Rais Samia aagiza kuandaliwe Kanuni za Mikutano ya Vyama vya Siasa Nchini

Rais Samia aagiza kuandaliwe Kanuni za Mikutano ya Vyama vya Siasa Nchini

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kwa kushirikiana na Tanganyika Law Society (TLS) pamoja na Zanzibar Law Society (ZLS) ameagizwa kuandaa kanuni zitakazoelekeza namna ya kufanya mikutano ya hadhara ya Vyama vya Siasa.

Rais Samia ameelekeza hayo baada va kupokea maazimio ya awali ya Kikosi kazi kilichoteuliwa kufuatilia hoja zilizojitokeza katika mkutano wa wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa uliofanyika Desemba 2021.

Maazimio yamegawanyika katika makundi matatu ya muda wa utekelezaji; Azimio la muda mfupi ni uandaaji wa Kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya Mikutano ya Hadhara. Miongoni mwa maazimio ya muda wa kati ni Rushwa na Maadili katika Uchaguzi. Katiba mpya ni mpango wa muda mrefu.

F555768F-D6E1-4B2D-A864-3B3205759A7F.jpeg
 
#HABARI Rais @SuluhuSamia amemwagiza Waziri wa Katiba na Sheria George Simbachawene, kuandaa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.
 
Ukishawapa Wanasiasa wanachotaka, kelele zote zinaisha.

Unaweza kufikiri nchi hii matatizo yote YAMEISHA😀😀😀
 
Bado anatokea mmakonde mmoja na kusema wanawake ni viumbe dhaifu, wakati kila mianaume ya upinzani inaitwa ikulu na huko kwa mabeberu kisha inainamishwa vichwa kwa sauti laini inakuwa miimba mapambio.

Hata Samson na miguvu yake aliwezwa na mwanamke mmoja tu legevu legevu kimuonekano, the same kwa Zitto, Mbowe na Lissu.

Maendeleo hayana chama
 
Green Light to Democracy
Huyu mama SSH aombewe sana. Akikomaa na hizo ajenda zake kuhusu demokrasia ataiacha Tanzania kwenye njia nzuri.

Wenye asili ya Pwani wana weledi mkubwa sana kuhusu maisha jumuishi.
 
Rais wetu mwacheni
Pia huu ni wakati wao
Sisi tulishindwa wao wanaweza
Tutulie
 
Back
Top Bottom