Rais Samia: Kabla sijaingia, biashara na Kenya ilikuwa ngumu. Asema kuchoma vifaranga wa Kenya yalikuwa makosa

Rais Samia: Kabla sijaingia, biashara na Kenya ilikuwa ngumu. Asema kuchoma vifaranga wa Kenya yalikuwa makosa

Mama unajichoresha tu we fanya mambo yako bila kumhusisha Magufuli utaonekana tu, by the way hatujui unatupeleka wapi
 
Rais Samia amesema amri ya kuchoma vifaranga 6400 vilivyoingizwa kutoka Kenya miaka mitano iliyopita ilikuwa sio sawa.

Rais Samia kasema hawakushulikia vizuri uingizaji ule wa vifaranga maana pia vifaranga vinavyo haki ya kuishi.

Rais Samia alizungumza haya wakati akiongea na mawakili wa ukanda ya Afrika Mashariki.

"Afrika Mashariki tuna soko la pamoja ambalo linatusaidia kufanya biashara zetu, tunakubaliana kwenye mambo ya customs na taxation lakini we had a lot of NTB's na ni tariff barriers ambazo mnajitahidi kuzifanyia kazi kuziondosha.

Ni kitu kidogo tu, ni mmoja kutoka kwenda kwa mwingine. Wakati mimi sikuingia, biashara yetu na Kenya ilikuwa ngumu sana, ngumu sana. Fika vifaranga mipakani pale, makaratasi hayasomi vizuri, vimetoka wapi haisemi vizuri, kunapita vifungu vya sheria as if sheria is everything. No no no sheria hairuhusu, solution hata hatuogopi dhambi, choma hivyo vifaranga.

Tumejisahau, vifaranga pia ni viumbe vya Mungu, walikuwa na life tukachoma"


Alisema Rais Samia

View attachment 2427229
Kabla hajaingia pia mgao wa umeme haukuwahi tulikuwa tunauona k.m historia
 
Yeye si alikuwa makamu wa Rais, alitoa ushauri gani? Aache unafiki
Hapo Sasa Ndiyo Utajua Siasa Lazima Uwe Ndumilakuwili Muda Wote


Mzilankende Unasemwa Huku!!
 
Rais wa Tanzania , Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye mkutano wa Wanasheria wa Africa Mashariki , amekiri wazi kwamba kitendo cha serikali ya Tanzania kupiga kiberiti vifaranga visivyo na hatia yoyote kutoka Kenya , haukuwa uamuzi sahihi.

Wakati unyama huo ukifanyika na kushangiliwa na Wanaccm wengi , Mh Samia Suluhu alikuwa Makamu wa Rais .

Chanzo : Mwananchi .

TOA MAONI YAKO
 
Rais Samia Suluhu anasimamia haki za wananchi na nchi pia anasimamia haki ata za viumbe hai pia kwaiyo haikua sahihi maana walikua na uwezo wa kuviludisha vifaranga vilikotoka
 
Mgao wa umeme na maji pamoja na gharama za maisha kupanda ndio changamoto kwa sasa wasitupoteze maboya, mambo ya vifaranga yalishapita yeye akaombe msamaha huko Kenya basi maana na yeye alihusika kwa huo ujinga kama hakupendezwa nao angejiuzuru.
 
wakati wa kutekeleza sheria kunachanganya sana, kwani sheria zetu zinasemaje?
 
Rais Samia amesema amri ya kuchoma vifaranga 6400 vilivyoingizwa kutoka Kenya miaka mitano iliyopita ilikuwa sio sawa.

Rais Samia kasema hawakushulikia vizuri uingizaji ule wa vifaranga maana pia vifaranga vinavyo haki ya kuishi.

Rais Samia alizungumza haya wakati akiongea na mawakili wa ukanda ya Afrika Mashariki.

"Afrika Mashariki tuna soko la pamoja ambalo linatusaidia kufanya biashara zetu, tunakubaliana kwenye mambo ya customs na taxation lakini we had a lot of NTB's na ni tariff barriers ambazo mnajitahidi kuzifanyia kazi kuziondosha.

Ni kitu kidogo tu, ni mmoja kutoka kwenda kwa mwingine. Wakati mimi sikuingia, biashara yetu na Kenya ilikuwa ngumu sana, ngumu sana. Fika vifaranga mipakani pale, makaratasi hayasomi vizuri, vimetoka wapi haisemi vizuri, kunapita vifungu vya sheria as if sheria is everything. No no no sheria hairuhusu, solution hata hatuogopi dhambi, choma hivyo vifaranga.

Tumejisahau, vifaranga pia ni viumbe vya Mungu, walikuwa na life tukachoma"


Alisema Rais Samia

View attachment 2427229
Rais Samia Suluhu ameleta Suluhu kati ya Tanzania na Kenya upande wa biashara sasa Tanzania inanufaika zaidi endelea kuupiga mwingi mama
 
Kipindi hicho watendaji walifanya mambo kwa mzuka sana. Ndiyo pamoja na uchomaji nyavu, kupasua mitumbwi, kukamata ng'ombe na kutaifisha za wafugaji, kuvamia account za watu. Kwa ujumla kilikuwa Kipindi kigumu sana.

Leo kote huko kama hawapo?!. Ulikuwa ni upuuzi.
Ulikua ni zaidi ya upuuzi lakini sasa Rais Samia Suluhu anaendesha nchi kwa akili na sio nguvu
 
Mgao wa umeme na maji pamoja na gharama za maisha kupanda ndio changamoto kwa sasa wasitupoteze maboya, mambo ya vifaranga yalishapita yeye akaombe msamaha huko Kenya basi maana na yeye alihusika kwa huo ujinga kama hakupendezwa nao angejiuzuru.
Sasa umeme mvua ikinyesha wiki tu, hiyo agenda inawafia, 😄tafuteni ajenda nzuri,, hili la umeme ndani ya nwezi huu tu hali itakuwa stable
 
Toka juzi mama alipoingia Arusha mpaka leo umeme haujakatika.
Nashauri mama aendelee Kukaa Arusha mpaka mwisho wa mwaka
 
Kwa akili yako timamu unaamini kwamba kipindi cha Jiwe alikuwepo mtu gani wa kumshauri?!
Au uliwahi kusikia Jiwe ameshauriwa kitu na nani?
Sasa kama huwezi kutimiza majukumu yako si unajiudhuru tu
 
Back
Top Bottom