Rais Samia amteua Jacob John Mkunda kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF)

Rais Samia amteua Jacob John Mkunda kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF)

Hakuna mwenye military CV Tanzania. Mara ya mwisho tumekuwa na military project was 1979, kizazi cha viongozi wa kijeshi wa leo walikuwa chekechekea.

Venance Mabeyo kwenye exit interview kaulizwa, nini vilikuwa vizingiti, mabalaa na changamoto kubwa kuliko zote ulizozipitia katika military carrer yako ???

Mabeyo akasema mafuriko na kifo cha Magufuli!

Disastrously embarrasing response, but it was the truth.

Sembuse huyu mteule wa leo ambaye hakuna aliyewahi kumsikia.
 
Karushwa viwili
Nimeambiwa kuwa kijeshi ni swala la kawaida,, Amiri jeshi mkuu anaweza kukupandisha vyeo kadri atakavyoona yeye ni sawa,,,,na CDF pia ana uwezo huo...

so Lipo sawa kwa taratibu za Jeshi.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda kuwa Jenerali, na amemteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF).

Kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo katika Makao Makuu ya Jeshi.

====

RAIS, Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda kuwa Jenerali na amemteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (Chief of Defence Forces – CDF).

Kabla ya Uteuzi huo, Mkunda alikuwa Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo katika Makao Makuu ya Jeshi (Chief of Operations and Training).

Rais Samia pia amempandisha Cheo Meja Jenerali Salum Haji Othman kuwa Luteni Jenerali na amemteua kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (Chief of Staff – C of S).

Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Othman alikuwa Kamishna wa Utafiti na Maendeleo Jeshini (Commissioner for Research and Military Development) katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Vile vile amemteua Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule kuwa Balozi ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Uapisho utafanyika tarehe 30/06/2022 saa saba mchana Ikulu, jijini Dar es Salaam.

View attachment 2276626

View attachment 2276683
Picha: Meja Jenerali Jacob John Mkunda
Watu hawana masihara na ugali wao panda kwenye gari sit, nyingi ila utaishia kusimama kutoka mwanzo wa safari Hadi mwisho wa safari.
 
Ule uzi wa utabiri wa nani atakuwa CDF mpya umemuharibia sana Luteni Jenerali Mkingule hana hu na ule uzi
 
Niliposoma ulichoandika hapa nilikuwa bado sijaangalia jina.
Nashangaa kidogo, lakini nimeanza kuzoea tabia hizi za kiTanzania zinazobadilika kila mara. Hazitabiriki.

Sasa uliyoandika hapo, sijui kama utayakumbuka baada ya miaka miwili mitatu ijayo!

Ningekuwa na uwezo ningeyaweka kwenye paji la uso wako kama lebo, ili usithubutu kusahau ulichoandika hapa.

Na ili usinione mimi kama ninakuonea, hebu jikumbushe habari zako juu ya Lissu, miaka michache iliyopita.
Hiyo error katika kutoa pasi na unapogundua umekosea unaurudisha mpira nyuma kidogo au unaendelea mbele.

Karata hazikuchangwa vizuri ndio maana haya hutokea.
 
Hiyo error katika kutoa pasi na unapogundua umekosea unaurudisha mpira nyuma kidogo au unaendelea mbele.

Karata hazikuchangwa vizuri ndio maana haya hutokea.
Dah,
Nimekusoma na kucheka kidogo ulivyopiga chenga hapa!

Hiki ndicho kipaji tulichojaliwa waTanzania wengi wa sasa, na ndicho kinachotumiwa na wanasiasa wetu kadri wawezavyo kwa maslahi yao.

"Unatoa pasi, unagundua umekosea..."; halafu sijui inakuwaje "...uurudishe mpira nyuma kidogo...", na huku ulishatoa pasi! Bila shaka utakuwa na miguu ya sumaku.
 
Mutiny Nyerere asingekimbia Ikulu na wanajeshi wasingefukuza maofisa wao. Soma New York Times ya mwaka 1964. Kilishanuka ila bahati yake Nyerere alirudishwa madarakani na Waingereza



Hata chanzo ulichoweka kinakataa kuita hilo tukio kama coup. Tofautisha coup na mutiny
 
ndiyo mambo yanavyokwendaga, ni kuishi vizuri na boss wako na kuchapa kazi !! hongera kwake ila tunataka jeshi ligeuke liwe chanjo cha technologia na ubunifu nchini - sina uhakika kama Jeshi lina kiwanda hata kimoja, au limeshiriki vipi kwenye sera ya viwanda ya Taifa.
Sina uhakika pia kama jeshi linazalisha zao la Kilimo lolote kubwa liwe la Chakula ama Biashara la kimkakati nchini - haya ni mambo ambayo jeshi linatakiwa kufanya wakati wa kipindi cha amani.
Napinga vikali jeshi kuwa na viwanda au kufanya biashara. Jeshi la Misri hapa Afrika ndio huwa linafanya hivyo, linasumbua sana serikali za kiraia. Jeshi la Pakistan nalo liko hivyo wasumbufu mno.

Mfumo wetu ulitakiwa uwe exactly kama tunakoiga Uingereza. Kule humpati mtu katoka Sandhurst alafu eti anakuwa balozi sijui mkuu wa bodi gani. Unafanya ilivyosomea.

Wizara ya ulinzi ndio iwe na research facilities na departments kusaidiana na sekta binafsi. Kama Marekani walivyo na DARPA au India walivyo na DRDO inayoshirikiana na kina Mahindra na TATA
 
Hii staili ya kupandisha vyeo na kuteua alianza JPM ina maana ile safu ya juu haiamiki kwa Cha cheo Cha CDF.......??????

..Ni utaratibu wa siku nyingi ktk kuteua Cdf na CoS.

..Kama anayeteuliwa kuwa Mkuu wa Majeshi sio Mkuu wa utawala jeshini [ namba mbili kwa cheo] basi ni lazima mteuliwa ataruka rank moja.

..Kwa mfano, 1974, Kanali Abdallah Twalipo alikuwa RC Ziwa Magharibi / Kagera akaruka ngazi ya Brigedia akapanda kuwa Meja Jenerali na kuteuliwa kuwa Cdf.

..Pia miaka ya 80 Meja Jenerali Ernest Mwita Kiaro aliruka rank ya Lt.Jenerali na kupanda kuwa Jenerali na kuteuliwa kuwa Cdf.

..Miaka ya 90 Meja Jenerali Robert Mboma aliruka rank ya Lt.Jenerali akawa Jenerali na kuteuliwa Mkuu wa Majeshi.

Nas Jr
 
Back
Top Bottom