Rais Samia amkabidhi nyumba Rais Mstaafu Kikwete
Huyo ndiye kaijenga.

Rejea salamu za Jk msibani.

Alitakuwa akabidhiwe siku nyingi
Watu wengine wanadandia tu topic kumshambulia Mama na kuna ziara alifanya JPM katika nyumba hii alikuwa na JK na akawaambia wale contractor wamalize nyumba haraka wanachelewesha.
 
Wanagawiana utajiri wa nchi hii kama Njugu.

Kikwete mwenye Lijumba lote lile Msoga ana shida gani ya nyumba?

Wanajitungia misheria ya kulipana mibenefits ya kufuru halafu tukiwauliza wanajitetea kwa sheria hizohizo!

Hiyo nyumba wala hajajengewa Kikwete bali ni urithi wa Riziwani, Miraji, Salama, Mama Salma na watoto wa Kikwete.

Mambo mengine ya nchi hii yanatia kinyaa ajabu.
Vipaumbele vya watawala wetu ni watawala wenyewe na sio masikini.
As if kazi tunazofanya sisi hohe hahe hatulitumikii taifa ila wao tu
Mshahara mkubwa vile na bado unapewa zawadi ila mwenye mshahara kidogo ajiandae na uzee kwa namna yake mwenyewe.
Kuna haja hii katiba ikaangaliwa upya,tuweke msisitizo kwenye hili.
 
Safi kabisa ,huku ajira , nyongeza ya mishahara mwaka Kesho , vutia wawekezaji , mambo ya madege tupa kule , Nani anafaidika na madege au napata sifa gan ujinga Sana tulilishwa
Ujinga hukulishwa, ila ww ni mjinga
 
Msimtafutie sababu Mama hizi sheria kazitunga mwenyewe JPM wakati wake na alishamkabidhi Mwinyi na Mkapa ya Kikwete alikuwa amkabidhi wiki 2 kabla hajafariki hapa anatimiza haki za kisheria. Suala la sheria mbaya au nzuri hilo ni jambo lingine lakini zote zilipishwa bungeni tena kwa makofi na sisi tukawapa tena 99% mwaka jana. hakuna kulalamika kazi iendelee.
Sasa alielalamika ni nani jamaa! Mie naona kazi iendelee tu
 
Wanagawiana utajiri wa nchi hii kama Njugu.

Kikwete mwenye Lijumba lote lile Msoga ana shida gani ya nyumba?

Wanajitungia misheria ya kulipana mibenefits ya kufuru halafu tukiwauliza wanajitetea kwa sheria hizohizo!

Hiyo nyumba wala hajajengewa Kikwete bali ni urithi wa Riziwani, Miraji, Salama, Mama Salma na watoto wa Kikwete.

Mambo mengine ya nchi hii yanatia kinyaa ajabu.
Tulia wewe! Mama anawakomesha mataga
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemkabidhi nyumba ya kuishi Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete iliyojengwa katika Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar es Salaam.

Nyumba hiyo imejengwa na Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ikiwa ni utekelezaji wa kifungu namba 12 cha Sheria ya mafao ya hitimisho la kazi kwa viongozi wa siasa, sura ya 225 na marejeo ya mwaka 2020 ambayo pamoja na stahili zingine za matunzo ya viongozi wakuu wastaafu inaelekeza kuwa Rais anayestaafu anastahili kujengewa nyumba ya kuishi yenye hadhi ya Rais.
Me nilidhani ile ya Mwl Nyerere ilijengwa na JWTZ kwa askari wake kujitolea kukatwa sehemu ya mishahara yao?
I stand to be corrected

View attachment 1778685

Je, ni lini sheria zitarekebishwa ili kila mstaafu ajengewe nyumba yenye hadhi ya kazi yake aliyokuwa anafanya?
 
Back
Top Bottom