Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Kweli...

Ndio maana TRA wakiwa around na center flani..kila mtu Nduki.

Kuna mambo ukibembeleza bembeleza hayaendi kamwe!
Kuna nchi watu hawakwepi kodi mbona, walau watu walio wengi isipokuwa wachache sana walioshindikana. watu wanaona fahari kulipa kodi.

Kitengo cha elimu kwa mlipa kodi hapo TRA mnakunywa chai tu badala msambae mitaani kutoa hii elimu adimu ya kizalendo, kodi zikiwa rafiki na haki watu watalipa bila msukumo, ni suala la muda mrefu kujenga nchi na kuwaelimisha walipa kodi sambamba na sheria kali za kodi, ukikwepa kodi sahihi uliyopangiwa yakupate tu yakukupata.

Rushwa kwa maafisa pia ni jipu, mtu kakwepa kodi 3M, afisa anamwambia nipe 1M tumalizane, hili jambo lina mzizi mrefu sana. Maafisa wa TRA wana mishahara ya kawaida kabisa, huo ukwasi wa ghafla ghalfa wachunguzwe wanakoutoa, Nchi hii tuwe waadilifu jamani.
 
Kuna nchi watu hawakwepi kodi mbona, walau watu walio wengi isipokuwa wachache sana walioshindikana. watu wanaona fahari kulipa kodi.

Kitengo cha elimu kwa mlipa kodi hapo TRA mnakunywa chai tu badala msambae mitaani kutoa hii elimu adimu ya kizalendo, kodi zikiwa rafiki na haki watu watalipa bila msukumo, ni suala la muda mrefu kujenga nchi na kuwaelimisha walipa kodi sambamba na sheria kali za kodi, ukikwepa kodi sahihi uliyopangiwa yakupate tu yakukupata.

Rushwa kwa maafisa pia ni jipu, mtu kakwepa kodi 3M, afisa anamwambia nipe 1M tumalizane, hili jambo lina mzizi mrefu sana. Maafisa wa TRA wana mishahara ya kawaida kabisa, huo ukwasi wa ghafla ghalfa wachunguzwe wanakoutoa, Nchi hii tuwe waadilifu jamani.
binti kiziwi
 
Tatizo la ukusanyaji mapato si kwa Wizara na Taasisi zake tuuu, hata Halmashauri zetu pia. Kuna halmashauri zimewafungia wafanyabiashara vibanda vyao zaidi ya mwaka sasa kwa kukosa busara na kukiuka mikataba ya kisheria iliyoridhiwa awali.
 
Kweli...

Ndio maana TRA wakiwa around na center flani..kila mtu Nduki.

Kuna mambo ukibembeleza bembeleza hayaendi kamwe!
Kwasababu kuna notion ya siku nyingi sana imejengeka kuwa TRA ni maadui, wafute hiyo notion kwa kutoa elimu. Halafu kuna muda wafanyabiashara wanaona bora wakwepe kodi tu, sasa kama mfanya biashara mkubwa wa kodi 100M anasamehewa halafu mfanyabiashara wa kodi 400k anakabwa unategemea nini? Mara nyingi wanaosamehewa kodi, kodi zao zinapelekwa kwa wafanyabishara wadogo kuzifidia, Huko TRA kunahitaji reform ya kiutendaji, kisera na kisheria.
 
Mtanzania hawezi lipa kodi bila shurtu.time will tell.
 
Mama kama mama, Watanzania tufanye kazi tulipe kodi, na tuwe proud kulipa kodi.
natamani hii mentality iwe induced kwetu.
sijui wazungu wamewezaji kuzishawish jamii zao zilipe kodi.
imefika mahali wanaona aibu hata wasipo lipa kodi. yaani kwao wanasikia msukumo toka moyoni kabisa.

lini tutafika huko?
 
Mheshimiwa Rais Mama Samia amemuonya Waziri wa wizara ya Fedha kuacha kutumia nguvu kwenye kukusanya kodi badala yake watumie akili.

Mama Samia ameonya tabia ya Watendaji wa Serikali kutumia nguvu kukusanya kodi, kufungia biashara zao, kunyang'anya fedha kwenye akaunti kisa Sheria inawaruhusu.

Ameongeza kuwa Kitendo hicho kinasababisha wafanyabiashara kufunga biashara zao na kukimbilia nchi Jirani na hatimaye Serikali kukosa mapato.


Tatizo la ukusanyaji mapato si kwa Wizara na Taasisi zake tuuu, hata Halmashauri zetu pia. Kuna halmashauri zimewafungia wafanyabiashara vibanda vyao zaidi ya mwaka sasa kwa kukosa busara na kukiuka mikataba ya kisheria iliyoridhiwa awali.
 
Mama kama mama, Watanzania tufanye kazi tulipe kodi, na tuwe proud kulipa kodi.

Naunga mkono hoja binti kiziwi lakini ukweli ni kwamba ukiwaomdoa wafanyakazi wa Umma wengi wote walio baki hakuna anayependa kulipa kodi hapa tanzania!

Hata yakiwekwa mazingira gani hakuna mfanyabishara mkubwa au mdogo atakuwa tayari kuleta haki ya TRA au Halmashauri bila kusukumwa na hilo sio africa pekee ni tatizo pengine la dunia!

Nina kuhakikishia bila nguvu na akili hakuna kodi wala ushuru TRA wataweza kusanya kamwe na hizi ni hadithi!

Wafanya biashara wote target yao ni kutengeneza faida kubwa hata maradufu huku wakitafuta mwanya wa kukwepa kodi!


“CCM mbele kwa mbele”
 
Weee mdanganye tuu,
nchi hii ni nani aliye tayari kulipa kodi stahili kwa biashara/ shuguli anayo ifanya labda mfanyakazi tuu through PAYE, Kila mfanya biashara ana wazo la kukwepa kodi ili maximize mapato yake., mwacheni rais akusanye kodi
Kama nchi tunatakiwa tukusanye shilingi ngapi kutokana na biashara kubwa, za kati na ndogo? tukifahamu hili tutafahamu ni kodi kiasi gani inayokwepwa, Msije mkawa mnajipangia malengo kwenye biashara hewa. Mwisho mkishindwa kufikia malengo mnaanza kufukia mashimo kwa kuwaibia watu na kuwafanyia unyang'anyi.

Je TRA wanazifahamu Biashara zote zilizofunguliwa walau kwa wakati fulani, wanafahamu waliofunga kwa sababu mbalimbali, mafaili yao yanawaambia nini juu ya trend ya biashara, wanafahamu biashara za mwaka jana, kwa mwaka huu zimeweza kuongeza faida ili waweze kukadiria kodi upya? maswali ni mengi kuliko majibu.

Ni ajabu mtu amefunga biashara kwa kutokuelewa hajaenda kuomba kudeactivate TIN, TRA nao wamekaa wanamhesabia deni, badala wamfuatilie kujua kwanini haji kulipa kodi. Mwishowe mtu amefunga biashara miaka mi3 nyuma huku ana deni la miaka yote hiyo, Mfanyabishara hapa ni Naive, na TRA ni wazembe.
 
Sisi wananchi wenyewe kulipa kodi bila kusukumwa ni mtihani!! Ukisema leo waje kwa kulemba kwenye kodi aaah hawapati ata bilion 1 kwa mwezi. Wakwepa kodi wengi wanajua kama wanakwepa kodi na wanafanya hivo ili faida ipige maradufu.

Nguvu bila akili.
 
Mama Samia ameonya tabia ya Watendaji wa Serikali kutumia nguvu kukusanya kodi, kufungia biashara zao, kunyang'anya fedha kwenye akaunti kisa Sheria inawaruhusu[emoji1752][emoji1752][emoji1752][emoji1752] Mungu akubariki Bi mkubwa
 
Kweli...

Ndio maana TRA wakiwa around na center flani..kila mtu Nduki.

Kuna mambo ukibembeleza bembeleza hayaendi kamwe!

Toka lini kutumia akili ni kubembeleza? Kama umeshindwa kutumia akili kupata kodi sogea pembeni usaidiwe na wenye akili. Hii na awamu ya sita awamu ya wenye akili
 
Back
Top Bottom