Rais ajaye Tanzania atokane na mmojawapo wa viongozi wafuatao

Rais ajaye Tanzania atokane na mmojawapo wa viongozi wafuatao

Duh Kinana tena..huyo na msoga pua na mdomo..haramu ya kinana halali ya msoga, haramu ya msoga halali ya Kinana.
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana:

1. Mzee.Abdulrahman Kinana
2. Prof. Palamagamba Kabudi
3. Dkt Bashiru Ali Kakurwa
4. Dkt. Hussein Mwinyi
5. PM Kassim Majaliwa

Nitarudi Kwa ajili ya Part 2 kuwaelezea na kuelezea Kwa nini nchi inawahitaji zaidi

Hussein Mwinyi hapana, hafai.
Anauza visiwa vya Zanzibar kwa Waarabu kama ambavyo Samia anauza bandari za Tanganyika kwa Waarabu wa Dubai.
Huo ni uhaini dhidi ya Jamhuri.
Uhaini unamwondolea kiongozi yeyote sifa ya kuendelea kuwa kiongozi.
KInana hapana, maana ile kashfa ya meli bado inamwandama.
Majaliwa hapana maana naye anaunga mkono hadharani kuuzwa kwa bandari zetu.
Kabudi na Kinana tuendelee kuwafikiria.
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana:

1. Mzee.Abdulrahman Kinana
2. Prof. Palamagamba Kabudi
3. Dkt Bashiru Ali Kakurwa
4. Dkt. Hussein Mwinyi
5. PM Kassim Majaliwa

Nitarudi Kwa ajili ya Part 2 kuwaelezea na kuelezea Kwa nini nchi inawahitaji zaidi
Huyo palamagamba toa kabisa
 
Makamu wa Rais
Dr. Philip Mpango anastahili kugombea Uraisi.
Kwakweli ana sifa zote.

Ni mnyenyekevu na Mchamungu.

Tunahitaji Kiongozi Mchamungu.
Kwa Karne hizi za Ukoloni Mambo Leo.
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana:
4. Dkt. Hussein Mwinyi
Naunga mkono No. 4, nami niliwahi kumpendekeza Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke nilisema
Wanabodi
Haya mambo ya mtu kusikia sauti, sio mambo ya ulimwengu huu wa mwili, haya ni mambo ya ulimwengu wa Roho.

Lakini kama ataisikia hii sauti, sio vibaya kama atajiandaa na kumuandaa mtu wa kumpokea, kwa maoni yangu, Dr. Hussein Mwinyi atatufaa sana, hivyo namuomba Rais Samia akiisikia sauti, amuombe Dr. Hussein Mwinyi, kwa uchaguzi wa urais wa 2025 aje kugombea urais wa JMT, kuimalizia awamu ya pili ya Mama Samia kwa yeye kukubali kuwa rais wa JMT kwa awamu moja tuu.

Hili la Mwinyi kuja huku, sio la sauti, hili ni langu tuu,
P.
P
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana:

1. Mzee.Abdulrahman Kinana
2. Prof. Palamagamba Kabudi
3. Dkt Bashiru Ali Kakurwa
4. Dkt. Hussein Mwinyi
5. PM Kassim Majaliwa

Nitarudi Kwa ajili ya Part 2 kuwaelezea na kuelezea Kwa nini nchi inawahitaji zaidi
Kwa nini hukuniweka mimi wa kwanza?
 
1. Mzee.Abdulrahman Kinana

Meli ya huyu dingi ilikutwa na pembe za ndovu huko Vietnam akadai eti ni kweli yeye meli ni yake ila hajui mteja alikuwa kapakia nini. Hauwezi kupakia mzigo kwenye meli bila kujua kilichopakiwa. Uadilifu wake ni mashaka matupu. Hafai kuwa Rais wa Tanzania.

2. Prof. Palamagamba Kabudi

Huyu dingi hana kashfa za ufisadi ila alishiriki kudanganya watanzania kwamba tunaidai Barric trilioni 495. Kwa uongo alioshiriki hafai kuwa Rais.

3. Dkt Bashiru Ali Kakurwa

Katibu mkuu kiongozi wa zamani hafai kabisa kuongoza nchi ya kidemokrasia. Alishiriki kikamilifu kubomoa umoja wa watanzania uliojengwa kwa miaka mingi. Shukrani kwa Mama Samia kuleta maridhiano tena.

4. Dkt. Hussein Mwinyi

Dr Mwinyi anafaa kwa zaidi ya 100% kuwa Rais wa Tanzania. Sifa zake zinaeleweka hakuna haja ya ufafanuzi.

5. PM Kassim Majaliwa

PM pia anafaa sana. PM anaweza kulaumiwa ila kwa cheo chake sio mwamuzi wa mwisho kwahiyo mambo mengine sio kwa utashi wake. Imagine huyu ndo PM pekee aliyewahi kuambiwa na boss wake kuwa mashangazi zake watapigwa. PM anafaa kuwa Rais wa Tanzania.
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana...
Ni hivi , Rais wa halali hutokana na Uchaguzi ulio huru na haki , ambao unamtoa kiongozi wa Watu aliyechaguliwa kihalali , kiongozi hatajwi na mtu binafsi kama wewe .

Zipo taarifa humu kwamba Hussein Mwinyi alikataa kujiunga na mafunzo ya JKT wakati ule alipotoka Shule , Hata leseni ya Udaktari wake inadaiwa alijipa kimabavu baada ya kuwa Naibu Waziri wa Afya , inadaiwa aligoma kufanya Mafunzo kwa vitendo ( Internship ), huyu ana uzalendo gani wa kumpa urais ? ni vema mkawajua kiundani hawa mnaowapigia debe .

Kasimu Majaliwa alishiriki kuteka kila mtu wa upinzani aliyegombea ubunge kwao 2020 ili apite bila kupingwa , yaani unakuwa PM halafu unaogopa uchaguzi , mtu kama huyu awezaje kuwa Rais ? acheni kudharau watanzania .

Mpaka leo muulize Kabudi ile dawa ya corona aliyoenda kuisomba Madagascar ilitibu watu wangapi ? au muulize ule uongo kuhusu fidia tutakayolipwa kwenye madini ulimsaidia nini Mtanzania ?
 
Makamu wa Rais
Dr. Philip Mpango anastahili kugombea Uraisi.
Kwakweli ana sifa zote.

Ni mnyenyekevu na Mchamungu.

Tunahitaji Kiongozi Mchamungu.
Kwa Karne hizi za Ukoloni Mambo Leo.
Sifa ya urais sio unyenyekevu wala huo uchaMungu, kiongoz ukiendekeza hii tabia ya huruma Taifa kamwe haliwezi kupiga hatua.

Jifunzen kwa nchi zilizoendelea viongozi wao wako vipi?

Stable kimaamuzi na katili kwenye mambo ya kipuuzi.

Hao wacha Mungu ndio hao akina samia na huyo dct mpango wanyenyekevu mpaka wanafuga majizi nawao wenyewe wanaficha uwizi wao kupitia huo unyenyekevu uchwara...

Ni bora kuongozwa na dicteta kuliko hao wanafiki
 
Hii ndio orodha ya wanasiasa na viongozi ambao ninaamini kama akampokea mikoba Rais Samia basi nchi itasonga mbele Kwa Kasi sana:

1. Mzee.Abdulrahman Kinana
2. Prof. Palamagamba Kabudi
3. Dkt Bashiru Ali Kakurwa
4. Dkt. Hussein Mwinyi
5. PM Kassim Majaliwa

Nitarudi Kwa ajili ya Part 2 kuwaelezea na kuelezea Kwa nini nchi inawahitaji zaidi
Ninavyozidi kukua kiumri na kiakili nimejifunza kuwa RAMLI hizi chonganishi wala hazina ukweli....

Hayati JPM hakuwa mtajika mbele ya wale "wana mitandao"....

Mh.Rais SSH hatukumtegemea kuwa aliko....

Hakika Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye kesho yetu na ikifika inakuja na maajabu mengi mno...

Kubwa tu uendelevu wa utulivu wa taifa letu teule duniani ,amen[emoji120]

Hakika nabii Adam A.S aliishi Ngorongoro [emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom