Rais Magufuli anahoji; Je, ninyi hamuamini kuwa yupo Mungu?

Rais Magufuli anahoji; Je, ninyi hamuamini kuwa yupo Mungu?

Mhe. Rais naona ameumaliza mzizi wa fitina leo katika mazishi ya Balozi Kijazi na kusema kuwa magonjwa yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo, na sisi si pekee ndiyo tunaotaabika na matatizo haya ya magonjwa ya milipuko hata nchi zingine wamekufa wengi sana. Na tatizo linapokuwa kubwa kuzidi uwezo wa binadamu tulisogeze kwa Mungu.

Rais anasema mwaka jana tulimuona Mungu akitusaidia lakini sasa naona wengine hawana imani tena wanatengeneza taharuki na kutishana mimi sifanyi lokudauni tuchape kazi Mungu yupo. Kwanini au amwamini kuwa Mungu anaweza kuishinda Korona?

Mimi mtoto wa mchungaji nahoji hivi hawa baadhi ya viongozi wa dini ambao nao pia wanaogopa Corona kiasi cha kwamba wanatushauri tuwasikilize watu wa afya na wamitandaoni hivyi hawa watumishi wa Mungu si wangeacha hiyo kazi na kuja huku mchangani ijulikane moja.

Nawauliza na ninyi wana janvi Mungu yupo au, maana babuzetu waliomba mvua zilinyesha, waliomba nzige waondoke asubui waliwakuta chali kificha mende, magonjwa ya mlipuko hayakuwagusa, hivi na yule Mungu wa babu zetu yupo wapi siku hizi na huyu wa kanisani na msikitini yupo wapi.
Mkuu umeuliza swali zuri, but omba mungu huku pia ikitumika mahalifa aliyokupa kujua hema na baya, mfano umepimwa umekutwa, typhoid, dawa zipo , na hutaki kunywa, alafu sema mungu tuone Kama hautazikwa,
Hoja hapa serikali pitia wizara ya afya , KWA kushirikiana na Tamisemi, lazima kuja na sheria ya mpito KWA ajili ya kujikinga na CORONA, maji tiririka kila mahali kila kaya , barakoa iwe lazima huna na unatembea mjini piga fain, mikusanyiko isiyo ya lazima piga chini,
Tutaweza vuka, ila kusema kwamba corona ya kwanza wenzetu walikufa Sana , ni sawa ila sio kigezo tusichukue hatua ,mpaka nasi yatukute, mdudu , huyu ana mutate kila wakati, hakuna sababu ya kusubili,
I wish , ningekua katibu mkuu, waziri or naibu , Ningeamuka hasubuhi natangaza mikakati tajwa hapo juu, wakati huo nikiwa na barua ya kujiuzuru , au kutumbuliwa mda huohuo!
 
Mhe. Rais naona ameumaliza mzizi wa fitina leo katika mazishi ya Balozi Kijazi na kusema kuwa magonjwa yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo, na sisi si pekee ndiyo tunaotaabika na matatizo haya ya magonjwa ya milipuko hata nchi zingine wamekufa wengi sana. Na tatizo linapokuwa kubwa kuzidi uwezo wa binadamu tulisogeze kwa Mungu.

Rais anasema mwaka jana tulimuona Mungu akitusaidia lakini sasa naona wengine hawana imani tena wanatengeneza taharuki na kutishana mimi sifanyi lokudauni tuchape kazi Mungu yupo. Kwanini au amwamini kuwa Mungu anaweza kuishinda Korona?

Mimi mtoto wa mchungaji nahoji hivi hawa baadhi ya viongozi wa dini ambao nao pia wanaogopa Corona kiasi cha kwamba wanatushauri tuwasikilize watu wa afya na wamitandaoni hivyi hawa watumishi wa Mungu si wangeacha hiyo kazi na kuja huku mchangani ijulikane moja.

Nawauliza na ninyi wana janvi Mungu yupo au, maana babuzetu waliomba mvua zilinyesha, waliomba nzige waondoke asubui waliwakuta chali kificha mende, magonjwa ya mlipuko hayakuwagusa, hivi na yule Mungu wa babu zetu yupo wapi siku hizi na huyu wa kanisani na msikitini yupo wapi.

Huu ujinga umeongea hapa ndio Kinjeketile aliwaaminisha waafrika kuwa mizinga ya wazungu itageuka maji, baada ya ujinga huo kuwaingia watu waliipata fresh. Mwaka jana Corona haiukuondoka kwa maombi, bali haikuenea vizuri na serikali iligoma kutoa taarifa za ugonjwa.
 
Kama ana itikadi Kali hivyo kama wasabato walokwenda airport Mungu awapeleke (sijui ulaya?) Haspitali zinajengwa za nini?
 
Chanjo, barakoa, kukaa mbalimbali
 
Wenye akili km zako hawapaswi kuwa JF kwa hakika. Inasikitisha kuona wapo watu humu wenye akili finyu za kusubiri rais aseme ndio ajue tatizo lipo au la na achukue hatua. Idiot!

Corona si tatizo la kumwita Mungu, ni tatizo la kupambana nalo kwa maarifa aliyotupa Mungu. Kimsingi Magu anashindwa kumeza maneno yake ya kujigamba, hawezi. Lakini cha ajabu hata sisi hatutaki kujikinga tunasubiri et rais aseme "chukueni tahadhari". Ujinga.

Ebola haikutoka kwa maombi, polio, surua, ndui n.k havikuisha kwa maombi. Jiue kwa ujinga wako km hao wapuuzi wanaoendelea kukusanyika misibani bila kuvaa hata barakoa.
Naaminii kuna mahali Watanzania hatujaelewana hasa katika awamu hii ambayo watu wamejaa hofu ya kugopa watawala!!
Tumeshaona madhara ya lockdown na kwa umaskini wetu na kutokuwa na takwimu sawasawa kuweka lockdown ni kuua watu.
Rais amekazania lockdown lakini hatuhitaji lockdown ila tunahitaji kauli yake "from horse's mouth" juu ya uwepo wa covid 19 na uwepo wa kirusi kipya na kibaya zaidi.
Kauli hiyo ya Raisi itabadilisha nguvu na mwelekeo wa mapambano dhidi ya ugonjwa huu.Kutokupata maelezo toka kwa Mkuu wa nchi kunaleta mkanganyiko na ndipo "wanafiki" wanapopatia pa kujikweza.
Kila binadamu anajua kufa kupo lakini kwa nini ubanwe na pumzi siku tano ndio ufe kwa ugonjwa ambao ungeweza kujikinga nao?
Binafsi naamini Mwenyezi Mungu akimpa ujasiri na akatamka hadharani ataokoa wengi na muda wa ugonjwa kwa nchi yetu utakuwa mfupi,Inshallah!
 
Hapa unapotosha mkuu.si dhani kama kuna kum jaribu Mungu hapa.Tunaambiwa tuendelee kuchukua tahadhari ila tusiache kumuomba Mungu.
Endeleeni tu kutetea upumbavu! Unasema vipi kwamba tuchukue tahadhali wakati mwenyewe huoneshi kwamba unachukua tahadhali?! Yaani kilichooneshwa kwenye ile shughuli ya kuaga kwako wewe ndo kuchukua tahadhali wakati rais na viongozi wakuu wote hata barakoa hawajavaa? Hivi unamwambia mwanao acha ulevu wakati mwenyewe kila siku unarudi ukiwa tilalila?!
 
Kama ndio hivyo muheshimiwa rais tugeuze shule zote na vyuo kuwa nyumba za ibada.

Haina maana tena kwenda shule kupata elimu ya kukabiliana na matatizo kama haya kwani Mungu yupo na ukiomba chochote atakupa bila jitahada zozote.

Hizi tiba zote na dawa zinazo patikana ni kutoka kwa shetani sio? Sio kwamba Mungu katupa elimu ?

Mh Rais hakuna mtu anataka ufanye lockdown, tulicho kuomba ni kubali ugonjwa upo, waambie wananchi wote wajikinge(barakoa lazima) tuepuke na mikusanyiko mikubwa, serikali iongeze misadaa kwenye hospitali zote hili waweze kuwahudumia wagonjwa wengi zaidi.

Sio kwamba hatumuamini Mungu, hapana, tunachukua tahadhali zote na kumuomba Mungu. Sio unaingia kwenye pango la nyoka alafu unamuomba Mungu akulinde; Mungu kashakupa akili ya kujua hatari na salama. Mungu anataka utumie akili pamoja na dua , sio dua peke yake.

Basi Mh. Rais naomba endelea na dua zako lakini sasa tumia na akili/elimu yako aliekupa Mungu kukabiliana na hili swala.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Nimeona leo kwenye mitindao muheshimiwa Sana ,mtukigu Rais anatuamasiha waumini wa dini za kikristo,kiislamu na kisabato tusali na kufunga na kwamba tumtegemee MUNGU tu

Je ,ana hofu na Nini?

Tuko uchumi wa Kati kwani shida iko wapi?

Mbona kila siku tunaenda kwenye nyumba zaidi iweje leo kwenye kuaga mwili wa kijazi asisitize Sana hivyo ana hofu gani?

Tuendelee kupiga nyonga[emoji1]
View attachment 1706217
Mods umeunganisha Uzi

Acheni hizo nyie

Mna vijiba vya roho
 
Mad president!Mungu huwa halipi maombi bali huwa analipa jitihada.Kama unamuomba Mungu bila ya kuwa na strategic plan nzuri pamoja na vitendo madhubuti vya kupambana na janga huko ni kumkejeli Mungu!
 
Wenye akili km zako hawapaswi kuwa JF kwa hakika. Inasikitisha kuona wapo watu humu wenye akili finyu za kusubiri rais aseme ndio ajue tatizo lipo au la na achukue hatua. Idiot!

Corona si tatizo la kumwita Mungu, ni tatizo la kupambana nalo kwa maarifa aliyotupa Mungu. Kimsingi Magu anashindwa kumeza maneno yake ya kujigamba, hawezi. Lakini cha ajabu hata sisi hatutaki kujikinga tunasubiri et rais aseme "chukueni tahadhari". Ujinga.

Ebola haikutoka kwa maombi, polio, surua, ndui n.k havikuisha kwa maombi. Jiue kwa ujinga wako km hao wapuuzi wanaoendelea kukusanyika misibani bila kuvaa hata barakoa.
Tatizo hii Ni Africa, ingekuwa kwenye nchi zilizostaarabika ambacho angefanya Jiwe ili kuitunza heshima na ushujaa wake (Kama anavyo anyway) Ni kujiuzulu...Nyerere alipojikuta kwenye Hali Kama hii hakujiuzulu tu Bali aling'atuka kabisa na ndiyo maana Hadi leo Watanzania tulio wengi tunamheshim na kumpenda pamoja na madhaifu yake ya ki ubinadam
 
Mzee nadhani anakosea sana kutia shaka imani za watu. Mungu yupo na tunamshukuru kwa kila kitu. Ila Mungu katupa maarifa binadamu yeye anatoa rizki lakini ni yeye anataka wafanye kazi ndio anatoa. Unapokuwa na mgonjwa unatumia kila ulichonacho kumtibu lakini pia unamuomba Mungu haya mambo yanaenda pamoja, unajisaidia na Mungu anakusaidia. huwezi kupona kwa miujiza tumepewa maarifa na Mungu tutumie. Ningemuelewa kama angesema ugonjwa hatari kuwashukuru wafanyakazi wa afya kwa kufanya kazi katika mazingira magumu na hatua gani za kuchukuwa kama serikali kusaidia, hakuna mtu amesema anataka lockdwon ila yako mambo yakufanya halafu baada ya jitihada zetu kwa uwezo wetu tumuombe Mungu atusaidie katika juhudi zetu, Mungu wa dunia sio wa Tanzania tu. enzi za mikate kushushwa toka mbinguni hakuna jitahidi, omba na Mungu huwa saidia wenye kujisaidia.
 
Dr Mpango Mungu amsaidie ainuke na wagonjwa wengine wote, mzee leo kasema katumiwa msg na Dr mpango lakini wakati huohuo kasema Dr mpango kapata salamu za mzee kupitia kwa mke wake hapa inakujulisha hali ilikuwa ni mbaya kiasi salamu zinapitia kwa mtu lakini majibu kwa mwenyewe kuna mashaka na hili. Kikubwa tumuombee apone na wengine wote. Huyu waziri kabla ya kupotea aliwaonya wafanyakazi wa wizara yake wajilinde alikuwa kishaona dalili labda. shida yangu kwanini mpaka watu wazushe uwongo ndio manakuja kukana hadharani? mambo kama haya mkiyaweka tu hadharani hata wale waongo watakuwa hawana jipya. kuna mawaziri wengi leo hawakuwepo watu wataanza kuongelea hata Ndungai leo kaingia mitini sijamuona na mzee kabudi kama sikumuona hivi.
 
Hujui chochote wewe
Mjuze na sisi tujue ili matendo ambayo tunaona Mungu hahusiki, tupate kujua kua ALIHUSIKA.

Mfano: Kupigwa risasi TAML, kupotea kwa Saa8 na mengine mengi ambayo mimi nawewe tunayajua.
 
Tuna muomba MUNGU lakini pia lazima tuchukue tahadhari maana hata MUNGU alisema jisaidie nitakusaidia
Hilo sijawahi kusoma popote kwenye maandiko labda uniambie imeandikwa wapi mkuu
 
Tatizo sio Mungu hayupo ila tunaomba atangaze hadharani kua C19 ipo ili tahadhari zianze kuchukuliwa.

[emoji40] [emoji40][emoji40][emoji40][emoji40][emoji40][emoji40][emoji40]
kweni alisha sema kua haipo?

wabongo bwana.
 
BAVICHA HILI KWAO CHUNGU.HAPO WALIPO WANATAMANI MODS WAUFUTE HUU UZIII. KATIKA RAIS AMBAE ATAKUMBUKWA KWA KUWA NA MAONO AMBAYO ILI UYAELEWE UNATAKIWA UWE NA THE WISDOM ABOVE NORMAL ni huyu jpm.I salute you!!!!
Akumbukwe kwa lipi au kwa nchi kuirudiaha kwenye umasikini? Yaani wewe duniani huyo ndoo unamuona raisi bora? Kweli una matatizo ndugu yangu.
 
Nafurahi sana napomuona Rais wangu akiijua sana dini kuliko watu wote duniani (ukimtoa Askofu Rasheed) Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko hata Watumishi wa Mungu! Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko wale waliotuletea habari za Mungu! Yaani Rais wangu mpendwa anamjua sana Mungu kuliko hata Bible inayosema "Imeandikwa pia, usimjaribu Mungu wako"!

Hivi anamuona Bwana Yesu ni zuzu aliyemgomea shetani kujitupa chini kutoka juu ya mnara, au Rais wangu anafikiria nini hasa? Mbona Yesu hakujitupa pamoja na bible kusema Mungu atawaamuru malaika wake watamchukua mikononi mwao ili asijikwae?
Daa Bro Asante hhhh
 
Back
Top Bottom