hata umachinga
Ungepungua mijini

Ova
Exactly mkuu... Imagine wakakopa hata Trilioni 3 wakaanza intensive program ya kuboresha kilimo, hasa kilimo cha kumwagilia, wakahakikisha kwanza ardhi kwenye vijiji vyote 15,000 inapimwa (wataalamu from UDSM, SUA na ARDHI Universities) kujua soil fertility kama ipo au mbolea gani inahitajika na mazao gani yapandwe. Pili extension officers wa kilimo, mifugo, uvuvi, masoko na ushirika wamwagwe hata kwa ajira za muda huko vijijini ili wawasaidie wakulima kwenye upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, namna bora ya kuandaa mashamba, kuhudumia mashamba, kuvuna kwa wakati, namna bora ya kuhufadhi mazao, kutafuta masoko ya pamoja etc... Hata kama hawawezi kuanza nchi nzima waanze awamu ya kwanza mikoa kumi yenye potential kubwa kwenye kilimo... Vijana huko vijijini wakipata fedha za kutosha kwenye kilimo, wengine kuuza mazao, wengine kuuza pembejeo, wengine kununua kirikuu na fuso za kusafirisha mazao, wengine kununua boda boda, trekta, power tillers, etc hawatakuwa na muda wa kukimbilia mjini kuuza karanga au kuuza vitunguu barabarani...
 
Profesa namkubali.
Hapa nilikuwa najiuliza kwanini nisijenge bwawa langu au kisima kikubwa chini ya milima huku kwetu. Navuna maji ya mvua kwa miezi 3 hadi 4. Nasafirisha maji kwa mabomba ya mipira hadi shambani.

Tanzania kuna mengi hatuja fanya.
Mkuu mfano ukiwa pesa kidogo ukachimba bwawa kwa kutumia katapila maji yanaweza kukaa mpaka miezi Saba - nane, yaani una uhakika wa mvua nyingine kuyakuta maji yako hayajaisha. Hivyo kamwe hautakuwa na shida ya maji labda itokee mvua imegoma mwaka mzima.
 
Nchi hii kweli ngumu sana Yan kuna baloz kuna mjumbe kuna mwenyekit ,mtendaji, kuna katibu tarafa, kuna diwan, kuna mkurugenzi, kuna mkuu wa wilaya kuna mbunge hiyo n ngaz ya wilaya tu halafu bado anakuja wazir na mkuu mkoa mpaka mkuu wa nchi Hawa viongoz wengine huwa wanafanya kaz gan

Wakitukanwa kwenye mitandao kwa madhaifu yao ndio utawaona wanafanya nini
Ila nyuzi kama hizi huwachangii bungeni wala vijijini
 
Back
Top Bottom