Rais Samia: Nikijua wewe ni dhidi yangu(Serikali) siwezi kukushirikisha. Utatumia sheria zote za Kimataifa, nitatumia za ndani kuku-bar

Rais Samia: Nikijua wewe ni dhidi yangu(Serikali) siwezi kukushirikisha. Utatumia sheria zote za Kimataifa, nitatumia za ndani kuku-bar

Mama anataka wanaomsapoti kwenye Mbio zake za Urais 2025 tu.

Nje ya hapo hakuna.

Ni lini Ccm au viongozi wake walishamshilikirisha mtu mwingine kwenye mambo yake?

Rais Samia awe mwazi asizunguke zunguke mbuyu.

Inaonekana Mbio za Urais zinamtesa sana.
Samia alikuwa na nafasi ya kuwa zaidi ya rais.

Alikuwa na nafasi ya kuwa kiongozi wa Africa na dunia.

Angeweza kuwa stateswoman.

Sasa hivi Africa haina rais mwingine mwanamke.

Ana nafasi kubwa ya kusikilizwa si kama rais wa Tanzania tu, bali mwakilishi wa watu wote, hususan wanawake kutoka nchi zote zinazoendelea.

Lakini kwa maneno haya ya shombo la taarab za mipasho, asahau kupata credibility.

Watu wanamsoma kimataifa na kuandikiana vimemo kwamba hapa hamna kitu.
 
Taarifa zimfikie Tundu Antipasi Lissu , huyu ndo anajidai anazijua sana Sheria kuwaliko watanzania wote.

Pamoja sana mama Samia
Hakika wewe ndo yule tuliyekuwa tunamsubiri

Samia for 2025
Binafsi utendaji wa Rais Samia bado haujanishawishi niamini kuwa ana nia thabiti ya kumsaidia mwananchi masikini wa nchi hii ajikwamue kiuchumi.
 
Kasema ukiwa "adui". Manake unampinga ili ashindwe ..haupingi ili kumkosoa ...ni Sawa na Wale wanapinga kila kitu
Katolea mfano wa TLS kwa miaka 5 iliyopita.

Je hicho chama kweli kilikuwa adui wa selikali?
 
Binafsi utendaji wa Rais Samia bado haujanishawishi niamini kuwa ana nia thabiti ya kumsaidia mwananchi masikini wa nchi hii ajikwamue kiuchumi.
Mama anapiga kazi , tumwamini, Kuna kakundi kadogo sana kanawaza kumrudisha nyuma mama, na kanakuwa kanazusha taarifa za uzushi dhidi ya mama.

Ila mama anapiga kazi, ona miradi yote iliyoachwa na mtangulizi wake inavyokamilika kwa wakati kitu ambacho maadui na watu wabinafsi wa taifa letu wangependa miradi hii ikwame ili wapate pa kusemea
 
Ndiye aliyejenga mfumo mbovu tulionao. Bila ya mfumo huu tungekuwa mbali sana


Kuendelea kumlalamikia Nyerere for your failures ni kutafuta excuses na kukosa akili. Sawa na mtu anayemlalamikia Babu yake kwa failures zake.

"If You Born Poor,It is not your mistake,
but if you die poor,it is your mistake"
 
Kuendelea kumlalamikia Nyerere for your failures ni kutafuta excuses na kukosa akili. Sawa na mtu anayemlalamikia Babu yake kwa failures zake.

"If You Born Poor,It is not your mistake,
but if you die poor,it is your mistake"

Mfumo mbovu uliojengwa na Nyerere bado upo. Lazima lawama zipelekwe kwake.
 
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa mkoani Arusha amesema haya kuhusu kushirikisha watu/taasisi ambazo ziko dhidi yake

Kwa mfano Tanzania, miaka minne mitano iliyopita tulikuwa na Tanganyika Law Society ambayo frankly speaking ilikuwa siyo chama cha Wanasheria, kilikuwa chama cha Wanaharakati na mapambano yao yalikuwa ni dhidi ya Serikali.

Sasa mimi nikijua wewe ni dhidi yangu nitakushirikishaje? Siwezi kukushirikisha, si ndiyo! Mpaka unioneshe kwamba am here to support you, I'm here to serve a country, I'm here kuonesha ujuzi wangu kwa nchi yangu.

Nikikuona una sura hiyo nitakushirikisha, nikikuona una sura ya uadui nami sitaweza kukushirikisha. Utatumia Sheria zote za Kimataifa, zoooote na mimi nitatumia zangu za ndani ya nchi kuku-bar usishiriki kwangu.

Kauli hii ni ya KUTISHA sana kutoka kwa kiongozi wa nchi ambaye amejipambanua kuwa analijenga Taifa lenye kuheshimu misingi ya utu na demokrasia.

Sisi tunaopinga Legacy yake anatuona ni maadui wa Taifa. Yeye ndie rais wa anchi na ndiye mmiliki halali wa Tanzania.

Katiba inatudanganya
 
Kinachosababisha watu au taasisi kuwa dhidi ya Serikali ni hatari zaidi ya hao watu wanaokuwa dhidi ya Serikali.
 
Back
Top Bottom