Rais Samia: Nikijua wewe ni dhidi yangu(Serikali) siwezi kukushirikisha. Utatumia sheria zote za Kimataifa, nitatumia za ndani kuku-bar

Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika mkutano wa 47 wa wanasheria Afrika Mashariki uliofanyika mkoani Arusha, amesema haya kuhusu kushirikisha watu...
Huyu huyu alipoingia madarakani akawadanganya chadema kwamba atateua wapinzani kwenye serikali yake, wakafikiri mbowe atateuliwa wakasema anaupiga mwingi.
 
"...ukikaa kiuadui..." Ndio kukaaje huko?
Inawezekana pia kusema "...ukikaa kiurafiki..."?

Watu hupenda kujitoa akili na mambo yaliyo rahisi kabisa wakidhani kila mtu karukwa na akili!
 
Huyu huyu alipoingia madarakani akawadanganya chadema kwamba atateua wapinzani kwenye serikali yake, wakafikiri mbowe atateuliwa wakasema anaupiga mwingi.
La mbowe wampe uwaziri, anafaa sana yule
 
Namshukuru MUNGU Kwamba hadi Sasa hakuna alieonyesha kuwa you dhidi yake!

Wanaopiga kelele wanapiga kuhusu mambo ya msingi tu kama maji na umeme!plus pembejeo za wakulima!

Wanasaidia Ili usilale usingizi wa pono ukaharibu!

KWA mfano umeme wa Sasa ni kama kibatari unazima Hata kwa ushuzi tu!!
 
Tatizo letu ni lile lile, wabongo wengi wanapenda burebure,, nyerere aliwadekeza sana,, umeme bure, matibabu bure, elimu bure, usafiri bure🙆🏻‍♀️
Hiyo sumu isiyokwisha mwilini ni sumu ya aina gani hiyo?

Halafu hata waliozaliwa miaka kadhaa bada ya huyo aliyemwaga sumu ndio wawe waathirika zaidi ya walioonja sumu wenyewe?

Hapana, sikubaliani na hoja yako.
 
Uadui tena? [emoji2369][emoji15]

Kitu ambacho nimekuwa Niki kuona au kusikia ni kuwa ni bahati mbaya sana na pengine inherited mistakes kuchukulia wapinzani au wakosoaji wenye nia njema kuwa kama maadui.
 
Hiyo sumu isiyokwisha mwilini ni sumu ya aina gani hiyo?

Halafu hata waliozaliwa miaka kadhaa bada ya huyo aliyemwaga sumu ndio wawe waathirika zaidi ya walioonja sumu wenyewe?

Hapana, sikubaliani na hoja yako.
Chukulia mfano PAP wametuuzia umeme tena kwa bei cheap kuliko hata songaz,,
Umefika mda wa kulipa , tena pesa ilitengwa escrow fund,, watu wanadai hiyo pesa ni ya umma,, yaAni utumie umeme wa watu kulipa iwe ishu🤗
 
Wapinzani sio maadui.

Sio Waasi.

Wakosoaji sio maadui .

Sio Waasi.

Wapo kuchagiza mambo yaende kwa uzuri na ufanisi zaidi.

Wapo kutoa alarming alerts matharani mahala fulani panapigwa serikali ingilieni kati kuzuia upotevu wa rasilimali usiwe mkubwa zaidi.

Au pengine ni viashiria ambavyo serikali ikiwahi kuzuia tutaokoa mapato ya serikali.

N.k
 
Nguvu nyingi Sana inatumika kusakama wapinzani na kuwafumba midomo mfano kwa kuzuia ufanyikaji wa mikutano ya hadhara kumbe huenda ni sababu ya kuchukuliwa kana kwamba ni maadui?!

Kuifikia demokrasia ya kweli tuna safari ndefu.
 
Chukulia mfano PAP wametuuzia umeme tena kwa bei cheap kuliko hata songaz,,
Umefika mda wa kulipa , tena pesa ilitengwa escrow fund,, watu wanadai hiyo pesa ni ya umma,, yaAni utumie umeme wa watu kulipa iwe ishu🤗
Kwa maumivu wanayotupa wale ni sioni ganzi
 
Ni jambo jema

Ndio sababu tunasema Vyama vya Upinzani vya Tanzania ni lazima visupport Serikali vinginevyo vinawekwa pembeni!

Mimi nina shida neno UPINZANI nalipinga sana. Maana wenyewe ni kuipinga tu serikali. Liwe jambo jema au siyo jema, wenyewe ni kupinga tu. Nadhani ni vyema tukataza upya muktadha na mantiki ya upinzani. Bora tungetumia neno M'BADALA.
 
Hii nchi mbona kama sio Ile ya Enzi za wale walioishi kwa matarajio na matazamio ya mbali? Ipo siku tunachokiona hatutakipata kisa tu kuteteleka na kukosa msimamo na mambo ya seriously we are going wrong totally imagine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…