peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 14,255
- 23,949
Kweli Bala is always here.😜😜Mzee...Gari limeangukiwa na Container kwa bahati mbaya...Bado tu unamlaumu Dereva?
Habari Wote.
Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lughano Kusiluka anasikitika kutangaza kifo cha Prof. Honest Ngowi na Dereva wake, waliofariki asubuhi ya leo kwa ajali ya gari wakiwa njiani kuja Kampasi Kuu Morogoro.
Tunaomba muwe watulivu wakati Menejiementi inaendelea kufuatilia taarifa kamili ya tukio hili, na kuweka taratibu zingine. Taarifa zaidi zitatolewa rasmi na taratibu zingine za kuwahifadhi wenzetu.
Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina la Bwana lihimidiwe. Poleni Wote kwa msiba huu mzito.
Imetokewa na,
Ofisi ya Mawasiliano
Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu Mzumbe amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi ya leo eneo la Mlandizi, Kibaha mkoani Pwani. Lori iliacha njia na kuilalia gari ya Ngowi. Alitoka kwenye ajali akiwa majeruhi, amefariki akiwa hospitali
View attachment 2166663View attachment 2166709
Profesa Honest Ngowi enzi za uhai wake
Pia soma > Dkt. Honest Ngowi aichambua sekta ya gesi na kukiri Serikali imejipanga
Alikuwa anafugia wapi?Daaah, Mungu wangu..nimelia kwa uchungu sana,
Jana mchana tu nimetoka kwake kutibia Mifugo yake.
Rest in peace Prof[emoji24]
Kwake ni makabe karibu na kituon cha polisi .Alikuwa anafugia wapi?
Namfananisha ndiye mwenye mtoto bonge?
R.I.P
Hii barabara isipotanuliwa na kuweka dual carriage way tutaisha sana kwa kweli lawama tutawapa sana madereva lakini ukweli tuuseme barabara hii ni bado ya kizamani hailingani na matumizi ya idadi ya magari iliyopo sasa.
Wanasiasa hebu tumieni hicho kiwango cha posho zenu kuokoa maisha ya watu kwa ajali ambazo huenda zingeepukika.
Hivi nchi mnazoenda kutembelea hamjifunzi tu kitu cha kufanya?
Oneni aibu kwa kuchelewa kujenga dual carriage way ya dar to morogoro tunazidiwa na nchi kama Zambia kweli?