TANZIA Profesa Honest Ngowi afariki dunia kwenye ajali Mlandizi Pwani. Alikuwa mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe

TANZIA Profesa Honest Ngowi afariki dunia kwenye ajali Mlandizi Pwani. Alikuwa mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe

 
APUMZIKE KWA AMANI MWALIMU WETU. POLE KWA WANAJUMUIYA WOTE WA MZUMBE UNIVERSITY
Screenshot_20220328-102613_WhatsApp.jpg
Screenshot_20220328-102613_WhatsApp.jpg


Screenshot_20220328-102559_WhatsApp.jpg


Screenshot_20220328-102539_WhatsApp.jpg
 
Habari Wote.

Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lughano Kusiluka anasikitika kutangaza kifo cha Prof. Honest Ngowi na Dereva wake, waliofariki asubuhi ya leo kwa ajali ya gari wakiwa njiani kuja Kampasi Kuu Morogoro.

Tunaomba muwe watulivu wakati Menejiementi inaendelea kufuatilia taarifa kamili ya tukio hili, na kuweka taratibu zingine. Taarifa zaidi zitatolewa rasmi na taratibu zingine za kuwahifadhi wenzetu.

Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina la Bwana lihimidiwe. Poleni Wote kwa msiba huu mzito.

Imetokewa na,

Ofisi ya Mawasiliano

Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu Mzumbe amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi ya leo eneo la Mlandizi, Kibaha mkoani Pwani. Lori iliacha njia na kuilalia gari ya Ngowi. Alitoka kwenye ajali akiwa majeruhi, amefariki akiwa hospitali

View attachment 2166663
Profesa Honest Ngowi enzi za uhai wake​
View attachment 2166709

Pia soma > Dkt. Honest Ngowi aichambua sekta ya gesi na kukiri Serikali imejipanga

I saw him last week at Mlimani City. Alionekana Ana nguvu zake. Kumbe ndio bye bye
 
Apumzike kwa amani, Dah jana tu nimetoka kudownload CV yake hakikia tumepoteza nguli wa uchumi.
 
Mida ya alfajiri huwa ni mida ya usingizi mwingi sana hasa kawa dereva aliedamka usiku mkubwa au kama hakuwa na usingizi wa kutosha kupumzika, najua wale madereva wa safari ndefu hili mtakuwa mnalijua. Pole kwa wafiwa...
 
R.I.P

Hii barabara isipotanuliwa na kuweka dual carriage way tutaisha sana kwa kweli lawama tutawapa sana madereva lakini ukweli tuuseme barabara hii ni bado ya kizamani hailingani na matumizi ya idadi ya magari iliyopo sasa.

Wanasiasa hebu tumieni hicho kiwango cha posho zenu kuokoa maisha ya watu kwa ajali ambazo huenda zingeepukika.

Hivi nchi mnazoenda kutembelea hamjifunzi tu kitu cha kufanya?

Oneni aibu kwa kuchelewa kujenga dual carriage way ya dar to morogoro tunazidiwa na nchi kama Zambia kweli?

Kifupi njia ya Dar, Morogoro au Dar chalinze ilipaswa kuongezwa walau njia zisizopungua mbili hadi tatu.
 
Wana magari mazuri ndio lakini waambieni waendeshe magari taratibu nayo yametengenezwa na binadamu.

R.I.P NGOWI
 
Back
Top Bottom