TANZIA Profesa Honest Ngowi afariki dunia kwenye ajali Mlandizi Pwani. Alikuwa mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe

TANZIA Profesa Honest Ngowi afariki dunia kwenye ajali Mlandizi Pwani. Alikuwa mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe

Screenshot_20220328-140924_Edge.jpg


vichwa vinapukutika..
 
Siku zile za kwanza, Magufuli alipokuwa fearsome dictator,Profesa Ngowi ndiye aliyekuwa one of the first people kutoa maoni mbadala kuhusu Sera za uchumi. Yaani,wakati ule ilikuwa siyo safe kumpinga Magufuli.
Acha ujinga wako Magufuli na Ngowi wamashatutoka umekalia ujinga wa wanasiasa hapa. Ngowi alikuwa anajitambua na hakuendeshwa na mihemko yenu ya kutukana viongozi.
 
Kwa mara ya kwanza kuonana naye ilikuwa wiki juzi pale Mzumbe University Dar Es Salaam Campus, tokana na physical appearance psychology alikuwa ni mtu mwenye hekima sana.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe milele amina [emoji26]
Kheeeh Dar kuna mzumbe university? Campus iko sehemu gan?
 
Majina ya watu yanaendana na tabia, Honest kama jina lako lilivyo, nimesikiliza interviews zake nyingi, alizungumza concept za uchumi In a very honest way, kiasi kwamba kila mtu alimuelewa. RIP prof
 
Yaani siku hizi ajali ikitokea lazima neno Morogoro liwepo.
 
Kheeeh Dar kuna mzumbe university? Campus iko sehemu gan?
Barabara ya Upanga ukitokea Mnazi Mmoja kuelekea Posta mpya, baada ya kupita kituo cha dala dala "Baridi" kabla ya kufika maktaba kuu ya Taifa kuna barabara inakunja kushoto 1 kwa 1 hadi MUDC ambapo ni kwa umbali wa robo 3 ya kilometers toka kona ya barabara kuu.
 
Prof Ngowi. Umeondoka kimasihara. Tumefanya KAZI nyingi pamoja. Sijawahi kuona binadamu msomi aliyeweza kutumia vipawa vyake Kwa umma Kwa upendo na weledi kama wewe. Msomi uliyejikita kwenye Elimu Kwa vitendo.

Mchapakazi Kitaaluma na binafsi. Uliiongoza Mzumbe Dar Campus kwa weledi mkubwa mno, humbled leader down to Earth. Tanzania tumempoteza MTU ambaye alikuwa tajiri wa Moyo na umefikia wengi mno.

My brother nitakukumbuka kwa mengi personal na kikazi tulipoweza kufanya KAZI nyingi pamoja na tumeishia kuwa marafiki. Ninaumia mno moyoni. Akili imetulia kwa muda natafakari sipati majibu.
Kwa nini watu muhimu kama hawa,hamuwajulishi na wenzenu wengine,ili wafaidike kwa ushauri.Mpaka wanafariki,ndio unapata habari zao.
Tuacheni ubinafsi,ikiwa kuna watu muhimu,tujulishaneni.
 
Amenifundisha industrial economics and international trade wakati nasoma Mzumbe. Juzi tarehe 25 nimeonana nae tena serena. Akaniuliza upo wapi sasa kijana. Dah kumbe ndio nilikuwa namuaga
 
Mmefukuza madereva wazuri kwa sababu za kipuuzi za vyeti fake mara sijui dereva naye awe form four wakati mbunge ni darasa la saba, pumbavu kabisa.

Qualification ya driver ni driving license na siyo hawa waliokosa ajira kwenye soko la ajira na kukimbilia udereva, kuendesha Passo yako ni tofauti kabisa na professional driving.

Ukiwa unasafiri jihadhari sana na hizi plate namba za STL, DFP na SU, hakuna madereva humo siku hizi ndio mitambo ya kupeleka watu kuzimu.

Wewe nae punguza uropokaji tuuu hii ajali hajasaba ishwa na dereva!
 
Habari Wote.

Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lughano Kusiluka anasikitika kutangaza kifo cha Prof. Honest Ngowi na Dereva wake, waliofariki asubuhi ya leo kwa ajali ya gari wakiwa njiani kuja Kampasi Kuu Morogoro.

Tunaomba muwe watulivu wakati Menejiementi inaendelea kufuatilia taarifa kamili ya tukio hili, na kuweka taratibu zingine. Taarifa zaidi zitatolewa rasmi na taratibu zingine za kuwahifadhi wenzetu.

Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina la Bwana lihimidiwe. Poleni Wote kwa msiba huu mzito.

Imetokewa na,

Ofisi ya Mawasiliano

View attachment 2166663
Profesa Honest Ngowi enzi za uhai wake
Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu Mzumbe amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi ya leo eneo la Mlandizi, Kibaha mkoani Pwani. Lori iliacha njia na kuilalia gari ya Ngowi. Alitoka kwenye ajali akiwa majeruhi, amefariki akiwa hospitali.

Pia soma > Dkt. Honest Ngowi aichambua sekta ya gesi na kukiri Serikali imejipanga


=======

Professor Honest Prosper Ngowi (PhD Economics) alikuwa mkuu wa idara ya kozi fupi, utafiti na ushauri chuo kikuu cha Mzumbe kampasi ya Dar es Salaam. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya ushauri ya ANO. Katika maisha yake amekuwa mtafiti, mshauri na kuchapisha machapisho ya kitaaluma zaidi ya 60, tafiti zaidi ya 70 pia makala zaidi ya 250 kwenye magazeti.

Prof. Ngowi amebobea kwenye uchumi wa maendeleo na biashara hasa kwenye uchumi mkubwa, biashara ya kimataifa, uwekezaji wa kigeni, ujasiriamali, uchumi wa mafuta na gesi na mengineyo. Prof. Ngowi pia amefanya kazi kama msahihishaji wa nje kwenye vyuo mbalimbali ikiwemo chuo kikuu cha Makerere, Udsm, North West University(Afrika kusini) na vingine vingi.
Duu! Hakika ni piga kubwa si kwa familia yake tu hata taifa kwa ujumla
 
Amenifundisha industrial economics and international trade wakati nasoma Mzumbe. Juzi tarehe 25 nimeonana nae tena serena. Akaniuliza upo wapi sasa kijana. Dah kumbe ndio nilikuwa namuaga
Haswaa...alipenda sana kutumia neno "kijana" RIP Ngowi profesa wa mfano wa kuigwa chuo kikuu Mzumbe
 
Anaongelea defensive driving , ambayo haswa ni package mahsusi unapoendesha executives.
Unaweza kuona tu ni lori limeangukia hiyo land cruiser , lakini dereva mahiri hawezi kuingia kwenye akward situations kirahisi.
Nakushukuru kwa kuwaelimisha wenzetu ambao hawapendi kujifunza kutoka kwa wenzao!
 
Mmefukuza madereva wazuri kwa sababu za kipuuzi za vyeti fake mara sijui dereva naye awe form four wakati mbunge ni darasa la saba, pumbavu kabisa.

Qualification ya driver ni driving license na siyo hawa waliokosa ajira kwenye soko la ajira na kukimbilia udereva, kuendesha Passo yako ni tofauti kabisa na professional driving.

Ukiwa unasafiri jihadhari sana na hizi plate namba za STL, DFP na SU, hakuna madereva humo siku hizi ndio mitambo ya kupeleka watu kuzimu.
Kwenye kudondokewa na kontena, dereva unamuhusishaje?
 
Back
Top Bottom