Rais Samia tafadhali muangalie sana Waziri wako Mmoja usidhani anakunyooshea njia bali anakupeleka Shimoni mazima

mkuu huyu tumesoma nae kabisa ni Genius kweli ila labda ni ushamba flani tu unamsumbua kupewa vyeo vikubwa vimemzidi umri!
He is obsessed to become the Head of State!
Genius au Genie?
 
Tumeingia second half, madiluuu atoke nje, aingie DR KIMEI.

Tatizo Nchi hii Si ktk Upatikanaji wa RASLIMALI, tatizo ni kukosa UONGOZI Bora. Amen
 
Ninawapenda mno JF Genius Members wachache kama Wewe Mkuu kwani huwa mnanirahisishia sana Kazi hapa tulipo.
Mkuu GENTAMYCINE! Huyu jamaa mimi sijawahi muamini hata siku moja.

Kuna wajanja wachache wameamua kumshawishi mama amuweke huyu pale HAZINA.

Ili wao watimize malengo yao vizuri.

Halafu huwa ninajiuliza kwa nini "VP" ambaye ni mbobezi wa hiyo sekta ya fedha.
Hatuoni akitoa mchango wake ili kuyazuia baadhi ya haya madudu yanayoendelea pale?
 
Mwigulu kamatia hapo hapo Hawa ni majizi waliozoea kula pesa Sasa Mwigulu kawabana wanajikosha kwa kujifanya wanatoa ushauri..

Kama mna ushauri pelekeni Umoja Party
Kweli kawabana majizi kwa

●Kodi ya kichwa kwa kila mtanzania over18yrs.
●Tozo za miamala ya fedha na kibenki.
●Tozo za ving'amuzi vya television.
●Tozo za kulipia kodi za majengo kupitia LUKU hata kwa wapangaji.

Kweli majizi tutakoma nchi hii.

Nini kinafanywa na hii mikopo na misaada lukuki tunayopewa kila uchao huko kwenye ufunguzi wa nchi?

Yaliwezekana vipi awamu ya tano na yameshindikana vipi awamu ya sita??
 
Acha upuuzi mkuu,Kila mtu mzima mwenye mapato kuanzia mil.4 na una miaka 18 lazima ulipe Kodi.
 
Atakuwa ni yule mpumbavu alochora jina lake kwenye mawe nchi nzima 2015. Anavaa skafu kwa uzalendo feki
 
Yuko pia waziri wa vito vya thamani amepoteza Kura zote za mama kwa wachimba Vito vya thamani. Mama akitembelea maeneo maeneo ya wachimba vito vya thamani atapokelewa na mabango ya kutisha.
Ana madalali wawili m1 anaitwa Nabi mwingine anaitwa Obuka hawa wanawanyang"anya wananchi maeneo yao kisha wanawauzia Wachina. Kwa ujumla ni madalali wa Wachina. Mama mrekebishe huyo waziri wako
 
Unakuja hapa kutupotezea muda na kujaza server kwa kumung'unya maneno ili itusaidie nini sisi au huyo mama yako?! Kama huna kifua cha kufunguka wafu waelewe baki hukohuko mvunguni mwa kitanda chako huko kwenu Nakapanya! Nonsense.
 
Sasa kama una hili Jambo muhimu kwa Rais Samia na Watanzania kwanini usilianzishie tu Mada ( Uzi) wake mpaka uje hivi Ulichomekee hapa katika huu Uzi wangu?

au kwasababu unajua Rais Samia na Watendaji wake ( hasa Idara zake Nyeti ) nchini huwa wananisoma sana GENTAMYCINE hapa JamiiForums ndiyo ukaona nawe upate Tiketi ya Kusomwa nao kwa msaada wa Lifti ya hii Mada yangu Mahsusi hapa?

Ulichoandika hapa kinachomuhusu huyo Waziri wa hiyo Wizara Dk. Dotto Biteko ( mwana SAUT ) Mwenzangu ( japo nilimuacha miaka Miwili ( 2 ) nyuma Chuoni Mwanza ungeuanzishia Uzi wake ingependeza na kuwa na Manriki halafu hata Mimi ningeunogesha huo Uzi kwakuwa nami pia nina Madhaifu yake kadhaa huyo Waziri huko huko katika hiyo 'Docket' aliyoko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…