Rais Samia: Waliopokea ongezeko la gharama za ununuzi wa ndege ya mizigo waachie nafasi zao watupishe

Rais Samia: Waliopokea ongezeko la gharama za ununuzi wa ndege ya mizigo waachie nafasi zao watupishe

Kwanini awatahadharishe wasile hadi wakavimbiwa.

Kwa akili zako Tanzania hii kuna mfanyakazi anapokea mshahara unamtosha hadi kuvimbiwa?
Kumbe unajua vizuri kwamba aliwaambia wasile hadi wakavimbiwa?

Kula hadi kuvimbiwa maana yake ni kula nje ya kile unachostahili.

Wewe kama umetoka bara huko nahau, misemo ama methali za kiswahili utakuwa nazo mbali sana . Sio kosa lako.

Ungekuwa mwenyeji wa ukanda wa Pwani basi vitu vidogo kama hivi ni rahisi kuvielewa.
 
Yani mkuu watu wanageuza maana ndo wanaona wako sawa. Alimaanisha upate kile ambacho unasitahili kulingana na kazi yako lakini si kwa kuiba mali ya umma.
Sasa usichokielewa kamba zingine ni ndefu kupitiliza maana wote hamuwezi kua na kamba zinazofanana na hapo ndio pesa unapopata sasa, au bado haujaelewa ? Wengine kamba zao sio fupi, shtuka
 
Kumbe unajua vizuri kwamba aliwaambia wasile hadi wakavimbiwa?

Kula hadi kuvimbiwa maana yake ni kula nje ya kile unachostahili.

Wewe kama umetoka bara huko nahau, misemo ama methali za kiswahili utakuwa nazo mbali sana . Sio kosa lako.

Ungekuwa mwenyeji wa ukanda wa Pwani basi vitu vidogo kama hivi ni rahisi kuvielewa.
Wewe lete mipasho hapa ya kichawa chawa usijue fedha za umma zinatapanywa kwa kauli za kijinga kutoka kwa mtu asiyefikiri kabla ya kunena kama mama yenu.
 
CAG ndio whistle blower anaewaamsha hao wengine kuwapa taarifa wakafanye uchunguzi na hatua zichukuliwe ili kuujua ukweli halisi, I'm not layman like you amka huko usingizini unataka waingilie majukumu yasiyowahusu yaan hakuna taarifa ya rushwa TAKUKURU wakaweke mtego ili kukamata Wala rushwa umerogwa au?
Nilikuwa najua una ujinga kidogo kumbe una ujinga mwingi sana.

Narudia hujui majukumu na madhumuni ya kuanzishwa kwa idara ya usalama wa taifa na TAKUKURU.

Nimekuelekeza nenda kasome sheria hizo utaelewa jambo. Kama sheria imekupiga knockout basi tafuta mjuvi wa sheria akusomee nakukutafsiria.

Mimi ni mdaubwa sheria ndiye ninayekwambia kwamba moja ya majukumu ya msingi ya Tiss ama Takukuru ni pamoja na ku detect vitendo vya wizi ama rushwa dhidi ya serikali.

Hujawahi kusikia taarifa ya Takukuru ikisema kwamba "tumefanikiwa kuokoa bilioni 10 ambazo zingetumika kinyume na matumizi kusudiwa"?

Leo Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru katoa taarifa juu ya fedha walizofanikiwa kuokoa ambazo zingetumika kinyume na matumizi tarajiwa.
 
Sasa urefu wa kamba maana yake ni kula nje ya unachostahili?

Mbona Watanzania wengi ni weupe kichwani ku reason mambo?

Ukiajiriwa kama muhasibu halmashauri maana yake ule kwa urefu wa kamba yako kwa mshahara huo usitake kula zaidi ya unachostahili. Simple like that.

Hata ule usemi kwamba "Kila mbuzi anakula kutokana na urefu wa kamba yake" una apply hapa kwasababu kama mbuzi amefungwa kwa kamba fupi atakula majani anayoyafikia tu na yule mwenye kamba ndefu hali kadhalika atakula kingi zaidi.
Sasa kama ni hivyo mbona aliwauliza mbona mnakula mpaka mnavimbewa? maana kama kina kula kwa urefu wa kamba yako hauwezi kula mpaka kuvimbewa,hakuna mshahara wa Serikali ya tanganyika uliwahi kumtoshereza mfanyakazi, wafanyakazi wengi wa Serikali wanaishi kwenye mikopo,hilo la mle lakini msivimbewe bado unaamini lipo kwenye mshahara?
 
Sasa hata wakikaa pembeni ndio Nini watu wameiba pesa za kuweza kununua ndege yakisasa kabisa ya mizigo
 
Kuna watu wameongezeka 110% kwenye gharama za Ununuzi wa Ndege ya Mizigo. Nadhani Sasa Mh. Rais ameanza kuwafahamu Watanzania. Hawa watu msiishie kuwafuta kazi waende mahakamani.

Hii Nchi watu Kuiba ni sehemu ya maisha Yao so kuwasimamia Kwa kuwabembeleza watakutafuna Hadi ukome. Watanzania wanatakiwa kuendeshwa kama punda ndio wanaleta.

Mwisho waboresheeni maslahi Yao pia vinginevyo Kuna syndicate kubwa sana ya wizi.

==============

Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha kuchukizwa na kitendo cha ongezeko la fedha za manunuzi ya Ndege mpya ya mizigo kinyume na fedha ambazo zilikuwepo kwenye mkataba wa awali huku akiwataka Watumishi wa Serikali waliokubali ongezeko hilo bila kuhoji waachie nafasi zao kwakuwa hawana uchungu na fedha za Watanzania.

“Kuna mradi hapa tumetengeneza Ndege ya mizigo ambayo tunakaribia kuipokea, last Installments ilikuwa tulipe dola milioni 37, invoice imekuja dola milioni 86….. unauliza mkataba ulisemaje? hii imetokana na wapi?, ooh vifaa vimepanda bei, vipi? mkataba wetu ulisemaje”

“Na bado aliyepokea anakuletea Serikalini hii ilipwe ndio invoice tumepokea….. stupid, ulipopokea umechukua hatua gani? umeuliza nini? umefanya nini? ukilitazama kwa undani hili ongezeko limeanzia huku ndani kuna Watu wameongea huko”

“Hatuwezi kwenda hivyo na nadhani hawa wanaopokea hizo invoice wakazileta kwa raha zao kabisa Serikalini watupishe, hawafai kuwa kwenye hizo nafasi, kama wanafaa angepokea huko akalihoji”

“Baada ya kuhoji akasema nilipokea hivi, nimeambiwa hivi lakini bado nimeoka tufanye hivi, huyu unamuelewa lakini Mtu anapokea kwa raha zake tu analeta Serikali ‘Kuna hiyo invoice imekuja, vifaa vimeongezeka baada ya covid, pumbavu haiwezekani….. Mawaziri tusaidieni over-invoicing zipo nyingi sana” ——— Rais Samia.

Aisee kuna watu ni wezi jamani

Ndo mna hawa watu wakishakufa mali zao nazo hufa mna huwezi kuendeleza mali ya dhulma na wengine huishia magonjwa ya ajabu tu wakipoteza pesa mahospitalini

Dhulma ni mbaya sanaa

Mifano hai ipo katika jamii zetu tazameni wenyenu

N. b .Tunaishi umri mdogo sana hapa duniani
 
Watanzania tuliowengi tumepokea kwa mshutuko taarifa ya ongezeko la mara mbili na ushee la gharama za kununua ndege yetu ya mizigo.
-Kitendo hiki ni uhujumu uchumi wa hali ya juu na ni ununuzi wa ndege moja.
-Serikali au wananchi walipa kodi watakuwa wamepigwa kiasi gani mpaka tutakaponunua ndege zote 5 kama manufacturer analeta hadithi za spare parts.
-Tunafahamu kuwa ndege inaponunuliwa huwa na package ya spare parts zinazotumiwa mara kwa mara, Je kwenye mkataba huo spare parts hazikuwekwa au manufacturer anazungumzia raw materials za kujenga ndege?
- Serikali ilitoa taarifa Bungeni ni kwamba ndege zinamilikiwa na TGFA (ndege za Serikali) na Air Tanzania wanakodisha toka TGFA.
-Hii ina maana mchakato wa ununuzi unafanywa TGFA na kushirikiana na Hazina au taasisi zingine za Serikali.
-Rais wetu SSH, sisi watanzania tunaimani na wewe na tunaamini unazo taarifa zote kuhusu wahusika wa mchakato wote wa manunuzi.Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa JMT safisha uozo, badala ya kuusafisha nawe unalilia na kutoa matusi, badala ya kuwaondoa wahusika wote na kuwaweka watanzania wengine.wakati uchunguzi na hatua za kisheria zinafuata.

Ushauri
1.Simamisha kazi wahusika wote kupisha uchunguzi wa wahusika wote
2.Tume ya kuchunguza na kupitia mikataba yote ya manunuzi ya ndege zote
3.Majukumu ya TGFA yawe kuendesha ndege za viongozi,
4.Mkataba wa Ukodishaji ndege (TGFA na ATCL) upitiwe upya, badala ya kuwa na minimum fixed charges za ATCL kulipa TGFA, regardless ndege kuwa hewani au kwenye matengenezo (Preventive or routine maintenance).
5.Serikali ilipe madeni ya ATCL (awali) ili kuweka sawa mizania ya ATCL (mpya), ili iweze kukopesheka,na kupunguziwa gharama za uendeshaji, ambazo mwisho wa Mwaka ATCL mpya inaonekana inapata hasara kutokana na utaratibu huu wa taasisi za Serikali kugombea fito wakati zote zinajengae nyumba moja
 
Aisee kuna watu ni wezi jamani

Ndo mna hawa watu wakishakufa mali zao nazo hufa mna huwezi kuendeleza mali ya dhulma na wengine huishia magonjwa ya ajabu tu wakipoteza pesa mahospitalini

Dhulma ni mbaya sanaa

Mifano hai ipo katika jamii zetu tazameni wenyenu

N. b .Tunaishi umri mdogo sana hapa duniani
Usichokitolea jasho hakidumu and so u can't be proud off.
 
Back
Top Bottom