Rais Joe Biden awaalika Viongozi wa Africa kwa majadiliano Washington

Rais Joe Biden awaalika Viongozi wa Africa kwa majadiliano Washington

Wasiwafanye Waafrika wajinga mbona miaka yote tangu mataifa ya Afrika kujinyakulia uhuru atukuwahi kusikia Merikani ikiweka mikakati kabambe ya kuiinua Afrika kiuchumi au kusaidia katika ujenzi wa miundo mbinu - Hakuna!! Walicho kuwa wanafanya ni kuwatetea: Makaburu, Wareno, Ian Smith na CIA kuwapatia makaburu taarifa za siri walizo tumia kufanikisha kumkamata Nelson Mandela.

Hii kitu ya Merikani suddenly kuanza kulichukulia bara la Afrika kuwa ni muhimu kwake,hii kitu inatia shaka sana sana, kuna kitu wanalenga.

Ninacho hisi mimi, hawa jamaa wana hidden ajenda tatu, ya kwanza na ambayo wanaichukulia seriously ni ujio wa Wachina barani Afrika, hii kitu inawakosesha usingizi kweli kweli , si kwa Marekani pekee bali hata mataifa ya bara la Ulaya, tumeshuhudia jinsi media zao zinavyo wakandia sana Wachina kwa kuwasingizia mambo chungu mzima yasio kuwa na ukweli wowote - Viongozi/Serikali za magharibi na media zao zilivyo za ajabu hawa zungumzii chochote kuhusu jinsi China ilivyo saidia African Nations to help themselves in terms of ujenzi wa Barbara, reli,Umeme,Mawasiliano kwa njia ya simu, Shule,Vyuo vya Ufundi, Viwanda, Hosptali nk.

Hapa swali ni: Hivi mataifa ya magharibi specifically Merikani inapozunguka Dunia nzima wakitangaza ubaya wa ujio wa Wachina barani Afrika na kwingineko hapo US wanakuwa wana na lengo gani zaidi ya Geopolitical reasons za kutaka kui-contain China kiuchumi na kijeshi, hivi US inataka bara la Afrika nalo lijiingize kwenye rivalry zao za kijinga na hatarishi.
Hakika
Ila kikubwa US EU na shost zao wanataka kurejesha ushawishi ambao umepotea ama unapotea huko AFRIKA kufuatia ujio wa UCHINA INDIA TURKEY nakwambaali RUSSIA
Je atafanikiwa huu mkutano utaleta mwanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ipo wazi kuwa bara la afrika limepoteza imani kwa marekani na ulaya mpaka sasa urussi na uchina wameimarisha sana mahusiano na mataifa mengi ya afrika, hili jambo linamkosesha mzungu usingizi. Mpaka sasa ulaya na marekani wapo dilema hawajui chakufanya tena wamebaki wakiweka vikwazo ambavyo urussi anavipangua. Juzi saudi arabia kanunua tani za mafuta kutoka urussi, serikali ya mali nayo imeungana na urussi na wamekubaliana kushirikiana ktk nyanja mbali mbali ikiwemo kupambana na ugaidi hii ni dhahiri ufaransa amepoteza ushawishi nchini mali, china amejenga jengo la bunge kwenye moja wapo za nchi za kusini mwa afrika na kulikabidhi kule ulaya wanajadili namna ya kutoa pesa kwa nchi za afrika kupambana na umaskini. Binafsi naamini kuwa hata vita inayoendelea huko ukraine ni mkakati kabambe kwa mataifa ya ulaya na marekani
Kabisa MKUU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Avamie Urusi aue Urusi ila alalamikiwe msaidiaj , mlitaka aachwe tu kuua km alivyowaua watu huko Georgia 2008 au huko Moldova alivyopora jimbo au huko Beralus mwaka 2020 alivyoua zaid ya raia 200 ili Lukashenko abakie madaraki kwa mwaka wa 27 au huko Kazaskan mwaka 2021 raia wameuawa kwa silaha za msaada kutoka Urusi ili kumlinda Kibaraka wao
Leta pia na ya NATO na wenzie
 
Tatizo la Africa ni sera za ujamaa zilizoharibu uchumi.Nchi ambazo hazikujiingiza kwenye ujamaa kama Botswana, Zimbabwe na Kenya ziliendelea kufanya vizuri kiuchumi.
Turudie tena kuwaambia hawa mazuzu ya kiafrika yatakayojikusanya Washington: sisi raia wa kawaida wa Afrika tushashtuka kitambo. Madhara ya structural adustment programmes (SAPs) ya miaka ya 1980 -1990 tuliyobambikiziwa na hao hao wamarekani tunaanza kuyaona leo. Leo hii vijana wetu wanagraduate mechanical engineering, electronics na Bcom lakini wanaishia kuendesha bajaji na kufungua vibanda vya mpesa kwa sababu viwanda vyetu vya nguo, matairi, betri, vibiriti, generies zetu za pamba, vililazimishwa kufa kwa sababu ya SAPs. Uwezo wetu wa kutengeneza ajira ndani za watoto wetu na vizazi vyetu vijavyo haupo kabisa na tumeishia kuomba omba na kufanya biashara za uchuuzi kwa bidhaa za kuimport.

Kama kuna viongozi wa Afrika wasioweza wasiong'amua tatizo la msingi kuhusu Afrika ni viongozi wajinga tu ndio wataenda kumsikiliza Biden.
 
Tatizo la Africa ni sera za ujamaa zilizoharibu uchumi.Nchi ambazo hazikujiingiza kwenye ujamaa kama Botswana, Zimbabwe na Kenya ziliendelea kufanya vizuri kiuchumi.
Hapa ndipo umuhimu wa elimu kuambatana na maarifa unapoonekana. Elimu itakufundisha kwamba ujamaa ulikuwa mbaya. Maarifa yatakuonyesha kwamba kinacholeta maendeleo ya nchi na watu si falsafa za ujamaa vs ubepari bali ni maono na mipango safi, watu sahihi na matumizi bora ya maliasili za nchi watu husika walizojaaliwa na mwenyezi.

Hivi unajua kuwa Israeli ni nchi ya kijamaa? google "kibutz". Hivi unajua kuwa maendeleo ya wajapan at the core ni spirit ya ujamaa? Msiwe mnasoma propaganda za magharibi -- tumieni
pia critical thinking. Hivi unajua kuwa hata hao tunaowaita mabepari na mabeberu wa magharibi lakini kwenye mipango yao inayofanyika sirini wanautumia ubepari kama strategy lakini spirit ni ya ujamaa? Hivi unajua mitaji iliyoanzisha corporations kubwa kama Microsoft, Facebook, Apple, ni pesa na dhamana kutoka kwa serikali ya Marekani (na serikali ina jicho lake kwenye hizo corporations kuhakikisha maslahi ya Marekani yanalindwa?) Ni nyie tu mnaoaminishwa kwamba ujamaa ni mbaya -- lakini tafsiri pana ya ujamaa maana yake ni Uzalendo, kufanya mambo kwa faida ya nchi na watu wa asili yako.
 
Ninachakiona ni kwamba huelewei hata Ujamaa na Ubepari ni kitu gani.

Unazungumzia sijui falsafa, spirit n.k kama vile unatoa mawaidha.
Hapa ndipo umuhimu wa elimu kuambatana na maarifa unapoonekana. Elimu itakufundisha kwamba ujamaa ulikuwa mbaya. Maarifa yatakuonyesha kwamba kinacholeta maendeleo ya nchi na watu si falsafa za ujamaa vs ubepari bali ni maono na mipango safi, watu sahihi na matumizi bora ya maliasili za nchi watu husika walizojaaliwa na mwenyezi.

Hivi unajua kuwa Israeli ni nchi ya kijamaa? google "kibutz". Hivi unajua kuwa maendeleo ya wajapan at the core ni spirit ya ujamaa? Msiwe mnasoma propaganda za magharibi -- tumieni
pia critical thinking. Hivi unajua kuwa hata hao tunaowaita mabepari na mabeberu wa magharibi lakini kwenye mipango yao inayofanyika sirini wanautumia ubepari kama strategy lakini spirit ni ya ujamaa? Hivi unajua mitaji iliyoanzisha corporations kubwa kama Microsoft, Facebook, Apple, ni pesa na dhamana kutoka kwa serikali ya Marekani (na serikali ina jicho lake kwenye hizo corporations kuhakikisha maslahi ya Marekani yanalindwa?) Ni nyie tu mnaoaminishwa kwamba ujamaa ni mbaya -- lakini tafsiri pana ya ujamaa maana yake ni Uzalendo, kufanya mambo kwa faida ya nchi na watu wa asili yako.
 
ttzo ni viongoz wetu wala sio hao tunaowalaumu kila siku yaan wapambane kuiangusha Afrika waiache China na India zinapiga hatua , afrika ndo makao makuu ya comedy dunian
Eti Afrika ni makao makuu ya comedy duniani😄😄🙌🙌 .daah mkuu umenivunja mbavu , Afrika sijui tumelaaniwa
 
Acha vichekesho, hao magharibi wanatuuzia nini? Magari tunaagiza yaliyotumika Japan, bidhaa nyingi tunatoa China, dawa zinatoka India, sasa sisi ni soko gani la magharibi?
Bana nawe jiongeze kupata tafsiri pana ya soko. Jichunguze hapo ulipo na angalia kuanzia asubuhi hadi jioni maisha yako, unavyokula na unavyovaa. Unajua kuwa ugali unaokula hayo mahindi mbegu zake ni new imported seeds? Wamagharibi kupitia systems zao za FAO na food security tumelazimika kuona mbegu zetu za asili hazifai. Matokeo yake lazima ununue mbegu kila msimu wa kulima, na hadi unavuna lazima uwe umeshanunua bidhaa imported kutoka kwao za kutosha.

Another thing: westerners wameadvance sana kwenye ukoloni wao mamboleo. Hata kama kitu umenunua kutoka China au Singapore lakini mwenye kiwanda na mtaji unaweza kukuta ultimately ni mmagharibi, na hapo sijaingiza "soft-products" kibao unazowalipa bila kujijua. Nyie kwenu mnahesabu kwamba ni maendeleo but mimi shida yangu ni namna ambavyo uwezo wetu wa kuingia katika hii system ya uchumi kama washiriki wazalishaji usivyokuwepo kabisa. We are reduced ti being mere consumers of imported technology, goods, service, etc. Na pale "tunapowauzia" tunawauzia mali ghafi mfano madini wanachimba na kuchenjulia nje huku watoto wetu wanaosoma mining processing kubakia kusoma theory and no real application. Yaani ni sheedah tupu. Fungukeni wajamenim
 
Tatizo la Africa ni sera za ujamaa zilizoharibu uchumi.Nchi ambazo hazikujiingiza kwenye ujamaa kama Botswana, Zimbabwe na Kenya ziliendelea kufanya vizuri kiuchumi.
Kenya, Zimbabwe njaa , rushwa , uchumi mbovu , madeni ya kutosha kutoka china [ wajamaa ] nao hawa ni wakutolea mfano. Afrika imeoza kote tena hasa hasa Kusini mwa jangwa la sahara.
 
20 July 2022
Washington DC

TAARIFA YA KIKAO KIJACHO CHA RAIS BIDEN NA VIONGOZI WA AFRIKA / US - AFRICA SUMMIT 2022

Rais Joe Biden awaalika Viongozi wa Afrika kwa Majadiliano Washington

Taarifa ya Ikulu ya Marekani maarufu kama White House imetolewa kuelezea mwaliko wa Rais wa Marekani kwa viongozi wa mataifa ya Afrika, wakutane kujadiliana mjini Washington kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea duniani.

Masuala hayo ni kama ya usalama wa chakula / food security, Covid-19, ulinzi wa amani, demokrasia pia haki za binadamu, nafasi ya sekta binafsi za kibiashara n.k ambayo yamesababisha chumi nyingi za dunia kuyumba huku bara la Afrika lilikabiliwa vibaya zaidi na changamoto ya uchumi kuyumba na gharama za maisha kupaa.

Mkutano huo wa Rais Joe Biden na viongozi utafanyika December 13 -15 2022 jijini Washington na kutumika pia kuimarisha mahusiano yaliyopo ktk ya nchi za Afrika na nchi ya Marekani.

Statement by President Biden on the U.S.-Africa Leaders Summit​

JULY 20, 2022SPEECHES AND REMARKS
I look forward to hosting leaders from across the African continent in Washington, DC on December 13-15, 2022, for the U.S.-Africa Leaders Summit. The Summit will demonstrate the United States’ enduring commitment to Africa, and will underscore the importance of U.S.-Africa relations and increased cooperation on shared global priorities.
The U.S.-Africa Leaders Summit will build on our shared values to better foster new economic engagement; reinforce the U.S.-Africa commitment to democracy and human rights; mitigate the impact of COVID-19 and of future pandemics; work collaboratively to strengthen regional and global health; promote food security; advance peace and security; respond to the climate crisis; and amplify diaspora ties.
I look forward to working with African governments, civil society, diaspora communities across the United States, and the private sector to continue strengthening our shared vision for the future of U.S.-Africa relations

Source : Statement by President Biden on the U.S.-Africa Leaders Summit | The White House
Hamna kitu hapo ni utapeli mtupu.
 
US /Africa,Russia/Africa,,France/Africa,China/Africa,Japan/Africa. Kila nchi tajiri inatuvuta. Jamani watuwache sasa. Halafu hii dharau. Yeye si ndo angekuja Africa ?Au anaogopa mbu ?
 
Tatizo la Africa ni sera za ujamaa zilizoharibu uchumi.Nchi ambazo hazikujiingiza kwenye ujamaa kama Botswana, Zimbabwe na Kenya ziliendelea kufanya vizuri kiuchumi.
Mbona hizo sera za ujamaa hazijaharibu uchumi wa China. tatizo sisi waafrika [ watu weusi ] tuna matatizo Sana kwenye bongo zetu.
 
Bana nawe jiongeze kupata tafsiri pana ya soko. Jichunguze hapo ulipo na angalia kuanzia asubuhi hadi jioni maisha yako, unavyokula na unavyovaa. Unajua kuwa ugali unaokula hayo mahindi mbegu zake ni new imported seeds? Wamagharibi kupitia systems zao za FAO na food security tumelazimika kuona mbegu zetu za asili hazifai. Matokeo yake lazima ununue mbegu kila msimu wa kulima, na hadi unavuna lazima uwe umeshanunua bidhaa imported kutoka kwao za kutosha.

Another thing: westerners wameadvance sana kwenye ukoloni wao mamboleo. Hata kama kitu umenunua kutoka China au Singapore lakini mwenye kiwanda na mtaji unaweza kukuta ultimately ni mmagharibi, na hapo sijaingiza "soft-products" kibao unazowalipa bila kujijua. Nyie kwenu mnahesabu kwamba ni maendeleo but mimi shida yangu ni namna ambavyo uwezo wetu wa kuingia katika hii system ya uchumi kama washiriki wazalishaji usivyokuwepo kabisa. We are reduced ti being mere consumers of imported technology, goods, service, etc. Na pale "tunapowauzia" tunawauzia mali ghafi mfano madini wanachimba na kuchenjulia nje huku watoto wetu wanaosoma mining processing kubakia kusoma theory and no real application. Yaani ni sheedah tupu. Fungukeni wajamenim


Hizo mbegu za mahindi ndiyo zinatoka Marekani? Hebu lete ushahidi kama ni kweli.

Bidhaa za westerners zinazozalishwa China kwa mfano Nike sisi hatuzimudu. Tunanunua feki ambazo Wachina wenyewe wametengeneza. Sasa Mmarekani anapata faida gani sisi tukinunua Nike feki au Iphone feki?
 
Zimbabwe ilikuwa ni nchi yenye uchumi mzuri, inayozalisha na kuuza chakula na bidhaa za viwandani kwa wingi nje mpaka pale Mugabe alipoanzisha vurugu zake za mashamba na ubabe wa kisiasa.

Kenya ni nchi yenye uchumi mkubwa na mzuri kuliko nchi zote za Africa Mashariki pamoja na migogoro ya kisiasa waliyoipitia kwa muda mrefu sana.

Nchi karibia zote duniani zinakopa na zina Rushwa, hata huko China Rushwa ipo sana tu.
Kenya, Zimbabwe njaa , rushwa , uchumi mbovu , madeni ya kutosha kutoka china [ wajamaa ] nao hawa ni wakutolea mfano. Afrika imeoza kote tena hasa hasa Kusini mwa jangwa la sahara.
 
Back
Top Bottom