Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Hotuba yake yote analalamika tu mm nahisi haelewi nguvu ya kimamlaka aliyokuwa nayo, 2025 atupishe kwakweli maana hatufai kwanza katurundikia mitozo Kila mahali, bei ya nafaka inazidi kupaa, maisha ya wananchi yanazidi kuwa magumu mbaya zaid watu wanatafuna pesa zetu sasa ya nn kuendelea kuwepo madarakani?
 
Watu wapo, wasimamizi wapo majaji wapo. Sasa maamuzi ni kulalamika au kuwasweka ndani wahusika?
 
Yusuf Manji
 
Mwenye kufahamu kwa ujumla hasara tuliyopata kutokana na upigaji na hatua Madame Presidaa alizochukua, hizi za yakhe waitwa Post sio wakati wake!!!
Watu wameiba na ushahidi umepata unataka wakakae nao tena, Rais Ng'ata sasa kubweka tu hakutoshi vyuma vimezoea kupiga na vimekaa pale.
 
Aisee..
Si achukue hatua badala ya kulalama?!
 
Yeye alitegemea hii nchi utaiendesha kwa huruma huruma za kike utaweza? Eti sitamtumbua mtu, watu wanatambaa na chaki tu. Advertise mama alianza kuwatoa wezi jela na kuwalipa hela 😀😀😀!

Sasa sahizi mchwa wamemzunguka wanatafuna bila huruma na wala hawamuwazi wala nini.
 
Hahahahahah sasa 66B unafikiri utakaa uwe maskini saa ngapi? Thats was almost 30M dollars! Ikienda kwenye stocks and bond Marekani wewe ni kuvuna mihela tu.
 
Acha porojo ww ni mtu mzima aisee mbona mnakuwaga kama mazombe kama unachuki zako binafsi na mwendazaek nenda kalichape kaburi
 
Tatizo Sasa hivi Ni kwamba, atatumwa Nani akamkamate Nani?
Waziri wanajua alivyoiba
Karibu mkuu mwizi
Makamishna wezi
Wakurugenzi wezi
Takukuru imekua rukukuta
Polisi imekua polisi jazz bend
iPhone inanunulika kiulaiiini.
Hahahah haah yani hapo hakuna wa kumkamata mwenzie maana kwenye hio migao bi mkubwa taarifa anazo. Tukisema hii ni awamu ya 4B muelewe.
 
ni aibu rais kulalamika ni wazi hatambui madaraka na kazi yake ndio maana anagawa pesa ovyoovyo. Kwa utaratibu wa sasa ni vigumu mtu kukopa benki tofauti bila kujulikana kwa sababu bot wana data zote za wakopaji, anatakiwa aanze na bot kisha benki zilizohusika.
 
Ndugu ukisikia mwanasheria mkuu anasema kuna sheria hazitekelezeki hilo sio jambo dogo. Mamlaka uisemayo aliyonayo rais usifikiri ndio jibu la matatizo haya. Jibu ni moja tu; kila mhimili (serikali, bunge na mahakama) uachwe ufanye kazi yake kwa uhuru wake haya yatapungua mno, ila kuacha sijui rais afukuze yule afanye hivi mwisho hata wanaofukuzwa mwishowe wanashinda kesi (kumbuka serikali iliyopita ilifukuza sana kwa matamko na wengi waliendelea kulipwa stahiki zao vilevile ila nje ya vyeo walivyotumbuliwa jambo ambalo lilikuwa la kisheria ila hasara kwa nchi)
 
Hio Trillion moja mnayoona nyingi zile alizopiga Lameki kwenye miradi badala ya trillion 4 akalipa 6, jumlisha na mabillion wanayopiga Makamba na wenzake haya hizo za CAG alizosema TRC wamepiga 500B na za Manunuzi ya Cargo Airline 115B hebu acheni mambo ya kikuma aisee.

Hio trillion 1.5 ni ya chuki wala haina ushahidi ila mmeishikia bango. Hakuna awamu itavunja rekodi ya ufisadi kama hii hapa. Hata kikwete hawezi ingia yani
 
Acha porojo ww ni mtu mzima aisee mbona mnakuwaga kama mazombe kama unachuki zako binafsi na mwendazaek nenda kalichape kaburi
Sio chuki Rais aliepita alifoka tu hata ukitukana huwezi kubadilisha ukwel, zombie ni wewe ambae unamuhusudu mtu kuliko hata taifa lenyewe, ATCl ilipotoa gawio wote si tuliona mwisho wa siku CAG akaripoti hasara, 1.5 tri ziliposhindwa kuonekana mwisho wa siku akatumbuliwa prof Assad kuhoji kwannn Bunge limekuwa bubu, acha utoto unapojibu watu wazima.
 
Sasa kama kila muhimili ukitakiwa kufanya kazi yake huoni kwamba ni ngumu sana kukamata wezi. Raisi ana influence kubwa asana katika hilo maana jaji mkuu yuko chini yake. Mimi uniwekee billion 30 kwanini nisifute kesi haraka au kuipotezea.

Tajiri hafungwi Tanzania. Maskini tu ndio watajazana jela.
 
Ewe lijinga na wajinga. Tena na hao wajinga wenzako nimeona kuna ma group kabisa ya wasomi eti wanasema eti mara Dkt Magufuli etc. Tulieni tuwaambie iko hivi. Prof. Asad alitumika na mabeberu na kundi la watu wabaya wale mafisadi ili kujaribu kutafuta makosa. Hiyo 1.5 trillion ilikuwa na maelekezo na yalitolewa na yeye akakomaa yaani ni sawa na budget ya CIA uende ukajifanye mara ohhh waliomtumbua ni hao hao walinzi wa taifa na ndiyo maana he will never amount to anything kwa hii nchi kwa sababu prof Asad ni mtu aliyeelimika ila hana common sense, na binaadamu ukikosa common sense hata uwe prof utaendelea kuwa mjinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…