Rais Samia atembelea maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko Katesh, Wilaya ya Hanang, Manyara na Kuzungumza na Wananchi, leo Disemba 7, 2023
Yani Leo ilikuwa vituko. Yani ziara ya maafa ikageuka mkutano wa kumsifu na kumuabudu Rais. Aibu kubwa Sana.
Ni aibu kubwa sana, tena walivaa kabisa na Jezi zao za chama.
Na hata Wapinzani walioenda huko Hanang leo nao pia walivaa na Jezi za vyama vyao vya siasa.
Kwa hakika wa-Tanzania tumerogwa malogi makubwa!
 
Ndugu Freeman Aikael Mbowe ni Mwenyekiti wa Chama kikubwa cha siasa nchini anapokwenda katika shughuli yenye itifaki ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT SAMIA SULUHU HASSAN taarifa zinapaswa kupatikana mapema Je uwepo wa Mbowe Hanang, CHADEMA kilitoa taarifa na Je walikuwa sehemu ya Itifaki?majibu ya Sauti ya matukio ni wazi kutokuwepo taarifa za ujio uwepo wake,

Mbowe amekuwa sehemu ya wananchi wa kawaida kuzuiwa kutokana na taratibu za Itifaki ambapo maeneo aliyokuwa alikusudia kutembelea yalikuwa sehemu ya itifaki ya Mfariji Mkuu wa Taifa ndio maana kwa hekima kubwa kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara amekutana nae na baada ya kujua amefika Mkoani Manyara kuungana na Rais Samia kutoa pole na ratiba ya kutembelea wahanga,itifaki yake ikaandaliwa na kuruhusiwa kuungana na Dkt Samia katika shughuli ya Hanang, lakini yeye na timu yake wakaamua kuishia Babati bila kufika katika eneo la maafa.
Screenshot_2023-12-07-22-17-17-1.png
 
MAMBO YALIYOFANYWA NA SERIKALI YA RAIS SAMIA, KATIKA KUKABILIANA NA MAAFA YA HANANG

● Serikali Imewaokoa Watanzania 117 na waliopewa huduma bure za matibabu kupitia gharama iliyobebwa na Rais Samia.

● Serikali imegharamia mazishi ya Watanzania 79 waliofariki kwenye maafa ya Hanang.

● Serikali inaendelea na zoezi la kutafuta miili ya watanzania wengine walioathirika na maafa hayo.

● Serikali imeanzisha makazi ya muda kwa wakazi 440 ambao walipoteza makazi yao ya kudumu.

● Serikali inatoa huduma za Malazi, Afya, Chakula, usafi pamoja na huduma za kisaikolojia.

● Serikali imeendelea kugawa misaada mbalimbali kutoka kwa Sekta mbalimbali.

● Serikali inaendelea kusikiliza na kutatua changamoto za mtu mmoja mmoja walioathirika na maafa.

● Serikali imetoa Askari 1200 wanaohusika kwenye zoezi la uokoaji wa maafa.

● Setikali imeandaa chakula kinachotosha kwa siku 30 kwa ajili ya wananchi.

● Serikali inapambana kurejesha miundombinu inayotakiwa kwenye mitaa na vijiji na huduma za biashara zimeanza kurejea.

● Serikali imerejesha tena huduma za umeme Hanang Transfoma 79 zimerejeshwa na Nguzo 600 zimesimamishwa tena.

● Serikali imeanza kuchimba visima 10 vya maji, pia imeleta matanki ya maji yenye lita za maji 5000.

● Serikali imetoa dawa na vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi Milioni 300.
Kwahiyo ?
 
Hili ndio jambo la Aibu la kufungia Mwaka 2023, lakini cha kushangaza ni kwamba Wananchi wa Hanang ni kama wamepuuza ujio huo huku wakionekana wazi kujitenga, pamoja na ukweli kwamba wana uhitaji sana , lakini hawana furaha na ugeni huo.

Nadhani shida kubwa ni kugeuza maafa haya kuwa shughuli ya ccm , Wanajeshi wanaofanya kazi kufa na kupona hawatambuliki tena!

Kiukweli Jambo hili ni Aibu kwa Taifa.
Nyie mlikatazwa kuvaa uniform zenu za CHADOMO? CCM ni chama cha watu kipo na watu wakati wote wa raha na matatizo.
 
Tanzania bado kuna matatizo!

Nadhani bado Elimu ya Afya ya akili inahitajika!
 
Hili ndio jambo la Aibu la kufungia Mwaka 2023, lakini cha kushangaza ni kwamba Wananchi wa Hanang ni kama wamepuuza ujio huo huku wakionekana wazi kujitenga, pamoja na ukweli kwamba wana uhitaji sana , lakini hawana furaha na ugeni huo.

Nadhani shida kubwa ni kugeuza maafa haya kuwa shughuli ya ccm , Wanajeshi wanaofanya kazi kufa na kupona hawatambuliki tena!

Kiukweli Jambo hili ni Aibu kwa Taifa.
Nyie na Rais nani aliepuuzwa. Mmedoda. Na michango mmekosa😂😂
 
Hili ndio jambo la Aibu la kufungia Mwaka 2023, lakini cha kushangaza ni kwamba Wananchi wa Hanang ni kama wamepuuza ujio huo huku wakionekana wazi kujitenga, pamoja na ukweli kwamba wana uhitaji sana , lakini hawana furaha na ugeni huo.

Nadhani shida kubwa ni kugeuza maafa haya kuwa shughuli ya ccm , Wanajeshi wanaofanya kazi kufa na kupona hawatambuliki tena!

Kiukweli Jambo hili ni Aibu kwa Taifa.
Bila picha umbea
 
Back
Top Bottom