Rais Samia akubali ongezeko la asilimia 23.3 kwa kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma

Rais Samia akubali ongezeko la asilimia 23.3 kwa kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma

Hongera Sana Mheshimiwa Raisi,unaupiga mwingi,unatekeleza Miradi ya Maendeleo na kuangalia masilahi ya watumishi.
Hongera Sana mama, wewe hujasubiri Miradi ikamilike ndiyo upandishe mishahara.
Mama Wastaafu hujawasahau,umeridhia kikokotoo kilichopendekezwa na tucta wakati wa Mei mosi 2022.

Utekelezaji

1.Watumishi wa Serikali kada ya operation na mikataba walikuwa wanachangia mfuko wa NSSF,na NSSF wao walisha-adopt kikokotoa cha 25% kinyemela kabla watumishi wa Serikali wanaochangia PSSSF kugomea kikokotoa cha 25%' kwa malipo ya mkupuo mmoja.
2.watumishi wa Serikali waliolipwa wanaochangia PSPF wamekuwa wanalipwa malipo ya mkupuo ya asilimia 50.

Ushauri
1. Kikokotoo Cha asilimia 33 kitumike kwa watumishi wote wa Serikali regardless ulichangia mfuko gani
2.Kwa watumishi wa Serikali waliolipwa 25 mfuko wa NSSF iwalipe tofauti.
3.kama ikikupendeza watumishi wa sekta binafsi na Serikali wawe wanalipwa kwa kikokotoo kimoja kwa mifuko yote miwili.
 
Ni kwasababu tu ya ubinafsi wake,na roho mbaya. Hakuna mtu haitaji masilahi juu ya shughuli yake anayoifanya.

Wafanyakazi wakiongezewa mshahara ni moja ya kuingiza pesa kwenye mzunguko.
Mkulima naye anapigania masilahi ya kazi zake za shambani na Kila mtu anaunga mkono iweje Kwa watumishi?

Magu ameacha kizazi Cha roho mbaya Sana.
Kilio cha kila siku cha mkulima kuhusu mbolea kuuzwa kwa bei kubwa kupindukia unakitafakarije? Kumbuka wakulima no 98% yai watanzania.
 
Kuongeza mishahara aitatusaidia hali kuna bidhaa ambazo ni muhimu kila kukicha zinapanda bei na sio watanzania wote ni wafanyakazi . Mimi nafikiri jambo la msingi ni kuwapa unafuu wananchi katika bidhaa muhimu wanazotumia kila siku. Wanaokula keki ya taifa ndio wanaozidi kufaidi hali mtu asie na kazi anaumizwa ktk bidhaaa
Kama hujui kwa gharama za Maisha za leo ili mtumishi amudu Maisha inabidi kima cha chini kiwe millioni moja
 
Bila kubisha andiko lina utata mkubwa.

Hapo hakukuwa na ulazima wa kutaja kauli ya
"ikiwemo kima cha chini"

Kama wengine walivyotangaza kuwa ongezeko ni kwa asilimia kadhaa. Hapo kila mtu ngeelewa kiasi atakacho ongezewa.

Kutaja kima cha chini pekee kunaweza kukuta watu wanaongezeana mishahara kwa kupendeleana tu na wengine wakaongezwa kidogo sana na huna pa kuanzia kudai.

Kwa mfano wewe sio wa kima cha chini ukikuta unaongezeko la asilimia tano utaanzia wapi kudai kuwa umepunjwa ?

Hii nchi ni bora tuanze kuona namna ya kujiongezea vipato kwa kuangalia kazi nje ya kazi rasmi.
Hapo watu hawajui tu! Hiyo 23% ni political issue ili kuwazubaisha wengine hapo kwa watu wa kima cha chini ni habari njema kwao! Waseme kwa uwazi ongezeko kwa wengine ni asilimia ngapi! Tofauti na hapo tutakuta ongezeko 17,000/=
 
Tafsiri yake ni kwamba Rais ameongeza 23.3% kwenye kima cha chini cha mshahara Kama kilikuwa (mathalan) 100,000 23.3% ni 23,300 i.e 123,300/-
 
Hongera kwa Rais Samia Suluhu Hassani kwa kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kiwango bora sana. Hakika mama umeupiga mwingi. Miaka mitano mingine tunakukabidhi👋🤗🇹🇿
Screenshot_20220514-155018_WPS Office.jpg
 
Huyo hajaelewa! Hapo hawajaongeza mshahara kwa asilimia 23.3%! Serikali imekubali ongezeko la mshahara kwa 23.3% kwa kila cha chini! Maana yake kwamba kama kila cha chini kilikuwa lakini mbili(200,00) inamaa itaongeza 23.3% kwa kimya hicho cha chini na kuwa kama 238,000/,=kwa maana hiyo 38,000/= ndo ongezeko kwa nagzi hiyo ya chini si kwa ngazi nyingine! Sio kuwa mshahara umepanda kwa asilimia 23.3% kwa wafanya kazi wote hapana!
Elimu yako ni level gani?
Mada nyingine sio za kuchangia wala ugoro na double kick
 
Tafsiri yake ni kwamba Rais ameongeza 23.3% kwenye kima cha chini cha mshahara Kama kilikuwa (mathalan) 100,000 23.3% ni 23,300 i.e 123,300/-
Kima cha chini kwa watumishi wa umma ni 300000

Hata kenya nyongeza inapimwa kwa kima cha chini

Watumishi wote wanaongezwa mshahara
 
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akubali ongezeko la 23.3% kwa kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma.

View attachment 2224213View attachment 2224214

Rais Samia badala ya mtumishi kustaafu na kulipwa mafao yake kwa mkupuo sasa wanalipwa 33% na awali ilitakiwa kulipwa 25% . Watumishi hili mmelisoma au mmeambiwa 23.3% ya kina cha chini kilichoongezwa? Mkafurahia​

 
Hebu ngoja hapa:-
23.3/100=0.233
0.233×270000/= =62,910
KWA hiyo:-
270000+62910=332,910/=
KWA kima cha CHINI hicho!!
Nakaribisha masahihisho kama yapo!!
Mimi Raisi ajaye nimeona hivi KWA lima cha CHINI ya wewe je!!?
Meaning kila mtumishi ataongrzewa 62,910
 
Je wewe ni mtumishi wa serikali? Maana kuongeza asilimia za mshahara kwa kima cha chini hakujaanza mwaka huu.
Kumbuka hata kwenye kodi ilipunguzwa kwa wenye kima cha chini ikawa asilimia 8 kwa wenye kima vha chini kama sijakosea wakati ambao hawapo kwenye kima cha chini wanalipa zaidi ya hapo.
Hivyo wanapotumia kima cha chini wana sababu zao za kimahesabu. Hii 23% sio flat rate na utakuja kukiri mwenye hapa.
Kubisha mie siwezi.
Upo sahihi jinsi mshahara unavyokuwa
mkubwa ongezeko linapungua...Kuna watu wataambulia elfu kumi kama kwenye lile punguzo la Kodi
 
Ni kweli huna, sio ww tu karibu walimu wote hamna.
Kusoma tu hiyo document na kuelewa umeshindwa

Unatoa wapi uhalali na ujasiri wa kudharau, kukejeli na kutweza waalimu au watu mnaopishana nao uelewa?

Mie nilichoelewa kwenye hiyo taarifa, kama kichwa Cha habari kilivyo na paragraph ya kwanza, ni kwamba, Rais ameridhia ongezeko la mishahara Kwa wafanyakazi wote wa umma ( hajataja asilimia ngapi), ameweka wazi kwamba wale wa kima Cha chini ndio ongezeko lao la mshahara ni asilimia 23.3%.

Mbona na wewe unasema nyongeza ni Kwa kima Cha chini pekee lakini haujaitwa hauna akili?

Kutokuelewa jambo inaweza kuwa ujinga Kwa Mara Moja lakini sio kukosa akili.
 
Tena siyo EAC tu, nadhani ni zaidi ya EAC. Ghana walikua juu, nadhani walikua 17%. Lakini mkuu, hii ni kwa sababu watu wamekaa 6+ bila ongezeko. Hizo nchi zingine walikua wakiongezewa. Hii ndiyo madhara ya kukaa miaka mingi bila kuongeza mishahara. Kwa hiyo hii 23% inaweza isiwe na impact kubwa ukilinganisha na nchi zingine za EAC ambazo wameongezewa mara kwa mara. Kenya wameongezewa 12% safari hii.
Hivi ni kweli hamjui kusoma?
 
Back
Top Bottom