Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Actually, msingi wa kuwa na katiba nzuri ni kupata sheria nzuri zitakazowalinda wananchi na mali zao na rasilimali za nchi. Katiba ya sasa imejaa 'clawbacks' ambazo zinafanya haki zilizotolewa zinyang'anywe tena na pia ilitungwa wakati wa mfumo wa chama kimoja na ndiyo maana hata pale vyama vingine vina haki ya kufanya mikutano yao inaingiliwa kwa sababu unakuta sheria iliyotungwa inakuwa na nguvu zaidi kuliko katiba yenyewe. Polisi akizuia jambo hata kama amefanya hivyo kimakosa anaonekana alichokifanya ni amri au agizo "halali" (alilolifanya with the authority of the law). Sasa kama hatupati katiba inayoweza kuweka msingi mzuri wa sheria zetu wananchi wataendelea kukosa haki zao za msingi na kuumizwa hata pale wanapokuwa na haki ya kufanya jambo ambalo wanakatazwa wasifanye.
Hakika.
 
Wamkumbushe kitabu kinachoitwa katiba ndiyo kimemfanya awe rais! Kweli Tanzania tumepata hasara. Ni aibu tupu kusema maneno ya kijinga kama haya yametoka kwenye kinywa cha rais wa nchi.
Huenda nchi yetu haina maendeleo maana kuna hii katiba iliyopo sasa, hivyo inatakiwa tusiwe na katiba kabisa hadi tuwe na maendeleo.
 
HUYO ATUELEZE KATIBA NININI??
Unapotaka kuongoza watu unavyojiskia wewe huwezi kutaka katiba Bora!!
Utateuaje MKWE wako kuwa waziri kama katiba haikupi nafasi yakufanya utakayo?? Watu wajinga wengi watakuabuduje? Utajilimbikiziaje Mali wewe na nduguzo??
Ili tupate katiba mpya inabidi kama taifa tuwe nawatu strong na conscious ( imara na wanaojitambua) kitu ambacho nishughuli maana wengi ni dhaifu na wasojitambua, wanajua kumsifu tuu kiongozi ili wapate chakula leo
 
Baada ya kuyasikia yote, niliishia kujisemea Nchi sio familia.
 
Kwa hiyo Rais Samia alitaka kusema nini?
Hakuna haja ya kuwa na vitabu vitakatifu au katiba?
Hata tukiwa na hivyo vitabu bado hatupaswi kuvifuata?

Kuna vitu mtu mwenye heshima au mamlaka hupaswi kuvisema mbele za watu, maana ukivisema watu watagundua ujinga ulionao.
Ni kweli pale naona kama alipanic na akikosa hekima sema wanawake ni waropokaji.
 
Rais Samia amesema " Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
[emoji2956][emoji120][emoji7][emoji1666][emoji106][emoji1720][emoji2788][emoji1732][emoji123][emoji95][emoji117][emoji109]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mh.Rais SSH yuko sahihi....

Sasa ujenzi wa SGR umeletwa na katiba ?!!!!

Ile adha ya pale lilipo daraja la juu la "mfugale" iliondolewa na katiba ?!!! [emoji3][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Rais Samia amesema " Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Huko kichwani mwako kuna kila aina ya wadudu, maana kila kukicha kuna aina mpya ya mdudu anayejitokeza mbele na kushikilia wadudu wengine wote siku hiyo wasifurukute.

Huyu mdudu wa leo ndiye kakufanya uuone ujumbe huo kuwa wa maana zaidi wakati hauna chochote cha kuufanya uwe wa maana.

"Viongozi wa kisiasa tunadhani tuna haki ya kuburuza watu tunawageuza watu makasuku." Kuna lipi la maana katika mstari huu la kukufanya uone ujumbe ni bora sana katika mwezi wa September?

"Nenda kamuulize kifungu gani cha katiba kinakuudhi. Hajui" - Hili ndilo linalokufanya uone uzito wa ujumbe huo kuwa mkubwa sana kwako? Huyu mdudu wa leo huko kichwani mwako hutumia kilevi?

"Sasa katiba mpya ilete nini" Anakujibu "Maendeleo" Kuna lipi la maana hapa katika maneno haya kama siyo kuonyesha upungufu wa uelewa wa mtu aliyeyatamka maneno haya yanayokufanya wewe uone ujumbe ni bora sana wa mwezi wa September?

Baraza la mawaziri alilo nalo Samia limejaa wanasheria wasiojua maana ya sheria na katiba, au ni yeyye Samia kawafundisha kwa miaka mitatu waielewe Katiba na sheria ili wazitumie kama wanavyotaka kuwafundisha wananchi wote matumizi ya katiba hata hii mbovu wanayoikiuka kila mara wao?

Wanataka kwenda kuwafundisha wananchi namna ya kuitumia katiba kwa njia wanazotaka wao?
Hii ni katiba ya nchi, au ni katiba ya genge la wahuni waliko ndani ya CCM, wewe Johnthebabtist' ukiwa mmoja wao?
 
Katiba ndio mkataba mama isipokua vzr utazaa vimikata vibaya vingi vya kutuibia
 
HOTUBA YA RAIS KWENYE UFUNGUZI WA KIKAO JANA: IMEACHA MASWALI MENGI KUHUSU KATIBA.

Mh. Rais yuko kwenye nafasi aliyopo kwasababu ya hiyo katiba, anawezaje kusema ni kitabu ambacho hakiwezi kuwaletea maendeleo wananchi, na kwamba hata vitabu vitakatifu havifuatwi!! Je, hicho kikao kinachoendelea ni kwa ajili ya kubatiza au kusilimisha watu? Kuna wengine ni wapagani na Imani tofauti hawana habari na hivyo vitabu vinavyoitwa vitakatifu, hao anawaweka kundi gani? Haya mambo ya Imani ni ya kuepukwa kwenye majukwaa ya siasa na kuacha mikononi mwa watu binafsi, Mashehe na Wachugaji.

Ni wanyama pekee wanaoweza kuishi bila kujiwekea utaratibu. Nchi nyingi uingia kwenye misukosuko na pengine serikali kuangushwa kwasababu ya kutokuheshimu hicho anachokiita kitabu. Na si kwamba nchi zilizoendelea hazina na wala hazifuati katiba eti kwasababu katiba haileti maendeleo. Siamini mtu kama Rais ambae alisha kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la kutunga katiba anaweza kutamka haya maneno, lah sivyo ama ameshaanza kulewa madaraka au kuna force nyuma yake inayomfanya aogope hiyo katiba mpya.

Maswali ya kujiuliza, alikuwa akitafuta kitu gani hadi akawa makamu mwenyekiti ndani ya Bunge la katiba ili hali akijua ni kupoteza fedha na wakati? Akijua ni kitabu ambacho hakiwezi kuleta maendeleo? Akijua wananchi hawana uelewa na katiba, ni darasa lipi atakaloliandaa watu wafundishwe na kuilewa hiyo katiba? Anawezaje kukaa madarakani kwa katiba ambayo wanchi wake hawailewi? Je, viongozi watangulizi wake hasa JK, Warioba na tume yake ya katiba hawakuyaona haya au hawakuwa na ulewa kuhusu wananchi wa nchi hii. Katika hili Rais aje na sababu za maana kuliko kutusimanga juu ya uelewa wetu wa katiba.
Inasikitisha. Tuko pamoja
 
Mwanafalsafa mkubwa Plato alipendekeza hii kitu "philosopher king";na akaweka msisitizo thabiti kwamba lazima Kiongozi (king) awe ni mtu mwenye upeo mkubwa wa kiakili ambaye ataweza kubaini ukweli jinsi ulivyo (objective truth) na ukweli kama unavyojitokeza (relative Truth).

Ni kwa bahati mbaya kwamba taifa letu vilaza ndo viongozi na hili,lisha wahi kutamkwa na nguli wa fasahi Tanzania na Afrika Mashariki bwana Shaaban Robert "Kuna Karne itafika kwa wajinga kuwa viongozi na werevu kuwa wafuasi nadhani Karne yenyewe ndo hii".
 
Yaani jana kama tungekuwa na kepteni jasiri kutoka jeshi la wananchi wa Tanzania basi leo angetangaza kuchukua nchi kwa maana Rais tulienae hakuapa kwa mujibu wa katiba aliapa kwa mujibu wake yy mwenyewe hivyo basi apatikane raisi atakayeapa kwa mujibu wa katiba na anatambua umuhimu wa kuapa kwa mujibu wa katiba lkn si huyu mama.

Hapa mama kaanza kuwa yeye sasa. Rais Magufuli alikuwa akiongoza kwa kutumia vipaji vyake vya asili na ndio maana alikuwa kiongozi bora kabisa hii nchi iliwahi kupata. Kitendo cha mama kuanza ku"question" motives za wanasiasa zinaonyesha jinsi ambavyo ameanza kung'amua kuwa usipotumia common senses zako katika uongozi wako utajikuta unaendeshwa tu kama lirobot. Ndio, umuhimu wa vitabu katika kuongoza nchi upo lakini nimependa jinsi ambavyo mama ameweza kufikiria kama yeye.
Tunajaribu kusafisha eneo kuku kanya, mara bata anaharisha.
 
haya maendeleo anayoyawazia Samia, ambayo anajua hayaletwi na kitabu, yeye anaamini yataletwa na kunadisha mali zetu na kuwategemea hao wanaokuja watuletee maendeleo?
Hicho ndicho kitabu chake anachokiamini yeye kuwaondoa waTanzania katika hali ya maisha duni?

Anaamini, ni yeye na Baraza lake la Mawaziri wanasheria, ndio wanaojua na kushikilia funguo za kuwaletea waTanzania maendeleo bila ya kuwashirikisha wananchi?

Hotuba hafifu kabisa isiyokuwa na mwelekeo kwa nchi.

Haya ndiyo matokeo ya kuokoteza tu viongozi bila hata kuwa na njia zinazofahamika hawa watu wanaokotwa wapi.
Haya yote ni matokeo hayo hayo ya kuwa na katiba mbovu.
 
Huko kichwani mwako kuna kila aina ya wadudu, maana kila kukicha kuna aina mpya ya mdudu anayejitokeza mbele na kushikilia wadudu wengine wote siku hiyo wasifurukute.

Huyu mdudu wa leo ndiye kakufanya uuone ujumbe huo kuwa wa maana zaidi wakati hauna chochote cha kuufanya uwe wa maana.

"Viongozi wa kisiasa tunadhani tuna haki ya kuburuza watu tunawageuza watu makasuku." Kuna lipi la maana katika mstari huu la kukufanya uone ujumbe ni bora sana katika mwezi wa September?

"Nenda kamuulize kifungu gani cha katiba kinakuudhi. Hajui" - Hili ndilo linalokufanya uone uzito wa ujumbe huo kuwa mkubwa sana kwako? Huyu mdudu wa leo huko kichwani mwako hutumia kilevi?

"Sasa katiba mpya ilete nini" Anakujibu "Maendeleo" Kuna lipi la maana hapa katika maneno haya kama siyo kuonyesha upungufu wa uelewa wa mtu aliyeyatamka maneno haya yanayokufanya wewe uone ujumbe ni bora sana wa mwezi wa September?

Baraza la mawaziri alilo nalo Samia limejaa wanasheria wasiojua maana ya sheria na katiba, au ni yeyye Samia kawafundisha kwa miaka mitatu waielewe Katiba na sheria ili wazitumie kama wanavyotaka kuwafundisha wananchi wote matumizi ya katiba hata hii mbovu wanayoikiuka kila mara wao?

Wanataka kwenda kuwafundisha wananchi namna ya kuitumia katiba kwa njia wanazotaka wao?
Hii ni katiba ya nchi, au ni katiba ya genge la wahuni waliko ndani ya CCM, wewe Johnthebabtist' ukiwa mmoja wao?
Katiba ni nini?
 
Rais Samia amesema " Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Ndiyo, maendeleo yanaletwa na kitabu. Kila jambo la maendeleo hupangwa kwenye kitabu ndio utekelezaji hufuata, mfano ni namba gani tutapata Rais, wabunge na madiwani imeandikwa, Ila CCM kwa uroho wao wa madaraka hukiuka na kupitisha wagombea kwa nguvu ya TISS na Polisi, kama ambayo watu tunavyokiuka vitabu vya dini na kuitwa Wadhambi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom